Kwani ni wewe na nani mnasema hivyo? Au ni wewe mizizi tu? Na bado.....!
wewe mzizi ndio asili. tawi linaweza kukatwa au kuhamishwa huyo ni mwana mafia halisi.
Kwani ni wewe na nani mnasema hivyo? Au ni wewe mizizi tu? Na bado.....!
Bw mzizi, ahsante kwa kutujuza mimi nilikuwa sinalo hilo,ila mafia mmbunge tuliyenaye ni mbumbumbu,ki upeo hata uwezo wa akili yake,analaghai kwa salam alykum na kujifanya muungwana. sasa maji yale pale hayatoshi hospitali, hayatoshi majengo wala kurungeni na msitu ndio huo tu unaotegemewa kutunza maji.sijui anawapigania watu gani.labda kila mtu awe na kisima chake sasa. nyundo uko wapi bw ulisema utagombea au umeogopa muhali? mzizi itabidi uni pm
Mkuu nipo, tunaendeleza harakati! Hayo ya mambo ya Mafia yanahitaji umakini mkubwa kuyazungumzia, inawezekana pia ikawa ni siasa, ila cna maana ya kwamba yapuuzwe! Kuhusu mimi kugombea hilo ni suala la muda, muda mwafaka ukifika nitatoa kauli, kuhusu 2010 mda wetu nadhani ulikuwa haujafika!
Mkuu nipo, tunaendeleza harakati! Hayo ya mambo ya Mafia yanahitaji umakini mkubwa kuyazungumzia, inawezekana pia ikawa ni siasa, ila cna maana ya kwamba yapuuzwe! Kuhusu mimi kugombea hilo ni suala la muda, muda mwafaka ukifika nitatoa kauli, kuhusu 2010 mda wetu nadhani ulikuwa haujafika!
Tumevumilia tumeshindwa, Mbunge wa kipindi flani alitangaza nia ya kujitenga wakamzima. Sasa nadhani tunahitaji kufikiria upya hilo. Kwani rasilimali tunazo, kama bahari nzuri kwa uvuvi, fukwe nzuri kwa utalii, tuna gesi kama songo songo, zao la nazi, korosho na mabonde mazuri ya kilimo pamoja na kina cha maji ya kutupatia bandari nzuri.
Kwani tumechoshwa na unyonyaji na dharau!
Kwa sasa hakuna kiongozi yeyote wa chama hapa mafia anayejishughulisha na mambo ya chama, kwani hata hao viongozi wa chama wamekosa hata hoja za kuwajibu wananchi kwa sasa, kwani ahadi zimejirudia mara nyingi bila utekelezaji, sasa imebaki stori tu. Hata huyo mbunge wa Mafia amekosa hata usema huko bungeni, nadhani nyinyi ni mashahidi, inawezekana hata kumfaham hamumfahamu. Viongozi wa serikali ya ccm wamedhurumu maeneo ya ardhi za walalahoi wa mafia na kuuzia wawekezaji uchwara, sas ni migogoro ya ardhi ndio urithi wao, kuna kijiji kimoja nilitembelea na kuambiwa wanakijiji wote wameshitakiwa kwa kosa la uvamizi wa eneo. Karibuni mtasikia yaliyotokea huko tarime yakitokea mafia. Kwa sasa ni wakati mzuri sana kwa chama kinachohitaji kuungwa mkono kufika mara moja, kwani wananchi kwa kweli wamekata tamaa
Wewe ni nani mpaka usemi wako ndio uwe usemi wa watu wote wa mafia? Matatizo uliyosema sio ya mafia tu ni sehemu nyingi tu za Tanzania, kumbuka kura yako ni moja tu, unless hayo uliyosema uwe kweli umetumwa na wana mafia.
Ndugu yangu pole. Mimi kama mwana jamiiforums nasikitika kwa majibu uliyopewa na wana ccm wenzako kwa kuwatukana ndugu zetu wa Mafia. ccm ndivyo walivyo wameshindwa kuwaendeleza sasa wanawatukana. Tena huyo aliyekujibu ana cheo kikubwa ccm.
POLENI SANA.