residentura
JF-Expert Member
- Mar 1, 2017
- 9,531
- 13,458
CCM hii hii ambayo kwa miaka 60 ya uhuru wa Tanganyika imeshindwa kuondoa maadui wakuu watatu wa Watanzania zaidi ya kuwaongeza maadui wengine ndio inayoweza kuwa imara kuwaletea maendeleo Watanzania kweli!?Hakuna asiyetaka mabadiliko ya uongozi kama yanaambatana na mabadiliko chanya. Ni msingi huo huo Rais amekuwa akiwatumbua viongozi wasiotimiza matarajio ya nafasi zao.
Hivyo basi kutahitajika chama chenye Sera mbadala na bora zaidi kwa maendeleo ya kijamii, kisiasa, kiuchumi na kiteknolojia. Hicho chama pia kinapaswa kuwa na viongozi wenye utashi wa kisiasa (wenye kuziishi sera za chama).
Hapa nchini kuna mfumo wa demokrasia ya vyama vingi vya siasa, bado wanasiasa na wananchi wanaishi, kwa maneno na matendo kama vile nchi iko kwenye mfumo wa chama kimoja.
Hilo linajitokeza dhahiri wakati wa chaguzi. Vyama vya siasa vingi huteua wagombea wenye sifa binafsi. Vichache, ambavyo hutumia mchakato wa kura za maoni pia huteua wagombea wanaokidhi sifa zilizowekwa na chama lakini si uwezo wao wa kuelewa na kuieleza Ilani ya Uchaguzi ya chama kwa wapiga kura.
Wagombea karibu wote, kwenye kampeni, badala ya kunadi sera zao wanashambuliana na kuonesha ubingwa wao jukwaani, wakijirundikia sifa wasizostahili na wakati mwingine kutoa ahadi hewa. Wananchi nao badala ya kusikiliza sera huvutiwa na malumbano na misifa ya wagombea jukwaani.
Pamoja na mapungufu hayo, kwa vyama vya siasa vinavyoshiriki chaguzi Mkuu, mwaka huu, ni CCM bado inazo sifa za kuongoza nchii, kimuundo, Kisera na aina ya viongozi wake.
Msikilize huyu bibi hapa chini.