Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 22,455
- 32,981
MAGAMBO MAKONGORO AMEFARIKI DUNIA
Kwa wanaomfahamu Magambo Makongoro amefariki leo hospitali ya muhimbili, maziko kesho Kisutu Alasiri.
Msiba upo nyumbani kwake Msasani opp na nyumba ya Mzee Rais Mwinyi Mikocheni.
Nimepokea taarifa hiyo hapo juu hivi punde.
Magambo tunajuana toka udogo wetu ni mtoto wa Chief Makongoro.
Tulipokuwa shule tukifanya picnic yeye akitupeleka Kigamboni nyumba ya mapumziko iliyokuwa ya Gavana wakati wa ukoloni na kwa wakati ule baada ya uhuru ikawa iko chini ya Mwalimu Nyerere kama Rais wa Tanzania.
Mwalimu alikuwa haitumii nyumba hii na Magambo yeye kwa ule usuhuba uliokuwa baina ya baba yake na Nyerere alikuwa mtoto wa nyumbani State House.
Nakumbuka siku zile hata jina hili la Ikulu lilikuwa bado.
Magambo alikuwa mwenzetu na mchezo wetu ulikuwa mmoja pamoja na Kleist na mdogo wake Ebby, Yusuf Zialor, Wendo Mwapachu, Bubby Bokhari, Christopher Faraj, Abdallah Mohamed Saleh (Tambaza), Abdul Mtemvu, Edward Makwaia (sasa Chief wa Siha), Abdallah Mgambo, Eyshe na Mariam Max, Erica Kisa, Janet Zebedayo, Haitham Rashid, Esther Mzena wenzetu wengine wengi siwakumbuki.
Wenyewe tukijiita Scorpions na wengi tulikuwa wanafunzi St. Joseph's Convent.
Baadhi wemetangulia mbele ya haki.
Miaka ya kati Magambo alikuwa akifanya kazi Inter King iko Mbezi wanafuga kuku.
Mara ya mwisho miaka michache nyuma mwezi wa Ramadhani tulikutana Masjid Ngazija alikuwa na Abraham Sykes.
Nakumbuka siku ile walinishambulia sana kwa kunichangia ati mie najidai sana na Msikiti Ngazija nauona kama mali yangu nikiwaona wao wanakuja kusali pale roho inaniuma.
Haya ndiyo yalikuwa mapenzi yetu tulikutana lazima tubwatizane huku tunacheka.
Nilipoteana na Magambo kwa muda hatujaonana.
Allah amsamehe na amtie Firdaus.
Amin.
Magambo Makongoro
Kwa wanaomfahamu Magambo Makongoro amefariki leo hospitali ya muhimbili, maziko kesho Kisutu Alasiri.
Msiba upo nyumbani kwake Msasani opp na nyumba ya Mzee Rais Mwinyi Mikocheni.
Nimepokea taarifa hiyo hapo juu hivi punde.
Magambo tunajuana toka udogo wetu ni mtoto wa Chief Makongoro.
Tulipokuwa shule tukifanya picnic yeye akitupeleka Kigamboni nyumba ya mapumziko iliyokuwa ya Gavana wakati wa ukoloni na kwa wakati ule baada ya uhuru ikawa iko chini ya Mwalimu Nyerere kama Rais wa Tanzania.
Mwalimu alikuwa haitumii nyumba hii na Magambo yeye kwa ule usuhuba uliokuwa baina ya baba yake na Nyerere alikuwa mtoto wa nyumbani State House.
Nakumbuka siku zile hata jina hili la Ikulu lilikuwa bado.
Magambo alikuwa mwenzetu na mchezo wetu ulikuwa mmoja pamoja na Kleist na mdogo wake Ebby, Yusuf Zialor, Wendo Mwapachu, Bubby Bokhari, Christopher Faraj, Abdallah Mohamed Saleh (Tambaza), Abdul Mtemvu, Edward Makwaia (sasa Chief wa Siha), Abdallah Mgambo, Eyshe na Mariam Max, Erica Kisa, Janet Zebedayo, Haitham Rashid, Esther Mzena wenzetu wengine wengi siwakumbuki.
Wenyewe tukijiita Scorpions na wengi tulikuwa wanafunzi St. Joseph's Convent.
Baadhi wemetangulia mbele ya haki.
Miaka ya kati Magambo alikuwa akifanya kazi Inter King iko Mbezi wanafuga kuku.
Mara ya mwisho miaka michache nyuma mwezi wa Ramadhani tulikutana Masjid Ngazija alikuwa na Abraham Sykes.
Nakumbuka siku ile walinishambulia sana kwa kunichangia ati mie najidai sana na Msikiti Ngazija nauona kama mali yangu nikiwaona wao wanakuja kusali pale roho inaniuma.
Haya ndiyo yalikuwa mapenzi yetu tulikutana lazima tubwatizane huku tunacheka.
Nilipoteana na Magambo kwa muda hatujaonana.
Allah amsamehe na amtie Firdaus.
Amin.
Magambo Makongoro