Magazeti ya leo yamekosa habari?

Magazeti ya leo yamekosa habari?

bulabo

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2015
Posts
628
Reaction score
783
Magazeti leo ukurasa wa kwanza ni Walimu kupiga wanafunzi tu. Leo yamekosa habari yakuandika nini maana hii ya walimu ndo wameona leo. Mbona hizi habari zipo sana na wanafunzi kuchapwa.

Magazeti yetu jitahidi kuwa mnafuatilia habari msiende na habari zinazoibuliwa nanyinyi jitahdin kuibua story mpya zenye mashiko!! Mkitegemea whatsapp mtafunga magazeti.
 
Nashangaa kabisa,stori ya watafiti wa kilimo waliouwawa kinyama,siyo kupigwa tu,coverage yake kwenye media ilikuwa ndogo sana.
 
Hata Tanzania Daima?
ee7e9c2a_b052_4760_989b_c9a1e865904b.jpg
 
Yani me nilishasahau kusomaga haya magazeti, naonaga ni marudio tu ya nilichoona jana yake kwenye mitandao taarifa za habari usiku
 
That was inhuman........ hatuwezi kuwa na kizazi cha walimu mapompompo watuulie watoto wetu
 
Kutoka kwa DOTTO BULENDU

Toka niione clip ya video ikimuonesha mwanafunzi wa shule ya sekondary huko Mbeya akiadhibiwa na walimu, ambao taarifa zinasema walikuwa kwenye mafunzo ya vitendo,na jinsi jamii ilivyojadili tukio hilo na serikali kutoa tamko lake linalozunguka humu mitandaoni,huu ni uthibitisho tosha kuwa mitandao ya kijamii si kitu kibaya,mitandao ya kijamii ni ulingo mzuri,ukitumiwa ipasavyo utaleta mabadiliko makubwa ndani ya jamii yetu,najiuliza isingekuwa mitandao ya jamii nani angelijua tukio hilo?mitandao ya kijamii kwa mtazamo wangu ina faida kubwa kuliko hasara,"wale unethical social media users"ndiyo tatizo,mitandao yenyewe si tatizo hata kidogo.Nimependa jinsi waziri Mwigulu anavyotumia mitandao siku ya leo kutoa ufafanuzi juu ya tukio hilo,nimependa jinsi waliopo Mbeya wanavyotupa taarifa sahihi,nimeona mpaka barua ya mkuu wa shule husika,kitu ambacho huwezi kiona kwenye vyombo vingi vya habari.Tusiilani na kuitungia sheria mbaya mitandao,tuendelee kupeana elimu juu ya faida ya mitandao ya kijamii katika kusukuma maendeleo.
 
Magazeti leo ukurasa wa kwanza ni Walimu kupiga wanafunzi tu. Leo yamekosa habari yakuandika nini maana hii ya walimu ndo wameona leo. Mbona hizi habari zipo sana na wanafunzi kuchapwa...magazeti yetu jitahidi kuwa mnafuatilia habari msiende na habari zinazoibuliwa nanyinyi jitahdin kuibua story mpya zenye mashiko!! Mkitegemea whatsapp mtafunga magazeti.
Mkuu hiyo ni habari nzito sio kila mtu yupo active na whatsap/Jf kuna watu wanasubiri habari za Magazeti tuu.
 
Magazeti leo ukurasa wa kwanza ni Walimu kupiga wanafunzi tu. Leo yamekosa habari yakuandika nini maana hii ya walimu ndo wameona leo. Mbona hizi habari zipo sana na wanafunzi kuchapwa...magazeti yetu jitahidi kuwa mnafuatilia habari msiende na habari zinazoibuliwa nanyinyi jitahdin kuibua story mpya zenye mashiko!! Mkitegemea whatsapp mtafunga magazeti.
Ndo habari ipo hot
 
Kuna watu ni wamiliki wa magazeti na wana wivu na bakhresa kwa kusifiwa pamoja na kupewa ardhi bure,hata kwenye tv zao jana habari ilikua kiduchu sana,ila ingekua ni wao pengine wangezipa airtime ya kutosha.
 
....yaan habari imeshasambaa nchi nzima wao ndo wanaandika ni bora wangefanya mahojiano na mwanafunzi aeleze kwanini alipigwa
 
Nashangaa kabisa,stori ya watafiti wa kilimo waliouwawa kinyama,siyo kupigwa tu,coverage yake kwenye media ilikuwa ndogo sana.
Jana si walisema KEYBAJAJ AMEHOJIWA POLISI???????????MAGAZET YANAENDANA NA INTEREST ZETU WATANZANIA TUNAPENDA KUSOMA KIPI AU KUSKIA KIPI?
 
Back
Top Bottom