Magumu yamkabiliyo Rais Samia katika awamu ya Sita

brazaj

JF-Expert Member
Jul 26, 2016
27,823
35,829
Mabibi na mabwana ni wazi kuwa awamu ya sita imepokelewa vyema na wapenda haki wote.

Hata hivyo ni wazi kuwa kwa waliokuwa na maslahi yao binafsi katika awamu ya tano, awamu ya sita imekuwa ni mwiba mchungu kweri kweri. Walipo wanatweta hawaamini kuwa hii ni awamu ya sita na bendera ziko milingoti mizima tena.

Miito inapoendelea kusikika kuhamasisha kuungwa mkono kwa awamu ya sita, uwepo kwa watendaji wakereketwa wa awamu ya tano kwenye awamu hii kutaendelea kuwa ni kikwazo kwa mama kwa muda mrefu.

Vipi aliyeshadadia Corona kuwa si ugonjwa bali vita vya kiuchumi tu dhidi ya Tanzania atabadilika ghafla leo na kuiacha busara na sayansi kushika hatamu zake?

Vipi ambaye hakuiona dhuluma ikiwamo ya TRA kwa wananchi atakuwa na msimamo sawa na serikali ya sasa?

Vipi ambaye hakuziona rushwa, urasimu, manyanyaso nk katika awamu ya tano atakuwa na msimamo sawa na serikali ya sasa?

Vipi aliyeshadadia maendeleo fyongo ya kule kwetu atatambua umuhimu wa haki sawa leo?

Vipi walioasisi na kushadadia sheria kandamizi kwenye awamu ile wakawepo kwenye awamu hii?

Vipi hawa akina Kabudi, Majaliwa, Jaffo, Gwajima, Mollel, Mwigulu, Chalamila, nk kwenye waliyokuwa wakiyasimamia yaliyotufikisha huku tunakohitaji kutoka leo?

Vipi watakuwa wa kubatizwa upya? Watakuwa na yapi mapya ya kutwambia leo tofauti na waliyokuwa wanatwambia kule?

Mama safari yake inafanyika kuwa ngumu zaidi kwa kuwapo watendaji wakereketwa 'ma "zealot"' hawa wa awamu ya tano kwenye awamu ya sita.

Tunapolazimika hata kuwataja kwa majina ni katika kuwahimiza kustaarabu tu kuyaweka maslahi ya taifa mbere! Ikiwezekana hata wakapisha kistaarabu tu.

Yaani ni katika kuhimiza kuwepo kwa uzalendo kweri kweri tu.

Au nasema uongo ndugu?

Mungu mbariki mama yetu.

Mungu ibariki Tanzania.
 
Rais anapaswa kuchoka karata zake vizuri tu kama unavyofanya sasa.

Mfano, May Mosi hiyo hapo around the corner, madam anamalizana na wafanyakazi wote wa nchi hii anasubiri nane nane kwa wakulima.

Mama akicheza vizuri mbona mambo yanaenda vizuri tu tena yupo kwenye ground nzuri ya kuweka nchi sawa.

Watanzania wameshamwamini kuwa anaweza kurejesha umoja wa kitaifa ba nadhani ameshafanya pakubwa kwa muda mfupi.
 
Rais anapaswa kuchoka karata zake vizuri tu kama unavyofanya sasa

Mfano, May Mosi hiyo hapo around the corner, madam anamalizana na wafanyakazi wote wa nchi hii anasubiri nane nane kwa wakulima

Mama akicheza vizuri mbona mambo yanaenda vizuri tu tena yupo kwenye ground nzuri ya kuweka nchi sawa

Watanzania wameshamwamini kuwa anaweza kurejesha umoja wa kitaifa ba nadhani ameshafanya pakubwa kwa muda mfupi

Ni kweli mkuu na pia hata kwa kuwaacha serikalini wakereketwa hawa ni moja katika siasa za kuhimiza umoja huo.

Japo hajawaambia watoke. Ilikuwa busara zaidi wakajitoa wao kuliko yeye kuwatoa.

Au nasema uongo ndugu zangu?
 
Rais anapaswa kuchoka karata zake vizuri tu kama unavyofanya sasa.

Mfano, May Mosi hiyo hapo around the corner, madam anamalizana na wafanyakazi wote wa nchi hii anasubiri nane nane kwa wakulima.

Mama akicheza vizuri mbona mambo yanaenda vizuri tu tena yupo kwenye ground nzuri ya kuweka nchi sawa.

Watanzania wameshamwamini kuwa anaweza kurejesha umoja wa kitaifa ba nadhani ameshafanya pakubwa kwa muda mfupi.
Wewe unawaza kuongeza mishahara wakati kuna maelfu ya watu hawana ajira?
 
Yule hayupo tena!! Bali tusonge Mbele, kukaa tunaongelea yeye kila siku ni kuchelewa Tu!!

Sasa tuna Rais mpya ni lazima asimamie anachoamini kitatuvusha
 
Back
Top Bottom