Magufuli anaiga kwenye ilani ya CHADEMA

Magufuli anaiga kwenye ilani ya CHADEMA

His excellence Magufuli atazidi kuwanyamazisha kwa vitendo

yes mshkaji agonge kazi tuu, awe makini asifanye maamuzi magumu yatakayoigharimu nchi coz sisi wapinzani ndio tutapatia kick hapo, awe makini sana na wasaidizi wake wasimuaibishe
 
Hata Mzee Makamba alimshauri hata kama atabuni ya kwake ambayo hayamo katika ilani ya Chama, kama ni kwa nia njema na kwa faida ya Taifa, afanye tu ilimradi Katiba na Sheria ziwe hazijavunjwa. Hata magazeti na mitandao ya kijamii yaweza kutoa ushauri utakaosaidia Taifa kwa kuwa wanaoshauri ni watu kutoka jamii hiyohiyo.
 
Hakika nimefarijika sana kuona Serikali ya CCM imeamua kutekeleza Ilani ya Chadema kwa kuanza Na "Kufuta safari za Nje ya nchi" hakina nimeikubali Chadema.Mie binafsi naamini kufanya hivyo in kuonyesha Serikali ya CCM imeamua kujali Utaifa zaidi kuliko Chama .Ushauri Wa Viongozi Wa Serikali ya CCM wasione aibu kutumia Ilani ya Chadema kwani ndio Ilani ambayo Watanzania itawaondolea Shida zao Na matatizo yaliyoletwa Na Viongozi Wa CCM."VIVA CHADEMA"
 
Anafanya vizuri sana kufanya kazi kwa kuchukuwa mawazo ya Chadema huko ndiyo kukoma kifikra na ni dhahiri hana kinyongo na watanzania,ifike mahali tuonyeshe uzalendo uwe mbele.
 
Pombe alimsikia Lowasa akiwaahidi kigamboni watapanda pantoni bure na yeye akaiga akasema hawatalipia tena pantoni,
vipi ndugu zetu wa kigamboni, pantoni mnapanda bure?
 
Acha ushamba ww,apa tunataka maendeleo2 mambo ya kuigana watajua wenyewe,ko unataka mpaka chadema waingie madalakan ndo yatekelezwe,acha uchama ww,
 
sasa kama akiyafanya na yakaleta tija ktk taifa wewe tatizo lako ni nini??
kwani kila kinachotekelwzwa na rais ni lazima kitoke katika ilani ya chama chake??
kama ni hivo basi page za ilani ya uchaguzi CCM ingekuwa kama Chand ya Biology au zaidi ya hapo,.
Na ili kuonyesha kwamba upinzani sio kukwamisha maendeleo; ACT walimpa ilani yao rais Pombe kuonyesha kwamba hata upinzani una mawazo mazuri kwa lengo la kuletea taifa maendeleo, ,

Magufuli Tuko Pamoja Nawe Katika Kujenga Taifa
 
We subiri uone serikali ya MAGUFULI sio ya ccm tena
 
hilo si kosa hapa namuunga mkono

Na hakika hajasema kama ni kosa ila utagundua Chadema/ukawa ni chama makini na ukiangalia kwa jicho la tatu utagundua ni kama chadema wanaendesha nchi maana kila jambo liliopo kwenye ilani ya chadema basi Magufuli anali fanyia kazi
 
Ndio sio kosa. Ila sasa kwanini ktk kipindi campaign huwa wanawaponda wapinzani kwa kuwaambia kuwa hawana sera na wakati hao hao wakiingia madarakani wanakopi sera za wapinzani. Waache unafiki.
 
M4C aliiga, yamkini huyo jamaa nawakubali CDM zaidi ya li chama lake..
 
Tunachotaka si u ccm wala u Cdm,Tanzania ni moja,kutumia ilani ya cdm au chauma sio ishu,kama ameona yaliyomo yanafaa kutekelezwa.
Nitampongeza zaidi Magufuli endapo baraza lake la mawaziri akiweka wapinzani wenye uwezo mkubwa,ni dhahiri wapo baadhi ya watu wa waupinzani wapo wanafaa kuendana na kasi ya Magufuli
 
Wanachadema huwa hamkosi maneno...

Kama hilo ni wazi walilokuwa nalo wao wakati CCM haikuwa nalo kuna ubaya akisema?Nadhani hajasema kwa ubaya na tutafurahi kama atapitia ikan zote za upinzani aone ni yapi ya msingi ambayo wananchi wanataka na ayatekeleze...kumbuka huwez kujijua kwa kujitathmini mwenyewe pengine ccm walikuwa wa naona ni sawa Rais asafiri kila Leo na ni heshima vigogo kutembelea mashangingi lakini jirani kawakumbusha kuwa hivyo vitu vinadumaza uchumi wa nchi.So Mimi sioni tatizo kwa hilo na huu sio muda wa vijembe na kukosoana.
 
Naitamani sana siku ambayo utaongea kitu cha maana

Usihangaike haiwez kutokea, na hata ikitokea basi tegemea baadae kuona kaandika.. "Jaman akaunti yangu imekuwa hacked.. "

Sabab hata nafsi yake itamsuta kwa kile alichoandika, kwa kutokuamiin kwamba kama ni yeye kwel aliyeandika kitu cha maana.
 
Nenda ukamshitaki!
Thubutu, hao jamaa watabaki kuweweseka tu hapa jamvini. Kipigo cha tarehe 25 Oktoba kilikuwa sio cha mchezo yaani. Sasa wamechanganyikiwa hata wanaloongea hawalijui.
 
Nimesoma ilani ya CHADEMA na kuona mambo yote anayojaribu kuyafanya Magufuli mpaka sasa yapo kwenye ilani ya CHADEMA ya 2015-2020 na wala sijayaona kwenye ilani yake CCM.

View attachment 305632

Alisema serikali ya Magufuli na siyo ya CCM itahakikisha inashirikana na Watanzania katika kuongoza nchi

Hizo ilani Ni ahadi za utajengaje nchi, baada ya uchaguzi kilichokizuri ndicho kizuri kufanywa, ndiyo maana mama Anna alimkabidhi, Rais Magufuli ilani ya ACT achukue anayoona yanafaa ayafanyie kazi.

Kumbe mnapenda mawazo yenu mnayowashaur serikali yapuuzwe!!kisa yenu tu!! Tuweke taifa mbele kwanza,vyama baadaye

Tunampongeza sana Magufuli kutumia Ilani ya Ukawa kwa faida ya Nchi kumbe yule aliyesema wapinzani ni malofa in lofa yeye mbona Rais anatumia ilani yao?

Ni jambo jema na la kuigwa.
Kutenda mambo kwa maslahi ya nchi na sio ya chama.
Na hivi sasa sio mashindano ya ilani ya nani ni bora zaidi bali ni jambo gani lina tija zaidi kwa taifa na wananchi wake.

Afu nimegundua wengi hawajaisoma ilani ya ccm. Jitabu lile linahitaji ujasiri na utulivu wa akili.
 
Back
Top Bottom