Mafia: Tumeibeba sana CCM sasa tutaiacha rasmi

Mizizi

JF-Expert Member
Mar 8, 2008
1,275
391
Tunasikitika sana kutamka haya lakini imefika wakati wa kusema. Kisiwa cha Mafia tumekua wanachama na wapenzi wa ccm, na tumekuwa tukiichagua wakati wote wa uhai wake. Pamoja na chama hiki kukipenda na kuendelea kukiunga mkono, hali imekuwa tofauti na matarajio yetu kwa nusu karne sasa. Kisiwa hichi kimekosa barabara nzuri, hakuna kiwanja cha ndege bora, usafiri wa majini sio wa kuridhisha, hakuna shule bora, zilizopo zote ni za kidato cha nne, hospitali mbaya, hata sekta ya uvuvi nayo imesahaulika. Pamoja na hayo yote, kisiwa cha mafia tumesahaulika hata kwenye kugawa keki ya taifa, kwani hakuna kiongozi aliyewahi kuteuliwa nafasi yeyote ile kama ya ukurugenzi, U-DC, RC, hata makatibu wa chama ngazi yoyote ile tangu uhuru mpaka sasa, si kama mafia hakuna walio na sifa zinazofanana na wateule tuliowahi kuwa nao au tulio nao, ila ni kutokana na kudharauliwa na viongozi wote waliowahi kutawala nchi hii, pia kutokana na upole wetu na kutoonyesha kuleta upinzani kwa chama hiki.
Nadhani sasa umefika wakati wa kujibu mapigo kwa vitendo kwa ccm kwamba, dharau na hila zote tulizovumilia sasa inatosha. Tumetengwa vya kutosha, tumebaguliwa inatosha, hali tulikuwa nayo inasikitisha. Kama ccm si mshirika wetu wa dhati na kweli, ni muda sasa wa kujivua kutoka kwao. Haiwezekani wilaya ya mafia pamoja na kuwa na idara ya maji tangu kuanzishwa kwake, ni kijiji kkimoja tu ndicho chenye maji yanayozalishwa na idara hiyo, ni vijiji viwili tu ndivyo vyenye umeme tangu uunganishwe miaka ya sabini. Zao la nazi tunalotegemea limesahaulika, hakuna kiwanda cha kusindika mafuta ya nazi sasa, hakuna soko la uhakika, hakuna usafiri wa uhakika wa kusafirishia nazi hizo, hakuna anayeshughulikia hilo, hakuna hata ahadi juu ya hilo.
Hayo machache, nitaleta zaidi.
 
poleni sana.hata hivyo hamjachelewa.kama kweli muna nia basi naamini mtakiunga mkono chama mbadala CHADEMA ili ikifika 2015 ishinde kwa kishindo.
 
wazee wa Bweni mpooo?? Wazee wa Kanga mpooo??? Watu wa far north esp Bweni kwa Dk. Dau wa NSSF nawafagilia sana! Kuku wako manati ya nini?? Poleni maana imewachukua muda kutambua ukweli kwamba CCm is now for tycoons not you wakwea nazi na wavuvi!!
 
Tangazeni kujitenga na tanzania,muhamie comoro mtapata maendeleo!sijawahi sikia kiongozi yeyote kutembelea huko
 
sio nyinyi tu,angalieni hali za sehemu zote wanaojifanya royal kwa CCM!! Tafakari,chukua hatua!
 
Duuu,ni kweli Jamani,nimeshawahi kufika Mafia sehemu inaitwa Kilindoni na Chole,hali ni tete saaaaana,Maisha ni duni mno,kweli wamewekwa pembezoni kama sio kutengwa!!
Tia bidii mkuu kuwaamsha wengine huko!!
 
