Last emperor
JF-Expert Member
- Mar 22, 2015
- 10,352
- 9,810
Imekuwa ni fashion sasa kwa serikali ya magufuli na mawaziri wake kufanya ziara za '' kushtukiza '' Dar tu kwenye media ambapo watapata coverage ya kutosha, ina maana matatizo ya watanzania yapo Dar tu? Alianza Magufuli kwenda bandarini, muhimbili, akafuata majaliwa bandarini, akaja kigwangallah kwa Dr Mwaka, Ummy mwalimu amekosa nitoke vipi na yeye ameamua arudi muhimbili. Hivi hakuna hospital zingine za rufaa Tanzania? Kwanini hawaendi mikoa mingine ambako kuna shida na matatizo mengi zaidi? Au Tanzania ni Dar tu? Utakuja kuona kinachoendelea mpaka sasa hivi ni usanii tu wa kutaka waonekane wanafanya kazi sana kumbe hamna kitu, Ni kuuza sura tu kwenye media kana kwamba matatizo yote ya Tanzania yapo Dar. Msituchoshe!