Magufuli: 2017 Mwaka wa Tanzania Mpya

Magufuli: 2017 Mwaka wa Tanzania Mpya

Ndicho atakachofanya sab alishasema ajira na stahiki zake ni kabla ya mwaka wa fedha kuisha
CiZH8WaWgAAdHIC.jpg


chikundi acha vituko, dereva hajui tatizo liko wapi, ya nini kung'ang'ania usukani?​
 
Sheria ya kumuweka ndani anayetamka kwamba Rais atakufa! Kwani sheria za kuwakamata waovu wote wezi, majangili, mafisadi, wanaonunua maboti uozo kwa mabilioni ya fedha, watoa rushwa na wapokea rushwa na wanaosaini mikataba mbali mbali nchi ya kifisadi HAIPO!? Mbona hawa hawakamatwi? Kulikoni?

Kama sheria za nchi zingekuwa zinafuatwa huyu aliyemo ndani ya Ikulu angekuwa lupango sasa hivi au ana kesi kubwa dhidi yake lakini kwa kuwa wanapindisha sheria za nchi mbali mbali sasa hivi katinga Ikulu na uongozi wake wa kulipuka na one man show government.
Ni kweli angekuwa lupango na lowassa wangekuwa manyapara kule jela sasa hivi.
 
Kumbe unajua kama sheria za nchi zinapindishwa eeh! Simamia haki na maslahi ya Tanzania na Watanzania badala ya kupigia makofi sheria za kidikteta dhidi ya raia mbali mbali nchini.

Ni kweli angekuwa lupango na lowassa wangekuwa manyapara kule jela sasa hivi.
 
Twenty sixteen tuliambiwa Tz mpya... Haikuwa hivyo, sasa imekuja twenty seventeen tunaambiwa hivyo, itakuja tena twenty eighteen tutaambiwa tujiandae kwa Tz mpya....!!! Well, tutafika tu!!
 
Wakati tendo linafanyika na wewe umo ndani ya gemu huoni kama timu inafanya vizuri.
Mtajua uzuri wa Magufuli baada ya yeye kuitengeneza Tanzania kwa watanzania wajao. Kizazi hiki kimeishi kwa mazoea muda mrefu hivyo si rahisi kusupporr mtu anayeyaondoa mazoea na kuleta uwajibikaji, ukweli na uhalisia wa maisha.

hayo mazoea yaliletwa na chama gani?

na huyu anayetoa hayo mazoea ametoka chama gani...
ukinijibu kwa ufasaha nakupa soda.
 
Hata kama kaitaja siku ya kufa! Kwani Lema ni Mungu akisema Rais atakufa siku fulani basi ni kweli atakufa siku hiyo!? Acheni kutetea sheria za kidikteta za kuwatia ndani watu ambao hawana hatia yoyote ile. Hivi akitoka ABC akitamka Chikundi atakufa kesho naye atakamatwa!? Kwa sheria ipi!? Ya kutisha kukuua wewe!? Na je kesho ikipita hujafa huyo jamaa kosa lake litafutwa ama litaendelea kuwepo?

Wanaostahili kuwa vifungoni wezi, majangili, mafisadi wanaokwiba mabilioni ya pesa, wanaosaini mikataba ya hawaguswi. Mnaenda kumkama mtu kwa kusema tu Rais atakufa! Nchi hii ina laana ya Mungu kwa manyanyaso ya hali ya juu dhidi ya raia wasio na hatia zozote zile.
Kama hujui viti bora ukawa kama mimi asee,..



Hujui pita tu
 
Viti ndiyo nini!? Kamwe siwezi kuwa kama wewe na ndiyo sababu sikupita kwa sababu najua kinachoendelea hili sakata la TANESCO sikuanza kulifuatilia leo bali tangu wakati wa Net Group Solutions walioingizwa TANESCO na fisadi Mkapa na mtutu wa bunduki huku wafanyakazi wa TANESCO wakiimba nyimbo za kumkumbuka na kumuenzi Baba wa Taifa na wakiwa wamwejawa hasira na wengine wakilia.

Kama hujui viti bora ukawa kama mimi asee,..



Hujui pita tu
 
Kusema tu ni Tz mpya haitoshi, hayo yalisemwa na watangulizi wake lakini hakuna kitu. Ikiwa ni kweli atupe mikakati yake kutufikisha kwenye mabadiliko hayo. Hata maisha magumu na hali inayoendelea sasa ni mabadiliko pia kwa Watanzania
 
Mwaka huu mpya 2017 utakua mwaka wa Tanzania mpya kwa wananchi wa Tanzania, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Dr John pombe Magufuli amewatakia Watanzania wote, wafanyakazi na wafanyabiashara wote
heri ya mwaka mpya wa amani na amesema utakua mwaka mzuri katika huduma mbalimbali na maboresho mbalimbali.

Chanzo: Mtanzania
Sisi watanzania ni watu wa ajabu sana maana huwa tunakuwa watu wakulishwa ahadi kila siku bila kuhoji zinaishiaga wapi
Kwa mfano hatujawahi hoji zimefikia wapi ahadi nyingi za viongozi wetu mfano BRN tuliahidiwa kuwa usimamizi na utekelezaji wa miradi ya maendeleo ungekuwa wa viwango vya kimataifa mata cjui MKURABITA sijui MKUKUTA ungepunguza umaskini..... tena sijui wakadai mahakama ya mafisadi ingefunga mafisadi wote cha kushangaza sahvi tunaambiwa kesi hamna, haya tuliaminishwa kilimo kwanza kingekuwa suluhu ya matatizo yote ya wakulima tz na zaidi ya yote ile ya maisha bora kwa kila mtanzania ila cha kushangza zote hizi ahadi zilipoishia anajua Mungu tu sasa kabla hatujahoji yote hayo bado mnaanza kushkia bango la ahadi ya rais kwa mwaka huu wa 2017.....
Mmmh watanzania kwa kweli inabidi tuwe serious tusiwe watu wa kulishwa kila neno na kumeza..... muulize hta viwanda vmefkia wapi sio mnarukia tu ahadi mpya kila siku bila kuhoji utekelezaji wa za nyuma yake.
 
Back
Top Bottom