Mafuta ya ubuyu hatari kwa afya

Mafuta ya ubuyu hatari kwa afya

Janga hili Wizara ya Afya imeagizwa kulimaliza haraka kwa kufanya utafiti yakinifu.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Tunawashukuru TFDA kwa tahadhali hii muhimu kulinda afya ya watanzania, lakini wanachelewa sana kuchukua hatua, hivi wanakuwa wapi kufanya uchunguzi wa kina mapema kabla hayajatokea madhara makubwa maana ni wajibu wao, sio mafuta ya ubuyu tu vipo bidhaa nyingi feki. Haya tunaambiwa hata mafuta ya Alizeti (sunflower) si original ni nembo tu ubandikwa! jamani TFDA tusaidieni.
 
Kama ni kweli TFDA ilipaswa itangaze hiii habari mapema, maana kuna watanzania wengi wanatumia haya mafuta na wengine ambao hawajapata hii habari wanaendelea kutumia maana watu huyaamini kutokana na faida nyingi zilizotajwa katika bidhaa hiyo ya mafuta ya ubuyu, wasiishie kwenye maonesho ya 8,8 tu kutoa taarifa hiyo!
 
kuna tetesi ya kwamba hiyo bussiness inatakiwa ichukuliwe na WACHINA.ndio longolongo lolote hili
 
kesho utasikia wachina wameleta mafuta ya ubuyu yalio original, hayana madhara! 🙂 he hehee chezea Bongo wewe.
 
Kwani hawa Jamaa walikuwa wapi siku zote ? Je ni watu wangapi watakuwa Tayari wameathirika na hiyo kansa? Jamani ! kwa hiyo madhara yapo kwenye kunywa 2. vp kuhusu kupaka?
 
tindikali kwa uelewa wangu sijui ndio standard ya elimu yetu ni ndogo mtanielewesha... tindikiali ni acid tu na ubaya wake unategemea na ukali wake kule shule tulikua tunaita concentraion vitu vingi sana hata vya kawaida vina acid(tindikali) ya namna flan... na connection ya acid na kansa imekujaje kwenye mafuta ya ubuyu lakini hawajaiweka iyo connection kwenye vitu vingine.... hata ukila chungwa, ndimu nk vina acid(tindikali) mbona hatuzuiliwi kwa kigezo kama icho unless labda kuna kitu kingine ndio kitaleta kansa na si acid basi waseme!!!
 
NINI KINATAKIWA KIFANYIKE SASA MAANA YALE MAFUTA YANAYOONEKANA YANA USALAMA GHARAMA YAKE IPO JUU?
:embarrassed1:
 
Hhahahahahahhahah inashangaza sana bhana kwani hawa tfda walikuwa wapi kupiga stop hata kabla ya watu kuanza kutumia coz mpaka kitu kuja kutoka magazetin ni tayari watu walishaanza kutumia so sijapata jibu hapo coz watu kibao kama ni kuugua ndo hivyoo washaugua!.
 
Tatizo letu sisi tunapenda kubishana bila sababu yeyote
 
Leo nimesikia kichwa cha habari kwenye nipashe eti mafuta ya alizeti si salama wajua yanavyotengenezwa ngoja nitafute niisome!
 
Hayo ya alizeti yaliyopigwa marufuku ni yale yanyouzwa kiholela mitaani
 
Back
Top Bottom