Kasheshe
JF-Expert Member
- Jun 29, 2007
- 4,694
- 787
Mwandishi Wetu
Daily News; Friday,January 16, 2009 @20:00
JESHI la Polisi mkoani Shinyanga limegundua mafuvu 40 ya binadamu na mifupa mingine katika shimo chini ya mti wa mbuyu.Taarifa iliyotolewa jana na Kamanda wa Polisi wa Mkoa, Shaibu Ibrahim, ilisema mafuvu 35 yaliweza kuhesabika na mengine matano yalikuwa vipande vipande.
JESHI la Polisi mkoani Shinyanga limegundua mafuvu 40 ya binadamu na mifupa mingine katika shimo chini ya mti wa mbuyu.Taarifa iliyotolShaibu Ibrahim, ilisema mafuvu 35 yaliweza kuhesabika na mengine matano yalikuwa vipande vipande.
Ilisema mafuvu hayo yaligundulika Januari 13 mwaka huu saa 10 jioni, mbali kidogo na makazi ya watu katika kijiji cha Mayangi kata
ya Ukenyenge wilayani Kishapu.
Kamanda Ibrahim alisema inaonekana mafuvu hayo yaliwekwa katika eneo hilo kwa muda mrefu bila kutambulika na hata hivyo umri wa binadamu wenye mafuvu hayo haukuweza kujulikana mara moja. Taarifa ya Kamanda huyo ilisema mafuvu hayo yamehifadhiwa kwa ajili ya uchunguzi zaidi, ili kubaini umri na jinsia ya binadamu wanaohusika nayo.
Tukio hilo limejitokeza huku wimbi la mauaji ya maalbino likiwa limeelemea zaidi maeneo ya Kanda ya Ziwa, pia mauaji ya vikongwe ambayo zamani yalisikika sana maeneo ya Shinyanga. Hata hivyo, haijaweza kubainika kama yana uhusiano na mauaji hayo, hadi uchunguzi utakapokamilika na kubaini ukweli.
Pia Kamanda Ibrahimu alisema katika matukio tofauti mkoani humo, watu wawili wamekufa akiwamo mwanafunzi wa darasa la kwanza katika shule ya msingi Butambata, Buya Joel, kwa kutumbukia kwenye kisima wakati akichota maji.
Alisema tukio hilo lilitokea Jumanne iliyopita jioni katika kijiji cha Butambala wilayani Bukombe wakati mwanafunzi huyo akichota maji katika kisima cha nyumbani kwao na polisi wanaendelea na uchunguzi kujua sababu za tukio hilo.
Alisema siku hiyo mchana, katika kijiji cha Nyasubi mjini Kahama, mwanaume mmoja (30-35) aliuawa na wananchi na kuchomwa moto kwa tuhuma za kuwa mwizi wa dirishani.
Katika tukio lingine, Polisi ilifanikiwa kumkamata jambazi sugu aliyekuwa akitafutwa kwa muda mrefu, Mseveni Jonathan (34) mkazi wa Majengo Ushirombo akiwa na risasi mbili za SMG na SAR vikiwa nyumbani kwake Jumatano iliyopita jioni.
Daily News; Friday,January 16, 2009 @20:00
JESHI la Polisi mkoani Shinyanga limegundua mafuvu 40 ya binadamu na mifupa mingine katika shimo chini ya mti wa mbuyu.Taarifa iliyotolewa jana na Kamanda wa Polisi wa Mkoa, Shaibu Ibrahim, ilisema mafuvu 35 yaliweza kuhesabika na mengine matano yalikuwa vipande vipande.
JESHI la Polisi mkoani Shinyanga limegundua mafuvu 40 ya binadamu na mifupa mingine katika shimo chini ya mti wa mbuyu.Taarifa iliyotolShaibu Ibrahim, ilisema mafuvu 35 yaliweza kuhesabika na mengine matano yalikuwa vipande vipande.
Ilisema mafuvu hayo yaligundulika Januari 13 mwaka huu saa 10 jioni, mbali kidogo na makazi ya watu katika kijiji cha Mayangi kata
ya Ukenyenge wilayani Kishapu.
Kamanda Ibrahim alisema inaonekana mafuvu hayo yaliwekwa katika eneo hilo kwa muda mrefu bila kutambulika na hata hivyo umri wa binadamu wenye mafuvu hayo haukuweza kujulikana mara moja. Taarifa ya Kamanda huyo ilisema mafuvu hayo yamehifadhiwa kwa ajili ya uchunguzi zaidi, ili kubaini umri na jinsia ya binadamu wanaohusika nayo.
Tukio hilo limejitokeza huku wimbi la mauaji ya maalbino likiwa limeelemea zaidi maeneo ya Kanda ya Ziwa, pia mauaji ya vikongwe ambayo zamani yalisikika sana maeneo ya Shinyanga. Hata hivyo, haijaweza kubainika kama yana uhusiano na mauaji hayo, hadi uchunguzi utakapokamilika na kubaini ukweli.
Pia Kamanda Ibrahimu alisema katika matukio tofauti mkoani humo, watu wawili wamekufa akiwamo mwanafunzi wa darasa la kwanza katika shule ya msingi Butambata, Buya Joel, kwa kutumbukia kwenye kisima wakati akichota maji.
Alisema tukio hilo lilitokea Jumanne iliyopita jioni katika kijiji cha Butambala wilayani Bukombe wakati mwanafunzi huyo akichota maji katika kisima cha nyumbani kwao na polisi wanaendelea na uchunguzi kujua sababu za tukio hilo.
Alisema siku hiyo mchana, katika kijiji cha Nyasubi mjini Kahama, mwanaume mmoja (30-35) aliuawa na wananchi na kuchomwa moto kwa tuhuma za kuwa mwizi wa dirishani.
Katika tukio lingine, Polisi ilifanikiwa kumkamata jambazi sugu aliyekuwa akitafutwa kwa muda mrefu, Mseveni Jonathan (34) mkazi wa Majengo Ushirombo akiwa na risasi mbili za SMG na SAR vikiwa nyumbani kwake Jumatano iliyopita jioni.