Maendeleo ya watu au vitu?

Maendeleo ya watu au vitu?

Huwezi kuzungumzia vitu bila watu na watu bila vitu. Hii sawa na maji na samaki vinategemeana hakuna mstari tenganishi. Combination ya watu na vitu huleta maendeleo.Kifalsafa watu huleta vitu li kuboresha maisha yako.yaani kwa kimombo ni Human +materialist approach (ideas + materials)ndipo utapata maendeleo ya kweli. Tunahitaji meli ili tusafiri kwa ajili ya maendeleo. Nyumba nzuri ili tuishi vizuri na kuondoa umasikini wa vitu.Tunalipa kodi ili
tupate maendeleo ya watu na vitu pia vyote vinahitajika kwa wakati wote.
 
Maendeleo ya watu ndo kila kitu ,unajenga reli ambayo haina faida kwa nchi, unarudia uchaguzi asubui na jion Rais asiyekuwa na uwezo ndo anafanya hayo.
Marndeleo yako unayaleta mwenyewe. Serikali kazi yake ni kukujengea mazingira ya wewe kuweza kufanya maendeleo yako kwa urais
 
Maendeleo ya watu ndo kila kitu ,unajenga reli ambayo haina faida kwa nchi, unarudia uchaguzi asubui na jion Rais asiyekuwa na uwezo ndo anafanya hayo.
Msiongee kama msiokuwa na akili, hivi maendeleo ya watu ni yapi
 
Mimi kwa mtazamo wangu nafikiri makosa yapo katika kutafsiri au kuelewa "Maendeleo", " Vitu" na "Watu". Mambo haya matatu, kimsingi hayawezi kutenganishwa na mtu au watu.

Hapa kuna chanzo cha maendeleo na kilele au lengo la maendeleo. Chanzo cha maendeleo ni nini na kilele au lengo la maendeleo ni nini?

Maswali haya ni msingi na muhimu kujibu: maendeleo ya watu au vitu?
 
Kimsingi jamaa yupo vizuri kwa mtazamo wake na vipaumbele vya ilani ya chama chake, Ila kutokana na malighafi nyingi tulizonazo inatakiwa tupate kiongozi atakae fumua mfumo w elimu iliyopo kwa sasa ambayo si rafiki Sana kwa maendeleo ya mtu mmoja mmoja.
Tukifanikiwa kutoa elimu itakayomfanya Kila mhitimu aweze kujitegemea na kuwa na uwezo wa kugundua fursa katika eneo lake itakuwa poa Sana, apo serikali kazi yake itakuwa ni kuwaendeleza na kuwatafutia masoko kwakile kinacho zalishwa.
Kwa kumalizia ni vyema nchi yetu ikafanya mabadiliko kwenye uongozi hiki chama kimoja hakitatufikisha kule tunakotarajia kwenda,inatakiwa siku moja wakae pembeni wajifunze kwa wenzao ili wakirudi Tena watajifunza kufuata ushauri wa wananchi Kama mtoa mada hapo juu!!
 
Kimsingi jamaa yupo vizuri kwa mtazamo wake na vipaumbele vya ilani ya chama chake, Ila kutokana na malighafi nyingi tulizonazo inatakiwa tupate kiongozi atakae fumua mfumo w elimu iliyopo kwa sasa ambayo si rafiki Sana kwa maendeleo ya mtu mmoja mmoja.
Tukifanikiwa kutoa elimu itakayomfanya Kila mhitimu aweze kujitegemea na kuwa na uwezo wa kugundua fursa katika eneo lake itakuwa poa Sana, apo serikali kazi yake itakuwa ni kuwaendeleza na kuwatafutia masoko kwakile kinacho zalishwa.
Kwa kumalizia ni vyema nchi yetu ikafanya mabadiliko kwenye uongozi hiki chama kimoja hakitatufikisha kule tunakotarajia kwenda,inatakiwa siku moja wakae pembeni wajifunze kwa wenzao ili wakirudi Tena watajifunza kufuata ushauri wa wananchi Kama mtoa mada hapo juu!!
Hakuna asiyetaka mabadiliko ya uongozi kama yanaambatana na mabadiliko chanya. Ni msingi huo huo Rais amekuwa akiwatumbua viongozi wasiotimiza matarajio ya nafasi zao.

