Watetezi mbona wapo wengi. Hujamsikia Kabudi anavyomtetea kwa kueleza walivyokuwa wakiwadanganya Watanzania kuhusiana na trilioni 360?
Hukumsikia wengi wakimtetea kwenye sifa yake ya kudanganya kuwa alikuwa bingwa kwelikweli wa kudanganya kuwa miradi yetu yote tunaijennga kwa pesa yetu kumbe tunakopa?
Hukumsikia CAG alivyomtetea marehemu jinsi marehemu alivyowaaminisha Watanzania kuwa yeye ni mzalendo kumbe alikuwa mwizi, pesa yote ya aliokuwa amebambikizia kesi za uhujumu uchumi, alizitia mfukoni mwake?
Hujo vijijini hukuwasikia watu wakimtetea marehemu kwa kipaji cha uwongo hadi kuwaaminisha wajinga wote kuwa kuna deni la kodi la kampuni moja la kutosheleza kumnunulia kila rai Noah moja wakati kampuni hiyo ilikuwa haina deni hata la shilingi moja?
Watetezi wapo wengi, wengi wanajua kipaji cha marehemu katika uwongo na hadaa, na hakika sijui kama kuna mtu atamfikia hata kwa karne nyingi zijazo. Kudanganya mamilioni ya watu,na watu wakakuamini na kukupigia makofi na kukusifia kwasababu unawadanganya, siyo jambo rahisi. Ni legacy hiyo ya marehemu lazima itetewe kwa nguvu zote ili kumkumbuka marehemu kwa uhalisia wake.
Pia ile sifa yake nyingine kubwa ya ujasiri wa kutenda uovu dhidi ya raia, tena bila woga: kuua, kushambulia, kuteka, kutesa na kuwabambikia watu kesi kisha kuwanyang'anya pesa, na pesa alizowanyanga kuzitia mfukoni mwake bila ya hofu ya kuhojiwa chochote na yeyote. Ule ni ujasiri wa pekee ambao lazima utetewe.
Kuanzisha uzi juu ya mtu huyu ni kama kuchokoza watu na kutaka waendelee kuzungumzia juu ya madendo ya ubaya na uovu wakati wa utawala wake.
Kuhusu utawala wake;
1. Utawaambia nini wafanyakazi kuhusu nyongeza zao za mishahara na kupandishwa madaraja?
2. Utawaambia nini wanasiasa wa vyama vya siasa katika undeshaji wao wa shughuli zao halali za kisiasa.
3. Utawaambia nini wafanyabiashara kuhusu 'task force" yake.
4. Je! Vipi kundi lile la wasiojulikana?
5. Vipi manunuzi ya kile kivuko cha MV. Bagamoyo kugeuzwa kuwa zana ya kijeshi isiyoweza kuhojiwa?
6. Vipi matumizi ya jeshi katika mgogoro juu ya bei ya korosho na kangomba?
7. Vipi kuhusu kuongezeka kwa zigo la deni la taifa huku tukiaminishwa kuwa sisi "dona kantri"
8. Je makinikia na ripoti za Prof. Mruma & Ossoro huku zipigiwa promo na Prof. Kabudi ili kuhalalisha madai ya TZS 360Tn
9. Vipi kuhusu uzalishaji wa wakimbizi na kesi za uchochezi wa kisiasa kutokana na chuki dhidi ya kutopenda kukosolewa?
10. Sakata la MKIRU na vifo vya mamia ya raia na wengine kukutwa katika viroba vikielea baharini.
11. Vipi kuhusu mhimili mmoja kujichimbia chini na athiri hasi za kiutendaji wa mihimili mingine?
12. Yure mupe, yule muruke kwa wakazi wa Kimara na wale waliompigia kura kule Mwanza.
13. Vipi kuhusu mbuga ya Burigi na uhamisho wa hayawani wa mwituni
14. Vipi kuhusu mradi wa ustawishaji wa maendeleo ya Chato!?
15. Vipi kuhusu chafuzi za 2019 na 2020 na ushindi wa kishindo wa chama chake.
Dug! Orodha ni ndefu sana, pengine mengi bado hayafahamiki na wala hajaweza kuwekwa hadharani kutokana na tabia zake za kuminya uhuru wa vyombo vya habari.