Mafundi uashi wana laana?

Mafundi uashi wana laana?

Ni FUNDI mzuri tatizo lazima ushinde hapo hapo ukitoka tu kashaiba Mimi ni MTU wa tano kumpasua baada ya kugundua kauza cement
Ujenzi ni usimamizi. Usipoangalia kwa kujifanya boss, gharama ya nyumba1 unaweza kuijenga kwa gharama ya nyumba mbili!
Nimeshuhudia jamaa alivyokuwa akiibiwa sementi iliyokwisha changanywa na mchanga tayari.
Alikuwa akifika asubuhi anawauliza mafundi 'leo mnatumia mifuko mingapi?'
Wakisema minne, basi anatoa kiasi hicho, wanachanganya bila kulowanisha na maji kwanza.
Akimaliza zoezi hilo anaridhika na kuamini kasimamia, anaondoka.
Huku nyuma, mafundi wanaanza kuuza sementi iliyokwisha changanywa na mchanga tayari.
Ndoo moja lt10 sh.1000/=.
Anayekuwa akinunua, kama hana ujenzi siku hiyo, basi ana kariba ya kufyatulia matofari, ipo standby.
Akiishakununua ndoo 5, basi anafyatua tofari 5 anazipanga, anasubiri tena.
Mafundi wanahadithi nyingi za kuchefua.
Hawaaminiki na hawastahili malipo ya kuaminiana kabla hajakufanyia kazi na kumaliza. Halafu usimamizi unatakiwa uwe tight na wa akili.
 
Mimi ndo sipendagi mambo haya ya kununuliwa materials na boss, nkija site kwako nakupigia total materials and cost plus na hela yangu ya kazi. Then nanunua hayo materials as per estimation afu wewe unakua na store keeper wako kuhakikisha kilichokadiriwa ndo kimenunuliwa then unanilipa pesa yangu, ndo raha ya kufanya kazi na mafundi wenye mitaji yao na taaluma zao.Mtafute Fundi Wa namna hii hakika hutojutia
Huko ni kujiaminisha tu.
Ukanunue vifaa wewe fundi, mimi nina uboss gani kushindwa kwenda madukani kununua kwa kufuata mkadirio wako?
Nani asiyejua unaponunua mzigo mkubwa kwenye maduka kuna disscount kubwa pia?
Hiyo disscount unapotoka manunuzi unaweza kuja kunipa taarifa?
Halafu nisipokusimamia, unaweza kufuata taratibu za uchanganyaji wa ratio inayotakiwa?
Mimi nadhani kusimamiana ni jambo la heri sana katika suala zima la ujenzi.
Kama hauna hila kwanini usipende kusimamiwa ili kuondoa majungu?
 
Hi great thinkers.
Leo mchana nimejikuta namtamkia fundi uashi nanukuu "hivi wewe una laana?" akanijibu mbovu nikampa vitasa kadhaa mdomoni. Hivi sasa kavimba mdomo eti kaenda kunishitaki nimemvimbisha mdomo Kwa ngumi.

Tatizo kala 3/4 ya pesa yote halafu anakuja site anashinda kilabuni. Cement kila mara anakuja eti imeisha kumbe anauza.

Si chini ya mafundi wanne wameniliza
Leo mbwaimbwai nitahakikisha uso unachakaa.
Hivi huwa wana laana?
Mi siwaelewi.
ukome,kuna kampuni za Ujenzi wake tenda ukae usubiri nyumba,padri anakula madhabahuni unataka Fundi akale wapi?
 
Mimi ni mtumishi muda mwingi nakuwa job ndo chance ya kunitia hasara pesa yenyewe ninekopa bank nipate Kwa kujihifadhi na wanangu halafu unaleta uhuni wa kijinga akipona nampasua tena makusudi

Aisee huwezi kujenga kistaff kwa kumtegemea fundi. Kama uko bize job na unajenga kwa kuungaunga toa tenda kwa mtu unayemwamini akusimamie. Ila ujue lazima umlipe, hata kama ni ndugu yako. La sivyo na yeye atakupiga tu.

Na pia funga kamera site. Kuna kamera wireless za kutumia betri unaweka hata kwenye mti inakaa unaona kinachoendelea live. Itakusaidia kuona wizi wa sementi na usanii mwingine unaoendelea site.
 
Aisee huwezi kujenga kistaff kwa kumtegemea fundi. Kama uko bize job na unajenga kwa kuungaunga toa tenda kwa mtu unayemwamini akusimamie. Ila ujue lazima umlipe, hata kama ni ndugu yako. La sivyo na yeye atakupiga tu.

Na pia funga kamera site. Kuna kamera wireless za kutumia betri unaweka hata kwenye mti inakaa unaona kinachoendelea live. Itakusaidia kuona wizi wa sementi na usanii mwingine unaoendelea site.
Bei zipo wapi
 
Huko ni kujiaminisha tu.
Ukanunue vifaa wewe fundi, mimi nina uboss gani kushindwa kwenda madukani kununua kwa kufuata mkadirio wako?
Nani asiyejua unaponunua mzigo mkubwa kwenye maduka kuna disscount kubwa pia?
Hiyo disscount unapotoka manunuzi unaweza kuja kunipa taarifa?
Halafu nisipokusimamia, unaweza kufuata taratibu za uchanganyaji wa ratio inayotakiwa?
Mimi nadhani kusimamiana ni jambo la heri sana katika suala zima la ujenzi.
Kama hauna hila kwanini usipende kusimamiwa ili kuondoa majungu?
Mimi siyo local fundi, Mimi ni contractor, civil engineer as well as building materials supplier.Kuna aina mbili za kufanya kazi , forced account ile ambayo unamnunulia mjenzi wako materials yote alafu yeye anakufanyia kazi as per your estimation hivo vifaa vikiisha itamlazimu kukusubiria wewe mwenye kazi ukampatie.

Aina nyingine ni full contract hapa wewe ni kumpa Fundi mchoro na kukubaliana bei afu yeye anakukabidhi jengo lako, ila hapa lazima uwe na consultant Wa kusimamia na kuhakikisha kuwa kazi inafanyika as per agreed specifications.Na hii ni njia wanatumia watu wenye pesa zao na wale ambao kidogo wanaona mbali.

Turudi kwako, wewe kama siyo mhandisi knowledge ya kusimamia standards za jengo huna, hivo hata kama ukiwa site zaidi utakua unasimamia usiibiwe materials.

Mtizamo wangu katika hili.

1.Watu wanipenda wajenge nyumba kubwa na za thamani kwa kutumia bei ndogo i.e kutumia mafundi wasoeleweka ilimradi tu wabane gharama ilihali ana project kubwa in hand, matokeo yake ni kucheleweshewa kazi, kucheleweshewa muda,kubadili mafundi kila Mara , pengine hata kuharibiwa kazi. Hapa Nina mfano hai, Nina client wangu mmoja anataka nimjengee ghorofa bila kutumia ramani, bila michoro ya Chuma, bila vibali vya manispaa eti anataka asevu cost, hili binafsi nimelikataa .

Kuna tendency ya watu kuogopa Ku hire expertise mfano engineer ,technician au architect kwa kukariri eti wana gharama without even consulting one.

N.B Honesty is an expensive thing ,do not expect it from cheap things.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom