Hodi wanajamvi,
Kwa zaidi ya miaka nimekua mfuatiliaji wa thread mbalimbali jukwa hili na nimejifunza mengi kwenu, naamini kwa busara zenu mtanishauri nini cha kufanya katika hili linalonisibu.
Mwanzoni mwa mwaka huu nilikutana na binti mmoja anasoma chuo uuguzi, nilimpenda na tukaanzisha mahusiano, mimi na huyu mpenzi wangu tulikua tunaishi wilaya moja ila maeneo tofauti hivyo tulikua tunaona wikendi moja kila wiki mbili.Nilimjali na kumthamini kwa kila hali na tukawa na mipango ya kutambulishana nyumbani mara tu atakapohitimu masomo yake.
Ilipofika mwezi wa tano nikaanza kuona mabadiliko, tunapokua naye wikend usiku anapigiwa simu ambazo sizielewi nikimuuliza anasema ni kaka yake. Ilipofika mwezi wa sita nikapata safari ya kikazi kwenda mkoa mwingine kwa kipindi cha miezi miwili, mpenzi wangu alikuja kuniaga nilimuomba simu yake nicheze game nikainstall spy application kwenye simu yake nikaenda zangu safari, kuanzia siku hiyo nikawa napata taarifa za mawasiliano yake.
Kupitia hiyo application niliweza kugundua ana mahusiano na watu wawili mmoja akiwa ni ndugu yake, nilijizuia kumuuliza chochote kwa kipindi cha mwezi mzima ili nikusanye ushahidi vizuri.
Juzi uzalendo ukanishinda nikamuuliza kakataa, nikamtumia baadhi ya sms walizokua wanachat akagoma sio zake, eti rafiki yake alikuwa anatumia simu yake. Nikawabana wote wawili rafiki yake kakubali kua sms sio zake (sms ni za mpenzi wangu), basi nikaamua kuachana nae.
Tatizo ni kuanzia jana ananisumbua turudiane nimegoma anatuma sms za kutishia kujidhuru nifanyejee?
1. Niendelee kukaa kimya nisijibu sms wala simu yake.
2. Nikatoe taarifa polisi.
3. .......
NB: Nimeshaamua SITARUDIANA NAE.