Tumevumilia tumeshindwa, Mbunge wa kipindi flani alitangaza nia ya kujitenga wakamzima. Sasa nadhani tunahitaji kufikiria upya hilo. Kwani rasilimali tunazo, kama bahari nzuri kwa uvuvi, fukwe nzuri kwa utalii, tuna gesi kama songo songo, zao la nazi, korosho na mabonde mazuri ya kilimo pamoja na kina cha maji ya kutupatia bandari nzuri.
Kwani tumechoshwa na unyonyaji na dharau!
Kwa sasa hakuna kiongozi yeyote wa chama hapa mafia anayejishughulisha na mambo ya chama, kwani hata hao viongozi wa chama wamekosa hata hoja za kuwajibu wananchi kwa sasa, kwani ahadi zimejirudia mara nyingi bila utekelezaji, sasa imebaki stori tu. Hata huyo mbunge wa Mafia amekosa hata usema huko bungeni, nadhani nyinyi ni mashahidi, inawezekana hata kumfaham hamumfahamu. Viongozi wa serikali ya ccm wamedhurumu maeneo ya ardhi za walalahoi wa mafia na kuuzia wawekezaji uchwara, sas ni migogoro ya ardhi ndio urithi wao, kuna kijiji kimoja nilitembelea na kuambiwa wanakijiji wote wameshitakiwa kwa kosa la uvamizi wa eneo. Karibuni mtasikia yaliyotokea huko tarime yakitokea mafia. Kwa sasa ni wakati mzuri sana kwa chama kinachohitaji kuungwa mkono kufika mara moja, kwani wananchi kwa kweli wamekata tamaa
 
poleniiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii
 
Tunasikitika sana kutamka haya lakini imefika wakati wa kusema. Kisiwa cha Mafia tumekua wanachama na wapenzi wa ccm, na tumekuwa tukiichagua wakati wote wa uhai wake. Pamoja na chama hiki kukipenda na kuendelea kukiunga mkono, hali imekuwa tofauti na matarajio yetu kwa nusu karne sasa. Kisiwa hichi kimekosa barabara nzuri, hakuna kiwanja cha ndege bora, usafiri wa majini sio wa kuridhisha, hakuna shule bora, zilizopo zote ni za kidato cha nne, hospitali mbaya, hata sekta ya uvuvi nayo imesahaulika. Pamoja na hayo yote, kisiwa cha mafia tumesahaulika hata kwenye kugawa keki ya taifa, kwani hakuna kiongozi aliyewahi kuteuliwa nafasi yeyote ile kama ya ukurugenzi, U-DC, RC, hata makatibu wa chama ngazi yoyote ile tangu uhuru mpaka sasa, si kama mafia hakuna walio na sifa zinazofanana na wateule tuliowahi kuwa nao au tulio nao, ila ni kutokana na kudharauliwa na viongozi wote waliowahi kutawala nchi hii, pia kutokana na upole wetu na kutoonyesha kuleta upinzani kwa chama hiki.
Nadhani sasa umefika wakati wa kujibu mapigo kwa vitendo kwa ccm kwamba, dharau na hila zote tulizovumilia sasa inatosha. Tumetengwa vya kutosha, tumebaguliwa inatosha, hali tulikuwa nayo inasikitisha. Kama ccm si mshirika wetu wa dhati na kweli, ni muda sasa wa kujivua kutoka kwao. Haiwezekani wilaya ya mafia pamoja na kuwa na idara ya maji tangu kuanzishwa kwake, ni kijiji kkimoja tu ndicho chenye maji yanayozalishwa na idara hiyo, ni vijiji viwili tu ndivyo vyenye umeme tangu uunganishwe miaka ya sabini. Zao la nazi tunalotegemea limesahaulika, hakuna kiwanda cha kusindika mafuta ya nazi sasa, hakuna soko la uhakika, hakuna usafiri wa uhakika wa kusafirishia nazi hizo, hakuna anayeshughulikia hilo, hakuna hata ahadi juu ya hilo.
Hayo machache, nitaleta zaidi.

Hamna lolote ni UJINGA TU!!! Subirini GATI lenu na huo uwanja wa ndege mnaojengewa...
 
Tunasikitika sana kutamka haya lakini imefika wakati wa kusema. Kisiwa cha Mafia tumekua wanachama na wapenzi wa ccm, na tumekuwa tukiichagua wakati wote wa uhai wake. Pamoja na chama hiki kukipenda na kuendelea kukiunga mkono, hali imekuwa tofauti na matarajio yetu kwa nusu karne sasa. Kisiwa hichi kimekosa barabara nzuri, hakuna kiwanja cha ndege bora, usafiri wa majini sio wa kuridhisha, hakuna shule bora, zilizopo zote ni za kidato cha nne, hospitali mbaya, hata sekta ya uvuvi nayo imesahaulika. Pamoja na hayo yote, kisiwa cha mafia tumesahaulika hata kwenye kugawa keki ya taifa, kwani hakuna kiongozi aliyewahi kuteuliwa nafasi yeyote ile kama ya ukurugenzi, U-DC, RC, hata makatibu wa chama ngazi yoyote ile tangu uhuru mpaka sasa, si kama mafia hakuna walio na sifa zinazofanana na wateule tuliowahi kuwa nao au tulio nao, ila ni kutokana na kudharauliwa na viongozi wote waliowahi kutawala nchi hii, pia kutokana na upole wetu na kutoonyesha kuleta upinzani kwa chama hiki.
Nadhani sasa umefika wakati wa kujibu mapigo kwa vitendo kwa ccm kwamba, dharau na hila zote tulizovumilia sasa inatosha. Tumetengwa vya kutosha, tumebaguliwa inatosha, hali tulikuwa nayo inasikitisha. Kama ccm si mshirika wetu wa dhati na kweli, ni muda sasa wa kujivua kutoka kwao. Haiwezekani wilaya ya mafia pamoja na kuwa na idara ya maji tangu kuanzishwa kwake, ni kijiji kkimoja tu ndicho chenye maji yanayozalishwa na idara hiyo, ni vijiji viwili tu ndivyo vyenye umeme tangu uunganishwe miaka ya sabini. Zao la nazi tunalotegemea limesahaulika, hakuna kiwanda cha kusindika mafuta ya nazi sasa, hakuna soko la uhakika, hakuna usafiri wa uhakika wa kusafirishia nazi hizo, hakuna anayeshughulikia hilo, hakuna hata ahadi juu ya hilo.
Hayo machache, nitaleta zaidi.
Wajinga sana nyie. Mlifikiri CCM wajomba zenu wale wawaletee haki zenu kwenye kisahani!!??
 
Wajinga sana nyie. Mlifikiri CCM wajomba zenu wale wawaletee haki zenu kwenye kisahani!!??

Kutuita wajinga mnakosea sana, kwani kila mtu alizaliwa na ujinga, akaelimishwa ndio akelewa, akawa mwelewa, sasa kama waelimishaji wanabagua sehem za kwenda tutajua vipi haki zetu? Nadhni si vyema ukatuita wajinga kisha kisha ukaishia hapo hapo, inawezekana wewe ni mjinga zaidi na ndio maana huna cha kutuelimisha, acha wanaoweza kutuonyesha njia, tena acha kabisa kuchezea hisia za watu, watu tuna uchungu sana na umasikini wetu, kama wewe ulisomeshwa kwenye shule za kuondoa ujinga moja kwa moja kaa kimya, sisi tunaongea tumesoma kwenye shule za kata, tumemaliza na bado ujinga tunao, na hatukupenda kuwa wajinga, mazingira ndio yametulazimisha!
 
Hamna lolote ni UJINGA TU!!! Subirini GATI lenu na huo uwanja wa ndege mnaojengewa...

Inaonekana wewe huijui Mafia vizuri, mimi nanaishi hapa maisha yangu yote, Uwanja wa ndege sio kipaumbele cha mwananchi wa mafia, kwani hata ukikamilika hautaleta mabadiliko yoyote kwa mwananchi wa kawaida. Kwani hakuna mvuvi au mkulima ama mpanda minazi wa mafia anayeweza kulipa nauli ya kusafiri kwa ndege ama kutumia ndege kusafirisha samaki kupeleka ferry kuuza ama nazi na ng'onda kupeleka dar na kwengineko kuuza.
Kwa taarifa yako, hilo gati halikuanza leo, ni miaka mingi linajengwa na halijakamilika, na hata likikamilika story haitakuwa kama inavyotarajiwa, kwani umbali wa mafia hadi dar kwa vyombo vya baharini ni Notiko miles 180 hii ni kujumlisha na mzunguuko wa miamba yote, imagine nauli itakuwa shilingi ngapi ikiwa znz to dar ni notiko miles 47 na ni almost 30ths?
 
Inaonekana wewe huijui Mafia vizuri, mimi nanaishi hapa maisha yangu yote, Uwanja wa ndege sio kipaumbele cha mwananchi wa mafia, kwani hata ukikamilika hautaleta mabadiliko yoyote kwa mwananchi wa kawaida. Kwani hakuna mvuvi au mkulima ama mpanda minazi wa mafia anayeweza kulipa nauli ya kusafiri kwa ndege ama kutumia ndege kusafirisha samaki kupeleka ferry kuuza ama nazi na ng'onda kupeleka dar na kwengineko kuuza.
Kwa taarifa yako, hilo gati halikuanza leo, ni miaka mingi linajengwa na halijakamilika, na hata likikamilika story haitakuwa kama inavyotarajiwa, kwani umbali wa mafia hadi dar kwa vyombo vya baharini ni Notiko miles 180 hii ni kujumlisha na mzunguuko wa miamba yote, imagine nauli itakuwa shilingi ngapi ikiwa znz to dar ni notiko miles 47 na ni almost 30ths?