Hivyo basi kutahitajika chama chenye Sera mbadala na bora zaidi kwa maendeleo ya kijamii, kisiasa, kiuchumi na kiteknolojia. Hicho chama pia kinapaswa kuwa na viongozi wenye utashi wa kisiasa (wenye kuziishi sera za chama).

Hapa nchini kuna mfumo wa demokrasia ya vyama vingi vya siasa, bado wanasiasa na wananchi wanaishi, kwa maneno na matendo kama vile nchi iko kwenye mfumo wa chama kimoja.

Hilo linajitokeza dhahiri wakati wa chaguzi. Vyama vya siasa vingi huteua wagombea wenye sifa binafsi. Vichache, ambavyo hutumia mchakato wa kura za maoni pia huteua wagombea wanaokidhi sifa zilizowekwa na chama lakini si uwezo wao wa kuelewa na kuieleza Ilani ya Uchaguzi ya chama kwa wapiga kura.

Wagombea karibu wote, kwenye kampeni, badala ya kunadi sera zao wanashambuliana na kuonesha ubingwa wao jukwaani, wakijirundikia sifa wasizostahili na wakati mwingine kutoa ahadi hewa. Wananchi nao badala ya kusikiliza sera huvutiwa na malumbano na misifa ya wagombea jukwaani.

Pamoja na mapungufu hayo, kwa vyama vya siasa vinavyoshiriki chaguzi Mkuu, mwaka huu, ni CCM bado inazo sifa za kuongoza nchii, kimuundo, Kisera na aina ya viongozi wake.
 
Lisu hatajenga barabara, shule wala zahanati maana hayo ni maendeleo ya vitu
Atakachokifanya ni kuwafukuza wamachinga barabarani maana hayo ndiyo maendeleo ya watu
 
Maendeleo ya watu ndo kila kitu ,unajenga reli ambayo haina faida kwa nchi, unarudia uchaguzi asubui na jion Rais asiyekuwa na uwezo ndo anafanya hayo.
Una akili ndogo, na fikra ndogo Sana. Mungu kwenye uumbaji alianza mtu au vitu ndio akamleta mtu kuwa in charge?.
Kwanye kile chama cha Mbowe, hakuna kiongozi mule wote wapigaji tu. Ndio maana watanzania wote wamewashtukia nia yenu. Wanaomba usiku na mchana, nchi hii isije ingia mikononi mwa wabakaji wa demokrasia na kuiuza kwa mabeberu wenu. Mungu tuepushie mbali na hili balaa la saccos.
 
Lisu hatajenga barabara, shule wala zahanati maana hayo ni maendeleo ya vitu
Atakachokifanya ni kuwafukuza wamachinga barabarani maana hayo ndiyo maendeleo ya watu
Ukitaka kujua chama cha Mbowe, kitalifanyia nini taifa angalia Mbowe anavyokibagaza chama chake ndio utajua kwanini manyumbu wana akili isiyo na akili hata Moja.
 
Lisu hatajenga barabara, shule wala zahanati maana hayo ni maendeleo ya vitu
Atakachokifanya ni kuwafukuza wamachinga barabarani maana hayo ndiyo maendeleo ya watu
Mimi na WaTz wenye hoja ya kujua maendeleo ya watu yataletwaje bila maendeleo ya vitu, tunasubiri lala salama ya kampeni ya mgombea Urais kupitia CHADEMA, atufafanulie. Asipofanya hivyo, akate tamaa na ataisikia Ikulu mpya ya Dodoma kwenye TV tu.

Ukurasa wa 1 wa Ilani ya CHADEMA, imeandikwa Ukombozi huu wa awamu ya pili unasukumwa na falasafa na madhumuni yanayofanana kwa vile, yanalenga kumtoa Mtanzania katika hali duni kwenda kwenye hali bora zaidi ya maisha.. Hili ni dhumuni lenye afya kimaendeleo lakini linabaki kuwa nadharia tu kwa sababu ndani ya Ilani, hakuna mahali popote limechambuliwa kwa kina jinsi ya kufikia azima hiyo.
 
Kwani mkuu, mwendokasi ikikuwahisha kkoo ukafanya mishe zako ukapata mpunga wako sio kitu hicho?.
Mwendokasi inagusa watu, ni maendeleo ya vitu yanayogusa watu. Yaani yawe lengo ni kugusa watu kwa kuangalia economic of scale. Si sawa na kutumia zaidi ya tilioni moja kununua ndege ambazo uajiri watu 404 na wawezao kumudu kupanda ndege tz nzima ni watu milioni moja.
 
Yanategemeana bila kujenga barabara miji itapanuka polepole bila kuwa umeme wakutosha kukiwa na migao ya umeme unarudisha biashara zinazotumia umeme nyuma watu wanakosa mapato bila hospitali watu wanaishi kwa afya mbovu bila miradi ya maJi watu wanapoteza muda kupata maji na kufikiria anapata wap maji ya kutumia badala ya kuwaza mawazo ya kimaendeleo au kufanya na hii miradi inasaidia pia kukuza ajira sababu waendeshaji ni sisi sisi wa tz hii ni mada chonganishi kutoka kwa wapinzani ila ukikaa chini ukawaza inasaidia sana ni nyenzo za kimaendeleo
Africa is fighting independence for the second time everywhere. This indigenous colonialists like maccm represent the worst form of colonialism, because they can camouflage as if they have the best interest of people.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwendokasi inagusa watu, ni maendeleo ya vitu yanayogusa watu. Yaani yawe lengo ni kugusa watu kwa kuangalia economic of scale. Si sawa na kutumia zaidi ya tilioni moja kununua ndege ambazo uajiri watu 404 na wawezao kumudu kupanda ndege tz nzima ni watu milioni moja.
Hao watu million 1 siyo watanzania wanaohitaji huduma kutoka kwenye serikali yao?
 
Mwendokasi inagusa watu, ni maendeleo ya vitu yanayogusa watu. Yaani yawe lengo ni kugusa watu kwa kuangalia economic of scale. Si sawa na kutumia zaidi ya tilioni moja kununua ndege ambazo uajiri watu 404 na wawezao kumudu kupanda ndege tz nzima ni watu milioni moja.
Yawezekana hicho ndiyo kiwango chako cha elimu ya uchumi hadi unasema "economic of scale" ukimaanisha "economies of scale" yaani uchumi ambao mizania yake ni faida makampuni yanapata yakizalisha kwa ufanisi.

Miundo mbinu inayosababisha makampuni yazalishe kwa ufanisi ni ile inayowezesha kusafirisha malighafi kwa haraka, kuchakata hiyo malighafi kwa haraka, na kusafirisha bidhaa kwa haraka kwenda sokoni. Makampuni hayo ndiyo yenye uwezo wa kulipa kodi kubwa kwa Serikali na ikatumika kuboresha ustawi wa jamii (maendeleo ya watu). Mifano ni usafiri wa anga, treni ya mwendo kasi, barabara bora na imara, usafiri majini, nishati ya bei nafuu, nk
 
Yawezekana hicho ndiyo kiwango chako cha elimu ya uchumi hadi unasema "economic of scale" ukimaanisha "economies of scale" yaani uchumi ambao mizania yake ni faida makampuni yanapata yakizalisha kwa ufanisi.

Miundo mbinu inayosababisha makampuni yazalishe kwa ufanisi ni ile inayowezesha kusafirisha malighafi kwa haraka, kuchakata hiyo malighafi kwa haraka, na kusafirisha bidhaa kwa haraka kwenda sokoni. Makampuni hayo ndiyo yenye uwezo wa kulipa kodi kubwa kwa Serikali na ikatumika kuboresha ustawi wa jamii (maendeleo ya watu). Mifano ni usafiri wa anga, treni ya mwendo kasi, barabara bora na imara, usafiri majini, nishati ya bei nafuu, nk
Kodi na magawio huwa na maana zinapotumika kwenye tija za maendeleo,na sio tija za wanasiasa kutafutia kura na kula
 
Back
Top Bottom