Magufuli kutaja mafisadi leo mjini Mbeya

Magufuli kutaja mafisadi leo mjini Mbeya

Makapi ni Mafisadi sanaa hawafai katika maendeleo ya tanzania
Kwakuwa wao ni maroho wa madaralka na inchi hii hatutaki watu wa aina hiyo.
tumchague magufuli anatosha katika maendeleo ya nchi hii.
 
Kazi ni kazi tu Dr, wanainchi tunakwuamini.
 
Hatimaye Dr Magufuli, mgombea urais CCM, leo anatarajia kutaja mafisadi mbalimbali wanaokwamisha maendeleo ya wanainchi katika mkutano wake wa kampeni mjini Mbeya katika uwanja wa Sokoine.

Hata hivo anatazamia kuweka wazi mikakati na hatua mbalimbali atakazochukua dhidi ya wahusika katika uongozi wake.

Dr Magufuli ataambatana na majembe wenzake hususani, Fildi Marshal Mwigulu Nchema na Dkt. Harrison Mwakyembe.


Ambapo Mwakyembe aliyekuwa Mwenyekiti wa kamati ya RICHMOND ataueleza umma namna Lowasa alivyoipatia serikali hasara kupitia dili lake la RICHMOND.


Mkutano huu utarushwa live Star Tv, Azam Tv na TBC1 Kuanzia saa na 8-12 leo.
Usikose.

HAPA NI KAZI TU; UMOJA NI USHINDI
we na mwakyembe mnainamishwa
 
Dr wanainch wanakutegemea sana, ushindi wa kishindo umepata.
 
atuambie kwa nini kila mwezi tunaponunua umeme lazima tukatwe tsh. 5,520?

Escrow Tegeta Account mgao wa Stanbick Bank, tutajiwe majina
 
Amtaje hata aliyeuza nyumba za serikali
 
Ajitaje na yeye nyumba za serikali halizowauzia mashemeji zake.


swissme

Yes kabisa, awataje na wanunuzi wa nyumba hizo akiwemo lowassa, hapo ndio maana naona kura yangu nimpe bi mkubwa wa ACT haya majizi lowassa na magufuli sio afadhali
 
Atamtaja Mkapa? Si unafiki huu kwani atatukanwa kila matusi!

Atamtaja Kikwete na Ridhiwani?! Si uongo huu kwani ataondolewa kesho tu kugommbea ili awekwe Membe kwa kisingizio kawa bubu so hawezi kufanya kampeni kumbe ni moyo!

Atajitaja Magufuli mwenyewe kwa kugawa nyumba za serikali nchi nzima?! Atajitaja Mwenyewe kwa wizi wake Wizara ya Ujenzi?!

Atamtaja nani kama sio unafiki tu upuuzi wa kina Makongoro wa kusema Gongo oyee na zipu oyeee?!

Au ndio gia ya kuhadaa watu ili waende uwanjani?!

Tehe teh teh teh.......natumia simu kamanda, ningekugongeaje malike ya kufa mtu.
 
Magufuli si mpumbavu kiasi hicho. Mafisadi ni watu wenye au waliokuwa na madaraka ndani ya serikali ya CCM aliyomo (yeye akiwa mmoja wao). Na anagombea urais kwa tiketi ya chama hicho. Awataje kwenye jukwaa la siasa? Mnafikiri na yeye ni mpumbavu na lofa?
 
Hatimaye Dr Magufuli, mgombea urais CCM, leo anatarajia kutaja mafisadi mbalimbali wanaokwamisha maendeleo ya wanainchi katika mkutano wake wa kampeni mjini Mbeya katika uwanja wa Sokoine.

Hata hivo anatazamia kuweka wazi mikakati na hatua mbalimbali atakazochukua dhidi ya wahusika katika uongozi wake.

Dr Magufuli ataambatana na majembe wenzake hususani, Fildi Marshal Mwigulu Nchema na Dkt. Harrison Mwakyembe.


Ambapo Mwakyembe aliyekuwa Mwenyekiti wa kamati ya RICHMOND ataueleza umma namna Lowasa alivyoipatia serikali hasara kupitia dili lake la RICHMOND.


Mkutano huu utarushwa live Star Tv, Azam Tv na TBC1 Kuanzia saa na 8-12 leo.
Usikose.

HAPA NI KAZI TU; UMOJA NI USHINDI

Naamini atataja mafisad wote papa wa Richmond,Escrow,Meremeta, Radar,Tangold,Kiwira, EPA, Boat ya Dar Bagamoyo,et al! Tunasubiri kwa hamu awataje mmoja baada ya mwingine KWA MAJINA!
 
Ni jambo jema kama kweli atawataja ila asisahau kutaja uuzaji wa nyumba za serekali ulivyosababisha hasara kubwa kwa serekali.
 
Mi Mwanaccm Lakini Naona Hapa Kama Kuna Makosa..Haiwezekani Mwenzako Anazindua Kampeni Zake Na Ni Siku Ambayo Tz Nzima Inahtaji Kusikia Ya Upande Wa Pili Afu Wewe Ukamiliki Matangazo Ya Tv Tena Tv Mojawapo Ikiwa Ya Taifa..Hii Haijakaa Vyema,ila Simaanish Kuwa Ccm Wamefanya Hujuma Au Vyombo Hvo Vinaitumikia Ccm Lakini Lipo Tatizo Hapa Leo Ilitakiwa Iwe Siku Ya Ukawa Tu Kama Ilivokua Ya Ccm Trh 23....!!
#hapakazitu #umojaniushindi
 
Back
Top Bottom