Taasisi ya Pollicy Data Institute Agosti 15, 2025 imeendesha mafunzo kwa waandishi wa habari nchini Tanzania, yakilenga mbinu za kuandika habari zisizowabagua wanawake, hasa wale wanaojihusisha na siasa. Mafunzo haya ni sehemu ya mradi wa kimataifa unaoitwa Vote Women, unaolenga kuongeza ushiriki wa wanawake katika uongozi na siasa
Kwa mujibu wa Brenda Namata, Meneja wa Programu wa Pollicy Data Institute, mradi wa Vote Women ulianzishwa mwaka 2021 na ulitekelezwa pia nchini Kenya wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2022. Mradi huo uliwasaidia wanawake waliogombea nafasi mbalimbali kukabiliana na changamoto, hususan zile zinazotokana na ubaguzi wa kijinsia
Programu hii ambayo sasa imeanza rasmi Tanzania inawaleta pamoja wanawake waliowahi kugombea nafasi za kisiasa ili kujadiliana, kubadilishana uzoefu na kujua namna ya kukabiliana na changamoto zinazowakabili
Miongoni mwa changamoto zilizotajwa ni pamoja na matusi na lugha za kudhalilisha mitandaoni, upotoshaji wa taarifa na mashambulizi ya kisaikolojia. Mafunzo haya pia yanawapa elimu ya afya ya akili ili kuwasaidia wanawake hao kukabiliana na msongo wa mawazo unaotokana na mashambulizi hayo
Aidha, mafunzo haya yameendeshwa na wataalamu mbalimbali wakiwemo Bonnita Pyamwire, Mkurugenzi wa Utafiti wa Policy Data Institute, na Farati H. Fomily, mkufunzi wa mradi huo
Kwa mujibu wa Brenda Namata, Meneja wa Programu wa Pollicy Data Institute, mradi wa Vote Women ulianzishwa mwaka 2021 na ulitekelezwa pia nchini Kenya wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2022. Mradi huo uliwasaidia wanawake waliogombea nafasi mbalimbali kukabiliana na changamoto, hususan zile zinazotokana na ubaguzi wa kijinsia
Programu hii ambayo sasa imeanza rasmi Tanzania inawaleta pamoja wanawake waliowahi kugombea nafasi za kisiasa ili kujadiliana, kubadilishana uzoefu na kujua namna ya kukabiliana na changamoto zinazowakabili
Miongoni mwa changamoto zilizotajwa ni pamoja na matusi na lugha za kudhalilisha mitandaoni, upotoshaji wa taarifa na mashambulizi ya kisaikolojia. Mafunzo haya pia yanawapa elimu ya afya ya akili ili kuwasaidia wanawake hao kukabiliana na msongo wa mawazo unaotokana na mashambulizi hayo
Aidha, mafunzo haya yameendeshwa na wataalamu mbalimbali wakiwemo Bonnita Pyamwire, Mkurugenzi wa Utafiti wa Policy Data Institute, na Farati H. Fomily, mkufunzi wa mradi huo