Mizizi
JF-Expert Member
- Mar 8, 2008
- 1,275
- 391
Tunasikitika sana kutamka haya lakini imefika wakati wa kusema. Kisiwa cha Mafia tumekua wanachama na wapenzi wa ccm, na tumekuwa tukiichagua wakati wote wa uhai wake. Pamoja na chama hiki kukipenda na kuendelea kukiunga mkono, hali imekuwa tofauti na matarajio yetu kwa nusu karne sasa. Kisiwa hichi kimekosa barabara nzuri, hakuna kiwanja cha ndege bora, usafiri wa majini sio wa kuridhisha, hakuna shule bora, zilizopo zote ni za kidato cha nne, hospitali mbaya, hata sekta ya uvuvi nayo imesahaulika. Pamoja na hayo yote, kisiwa cha mafia tumesahaulika hata kwenye kugawa keki ya taifa, kwani hakuna kiongozi aliyewahi kuteuliwa nafasi yeyote ile kama ya ukurugenzi, U-DC, RC, hata makatibu wa chama ngazi yoyote ile tangu uhuru mpaka sasa, si kama mafia hakuna walio na sifa zinazofanana na wateule tuliowahi kuwa nao au tulio nao, ila ni kutokana na kudharauliwa na viongozi wote waliowahi kutawala nchi hii, pia kutokana na upole wetu na kutoonyesha kuleta upinzani kwa chama hiki.
Nadhani sasa umefika wakati wa kujibu mapigo kwa vitendo kwa ccm kwamba, dharau na hila zote tulizovumilia sasa inatosha. Tumetengwa vya kutosha, tumebaguliwa inatosha, hali tulikuwa nayo inasikitisha. Kama ccm si mshirika wetu wa dhati na kweli, ni muda sasa wa kujivua kutoka kwao. Haiwezekani wilaya ya mafia pamoja na kuwa na idara ya maji tangu kuanzishwa kwake, ni kijiji kkimoja tu ndicho chenye maji yanayozalishwa na idara hiyo, ni vijiji viwili tu ndivyo vyenye umeme tangu uunganishwe miaka ya sabini. Zao la nazi tunalotegemea limesahaulika, hakuna kiwanda cha kusindika mafuta ya nazi sasa, hakuna soko la uhakika, hakuna usafiri wa uhakika wa kusafirishia nazi hizo, hakuna anayeshughulikia hilo, hakuna hata ahadi juu ya hilo.
Hayo machache, nitaleta zaidi.
Nadhani sasa umefika wakati wa kujibu mapigo kwa vitendo kwa ccm kwamba, dharau na hila zote tulizovumilia sasa inatosha. Tumetengwa vya kutosha, tumebaguliwa inatosha, hali tulikuwa nayo inasikitisha. Kama ccm si mshirika wetu wa dhati na kweli, ni muda sasa wa kujivua kutoka kwao. Haiwezekani wilaya ya mafia pamoja na kuwa na idara ya maji tangu kuanzishwa kwake, ni kijiji kkimoja tu ndicho chenye maji yanayozalishwa na idara hiyo, ni vijiji viwili tu ndivyo vyenye umeme tangu uunganishwe miaka ya sabini. Zao la nazi tunalotegemea limesahaulika, hakuna kiwanda cha kusindika mafuta ya nazi sasa, hakuna soko la uhakika, hakuna usafiri wa uhakika wa kusafirishia nazi hizo, hakuna anayeshughulikia hilo, hakuna hata ahadi juu ya hilo.
Hayo machache, nitaleta zaidi.