Mafao ya NSSF yachukua sura mpya Ilala

Kande

Senior Member
Mar 15, 2016
116
106
Wakuu Niko hapa ofisi za NSSF Ilala karibu na Mwalimu Complex nafuatilia mafao yangu baada ya kuachishwa kazi katika kampuni moja ya kichina mwaka mmoja uliopita.

Lakini hali iliyopo hapa, watu wamepandwa na hasira baada ya kuambiwa hawawezi kupata mafao yao kwasababu shirika liko kwenye uchunguzi wa kubaini kama kweli fomu zilizowasilishwa kuomba mafao ni za watu walioachishwa kazi.

Kaka mmoja analalamika kuwa alifungua madai Juni mwaka Jana akaambiwa akae miezi 6. Aliporudi akapigwa miezi 3 tena.

Leo karudi anaambiwa baada ya mwaka 1 mpaka wakamilishe uchunguzi.

Wafanyakazi wa NSSF waliopo hapa wana wakati mgumu kuwatuliza watu kwasababu majibu yanayotolewa hawakubali.

Changamoto nyingine, wakiomba waonyeshwe sehemu ya kutoa malalamiko kwa uongozi wa shirika wamegoma na wanasema lazima wakubaliane na utaratibu uliopo.
 
Hii no moja ya picha
 

Attachments

  • IMG_20171221_092006.jpg
    IMG_20171221_092006.jpg
    188.1 KB · Views: 70
Hao jamaa ni wasumbufu balaa. Sitasahau nilivyodai pesa mwaka mzima na nikaja pewa pesa nusu ya stahili yangu.
 
hii nchi acheni tu km alijakukuta uwezi amini kuna ntu wangu akupewa kiinua mgonga na huu mfuko Nssf kwa miaka 40 ya kazi ila Mungu aliyesirini anawaona.
 
Wakuu Niko hapa ofisi za NSSF Ilala karibu na Mwalimu Complex nafuatilia mafao yangu baada ya kuachishwa kazi katika kampuni moja ya kichina mwaka mmoja uliopita.

Lakini hali iliyopo hapa, watu wamepandwa na hasira baada ya kuambiwa hawawezi kupata mafao yao kwasababu shirika liko kwenye uchunguzi wa kubaini kama kweli fomu zilizowasilishwa kuomba mafao ni za watu walioachishwa kazi.

Kaka mmoja analalamika kuwa alifungua madai Juni mwaka Jana akaambiwa akae miezi 6. Aliporudi akapigwa miezi 3 tena.

Leo karudi anaambiwa baada ya mwaka 1 mpaka wakamilishe uchunguzi.

Wafanyakazi wa NSSF waliopo hapa wana wakati mgumu kuwatuliza watu kwasababu majibu yanayotolewa hawakubali.

Changamoto nyingine, wakiomba waonyeshwe sehemu ya kutoa malalamiko kwa uongozi wa shirika wamegoma na wanasema lazima wakubaliane na utaratibu uliopo.
Dawa yao kuwapelekea vikongwe wetu wawaleee M~Mae, Wawatibu na wawalishe,tunafanya Kazi kwa shida, tunalipishwa 30% PAYE, tunakatwa 10% NSSF, Tunakatwa HESLB, Tunatakiwa tulips kodi na kusomesha watoto.

Ipo Siku nitajitoa ufahamu
 
Kweli naona kauli ya vyuma vitavunjika kweli kweli inatekelezwa kwa kasi ya ajabu.

Huo ni unyanyasaji na uonevu kwa wafanyakazi walioteseka tena wana majonzi ya kufukuzwa kazi na bado kupata hata hizo hela kidogo walizojichangia wenyewe bado inakuwa nongwa.

Mambo mengine yanaiaibisha serikali.

Aiseeeeh.
 
Haya ndio madhara yake. Kila wapinzani wakikosoa utendaji mbovu na wa mabavu unaofanywa na serikali mnasema sio wazalendo. Wananchi watapigika sana kwa stahili hii, watu waache ushabiki wa kisiasa kwenye masuala nyeti ili serikali iwajibike.
 
mimi PSPF huku Mwanza walisha niambia mpaka nifikishe miaka 55 ndo ntapata, yn nlifatilia nikaambiwa nikae miezi 6 ndo watanipa nliporudi ndo nkakutana na majibu ya miaka 55 sio siri machozi yalinitoka, sasa ni mwaka 1 na miezi 3 toka bank moja maarufu hapa tz ikatishe mkataba wangu ila mpaka leo cjawai pata haki yangu na ndo nlikuwa napigia hesabu haka ka mafao kawe ka mtaji kangu mtaani. Ila kinacho nshangaza ni kuwa wenzangu tulioctishiwa mkataba kwa pamoja walio kuwa mfuko tofauti na PSPF kule LAPF hawakuchukua hata miezi 6 wakapata mafao yao, sasa ckuelewa cjui kwnn PSPF wamekatalia hela yangu mpaka sasa ilihali ndo nlikuwa ningalia kwa macho yote kama mtaji jmn.
 
katika uamuzi bora niliowahi kuufanya ni kuchukua changu mapema nssf... japo nusu ya mafao nilikula hasara... ila nusu mengine yananipa chakula mpaka leo... mradi mmoja ulibuma na mwingine ukatiki
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom