mafuta ya mbegu za mawese

mafuta ya mbegu za mawese

rugwebe78

JF-Expert Member
Joined
Aug 25, 2013
Posts
265
Reaction score
78
habari zenu wapenz, natumaini mko poa.
naombeni mwenye kujua yanapouzwa mafuta ya mbegu za mawese, nahitaji kuwasiliana na muuzaji kama unauza au una rafiki yako anauza, nipm tuongee biashara. au hata kama unajua yanapouzwa tafadhali nielekeze
 
Haya mafuta Asili yake ni kwetu huko Kigoma
Haya kwa watu wa Kigoma tunayaita Mafuta ya Mise.
Maana kwa lugha uliyotumia hapo juu ukikutana na mtu wa Kigoma lazima akuulize mawese au.
Maana mbegu za Chikichi zinaitwa MISE na mafuta yake ni Mafuta ya Mise.

Nenda Pale magomeni yapo telee.
Kuna Jamaa wa Kigoma wanaduka Kubwa sana la bidhaa zote za kule,Mawezse ,Dagaa wa bichi na wakavu,Samaki wabichi aina ya Migebuka na wakavu pia,maana jamaa wamejipanga kweli,we samaki mbichi wa Kigoma unamla Dar.Na Pia hayo Mafuta ya Mise na mawase yapo..

Ngoja nitakuulizia Jina la mtaa na maeneo waliyopo,maana mie nipo Zanzibar ila asili yangu ni Kigoma na huwa naagiza kwa mdogo wangu ndio anaenda kunichukulia.
 
mkuu, kwa faida ya wengi,
haya mafuta yanamatumizi gani? faida zake nini? etc.. etc

natanguliza shukrani
 
Haya mafuta Asili yake ni kwetu huko Kigoma
Haya kwa watu wa Kigoma tunayaita Mafuta ya Mise.
Maana kwa lugha uliyotumia hapo juu ukikutana na mtu wa Kigoma lazima akuulize mawese au.
Maana mbegu za Chikichi zinaitwa MISE na mafuta yake ni Mafuta ya Mise.

Nenda Pale magomeni yapo telee.
Kuna Jamaa wa Kigoma wanaduka Kubwa sana la bidhaa zote za kule,Mawezse ,Dagaa wa bichi na wakavu,Samaki wabichi aina ya Migebuka na wakavu pia,maana jamaa wamejipanga kweli,we samaki mbichi wa Kigoma unamla Dar.Na Pia hayo Mafuta ya Mise na mawase yapo..

Ngoja nitakuulizia Jina la mtaa na maeneo waliyopo,maana mie nipo Zanzibar ila asili yangu ni Kigoma na huwa naagiza kwa mdogo wangu ndio anaenda kunichukulia.

Mkuu! naomba maelekezo zaidi ya mtaa hapo magomeni yanapopatikana hayo mawese.
 
Ni Rahisi sana kupajua mkuu..
Kama unatokea mjini shuka pale Magomeni Mwembechai,basi ukishuka tu angalia mkono wako wa kushoto kuna Frame imeandikwa kwa maandishi makubwa sana IBITUNGWA,hao ndio wenyewe mpango mzima.Bidhaa zote za Kigoma unapata.
Na hao Kabila lao ni WAHA na asili yao ni Kigoma na pia wanamashamba yao.So is the cheapest and best in town kwa Products za Kigoma.
 
habari zenu wapenz, natumaini mko poa.
naombeni mwenye kujua yanapouzwa mafuta ya mbegu za mawese, nahitaji kuwasiliana na muuzaji kama unauza au una rafiki yako anauza, nipm tuongee biashara. au hata kama unajua yanapouzwa tafadhali nielekeze
Wakaanga chips wote huwa wanatumia mafuta ya mawese ( palm olein) as yapo cheap. Au ww unataka crude?
 
Back
Top Bottom