Wewe ndio huijui Mafia. Kwa nini Bulji amepata ubunge tena Mafia kama sio Gati na Uwanja wa ndege tena kwa ahadi kuwa airport itapeleka barabar ya lami mpaka Utende!!!?? Mbona nyumba za barabarani kwenda Utende zote zimepigwa alama kwamba zitafisdiwa kwa ajili ya Barabara ya Lami kwenda Utende?
Gati tayari mmeshaanza jengewa na karibu litamalizika, au unataka niaattach picha hapa?
 
Tunasikitika sana kutamka haya lakini imefika wakati wa kusema. Kisiwa cha Mafia tumekua wanachama na wapenzi wa ccm, na tumekuwa tukiichagua wakati wote wa uhai wake. Pamoja na chama hiki kukipenda na kuendelea kukiunga mkono, hali imekuwa tofauti na matarajio yetu kwa nusu karne sasa. Kisiwa hichi kimekosa barabara nzuri, hakuna kiwanja cha ndege bora, usafiri wa majini sio wa kuridhisha, hakuna shule bora, zilizopo zote ni za kidato cha nne, hospitali mbaya, hata sekta ya uvuvi nayo imesahaulika. Pamoja na hayo yote, kisiwa cha mafia tumesahaulika hata kwenye kugawa keki ya taifa, kwani hakuna kiongozi aliyewahi kuteuliwa nafasi yeyote ile kama ya ukurugenzi, U-DC, RC, hata makatibu wa chama ngazi yoyote ile tangu uhuru mpaka sasa, si kama mafia hakuna walio na sifa zinazofanana na wateule tuliowahi kuwa nao au tulio nao, ila ni kutokana na kudharauliwa na viongozi wote waliowahi kutawala nchi hii, pia kutokana na upole wetu na kutoonyesha kuleta upinzani kwa chama hiki.
Nadhani sasa umefika wakati wa kujibu mapigo kwa vitendo kwa ccm kwamba, dharau na hila zote tulizovumilia sasa inatosha. Tumetengwa vya kutosha, tumebaguliwa inatosha, hali tulikuwa nayo inasikitisha. Kama ccm si mshirika wetu wa dhati na kweli, ni muda sasa wa kujivua kutoka kwao. Haiwezekani wilaya ya mafia pamoja na kuwa na idara ya maji tangu kuanzishwa kwake, ni kijiji kkimoja tu ndicho chenye maji yanayozalishwa na idara hiyo, ni vijiji viwili tu ndivyo vyenye umeme tangu uunganishwe miaka ya sabini. Zao la nazi tunalotegemea limesahaulika, hakuna kiwanda cha kusindika mafuta ya nazi sasa, hakuna soko la uhakika, hakuna usafiri wa uhakika wa kusafirishia nazi hizo, hakuna anayeshughulikia hilo, hakuna hata ahadi juu ya hilo.
Hayo machache, nitaleta zaidi.

Dunia nzima hawaitaki ccm!
 
Wewe ndio huijui Mafia. Kwa nini Bulji amepata ubunge tena Mafia kama sio Gati na Uwanja wa ndege tena kwa ahadi kuwa airport itapeleka barabar ya lami mpaka Utende!!!?? Mbona nyumba za barabarani kwenda Utende zote zimepigwa alama kwamba zitafisdiwa kwa ajili ya Barabara ya Lami kwenda Utende?
Gati tayari mmeshaanza jengewa na karibu litamalizika, au unataka niaattach picha hapa?

Unaweza kuthibitisha ni mwananchi gani aliyelipwa fidia ya nyumba yake kwa upanuzi wa barabar? Waweza kunitajia hiyo pesa ipo kwenye bajeti ya serikari ipi? Na ahadi ilitolewa wakati gani? Au na wewe unataka kusema hujui janja ya ccm kupata kura? Unakumbuka mbunge kimbau aliahidi kujenga bara bara kwa mchanga kutoka Ulaya, ilijengwa? Hizo ni siasa tu. Kwani kutiwa X nyumba za kando kando ya bara bara ndio kujengwa barbara? Angalia ilani ya ccm 2005- 2010 ilisema waislamu watapatiwa mahakama ya kadhi, ipo wapi? Pia ilisema kila wilaya itajengewa chuo cha veta, muda umepita, mafia kipo wapi? Balleni? Kilindoni? Chole? Malimbani? Utende? Au kirongwe na jojo?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom