Magufuli anaiga kwenye ilani ya CHADEMA

Magufuli anaiga kwenye ilani ya CHADEMA

Hata wewe mtao mada ukiwa na sera nzuri aitumie tu ili mradi tujenge nchi
 
Hivi, kwa nini baadhi yetu tumekaa ki negative attitude!??? Kwani kama chadema wangekamata dola hiyo ilani yao ingetekelezwa ktk nchi gani!???

Hata kama ata copy na ku paste kutoka Mbinguni, watanzania tunataka mabadiliko...

Hapo hakuna ubaya, tubadilike jamani, tuachane na majungu yasiyo na tija.

Tumuunge mkono, maana hakuna namna, hutake husitake, Magufulu ndiyo Rais
 
Hofu ya mtoa uzi ni kwamba JPM asije akatema big G kwa karanga za kuonyeshwa.
 
Huu sio mda wa vijembe na chokochoko za kuonesha nani zaidi, ni wakati wa kuwapa wanachi maisha bora. Haijalishi ni mbinu za nani zinatumika kuwapa hayo maisha bora

heeeee maisha bora tena kama kikwete???
 
Hofu ya mtoa uzi ni kwamba JPM asije akatema big G kwa karanga za kuonyeshwa.
Nawashauri Chadema wachukue hati miliki ya ilani yao 2020. La sivyo wataendela "kuibiwa" kila siku.
 
Kwa manufaa ya Nchi, acha aige tu, tena kama ya ccm ni porojo tupu, aitupe kabisa na kudili na chadema tu
 
huyu ni mwizi wa interlectural material rejea m4c na ilo la ilani.

Anajaribu kujifananisha na upinzan kwa kukosa mvuto kwa ccm.
 
Ile ya ccm si waliiacha katikati ya kampeni wakaenda kutengeneza nyingine waliyodai italeta mabadiliko makubwa? hebu tuisubiri na jopo lao waliliosema la kuwashauri mambo ya kufanya kuleta mabadiliko makubwa!
 
Mbon huwa wansema wapinzani hawana sera? Huku wanzikopi? Waaknowledge basi kwamba hili tunashukuru tumelichukua kwa upinzani!
 
Tunampongeza sana Magufuli kutumia Ilani ya Ukawa kwa faida ya Nchi kumbe yule aliyesema wapinzani ni malofa in lofa yeye mbona Rais anatumia ilani yao?

Nadhani hapo kwenye jambo la ulofa hukumwelewa au umetafsiri vibaya kama viongozi wa ukawa. Mkapa hakutukana watz ila yy alituka viongozi wa ukwa.
 
Mimi ninaamini kwamba Mh. Magufuli akifanikiwa kuuweka U-CCM kando na kisha kuuweka uzalendo mbele atakuwa shujaa wa kila mtanzania. Tatizo la chama cha mapinduzi ni ile hali yao ya kutanguliza maslahi ya chama mbele ya maslahi ya umma. Mfano mzuri ni jinsi walivyoichakachua Rasimu ya katiba ya wananchi. Mh. Rais aweke mbele uzalendo kwa kuchukua mawazo yote bora yatakayonufaisha taifa hili bila kujali yameanzia kwa mpinzani au kwa CCM. akifanya hivyo, historia itamtukuza.
 
Nimesoma ilani ya CHADEMA na kuona mambo yote anayojaribu kuyafanya Magufuli mpaka sasa yapo kwenye ilani ya CHADEMA ya 2015-2020 na wala sijayaona kwenye ilani yake CCM.

View attachment 305632

Kwani tatizo liko wapi?! Kwa taarifa yako correlation ya ilani za vyama mwaka huu ni kubwa sana!! Matatizo ya watanzania ni yaleyale, cdm hawatoi matatizo Congo au Kenya ni yaleyale ya watanzania ambayo rais bora ni lazma ayaaddress na ndo maana ya watanzania 58% kumwamini!!
 
Chadema haikuwa na ikani imecopy na kupaste ya ACT.
 
Mbon huwa wansema wapinzani hawana sera? Huku wanzikopi? Waaknowledge basi kwamba hili tunashukuru tumelichukua kwa upinzani!
Hawa watu ni wanafiki sana.Wana copy na ku-paste sera za wapinzani huku wanakejeli upinzani!!

Ovyo kabisa!!
 
Mimi hiyo ilani ya chadema sijaiona nimeiona ya ccm na act wazalendo lakini ya chadema sijaiona zaidi ya kupiga bla bla kwenye majukwaa
 
Back
Top Bottom