Mimi nimesikia njiwa ni ndege wa baraka sana kiasi kwamba
kama una mikosi au nuksi kubwa kubwa huwezi kuwafuga
hapa nazungumzia watu kama wauaji
au wachawi sugu nasikia njiwa hawakai majumbani mwao
au watu wenye kufanya taboo kama kutembea mtu na mzazi wake na kadhalika
Zile mechi za kishule ama mtaani, tukiwa wadogo, nlikuwa ili kuwatisha tu wapinzani, naenda uwanjani na njiwa niliemfunga hirizi mguuni na kumrusha hewani! Ile taharuki ilikuwa burudani tosha
Huwaambia kwa lugha ya Kiswahili tu kwa maneno-taarifa. Kwa mfano: "Jamani hapa kuna tatizo limetokea.Kuna msiba. Ndiyo maan kuna watu wengi na vilio.Msishangae wala kushtuka." Wakati wa kusema hivyo,ni wakati wa kuwapa chakula kwa pamoja ili waje wote mahali fulani
Kukiwa na sherehe je? Maana isije ikawa huwa wakiona mazingira ya watu kuwa wengi katika namna ambayo hawajazoea kuona siku zote wanajificha. Kukiwa na sherehe ambayo nayo huwa inakusanya watu wengi mithili ya msiba, huwa wanakuwaje?
By the way, naamini ulikuwa unafuga kwa ajili ya Biashara na ulikuwa unawauza kama kitoweo. Vipi kuhusu maslahi, ilikuwa inalipa? Changamoto ya biashara hiyo nini, epsecially wanapofikia kwenye idadi kubwa kama hiyo ya 2000, je baadhi yao walikuwa hawapotei na kukusababishia hasara? Kama walikuwa wanapotea, kiwango chao cha kupotea kilikuwaje?
HUYO NJIWA ANAITWA Sir Phillip. Anaumri wamiaka 7, Nimoja kati yawale njiwa 8 nilioanza nao ufugaji. Phillip ndio jina nililompatia ila namwita Sir kwakuwa ndiye njiwa dume mbabe kuliko wengine wote nilionao.