Maendeleo ya watu au vitu?

Maendeleo ya watu au vitu?

Watu wanataka pesa mfukoni(maendeleo ya watu) ,hata ukijenga lami hadi mlangoni,flyover hadi kushukia sebuleni etc kama watu hawana fedha,mzunguko hovyo wa pesa kamwe watu hawawezi kukukubali.

Watu wakiwa na Mpunga usipowajengea barabara watajiorganise na kujenga hata ya moramu ,usipowaleta umeme kwakuwa wana fedha wataweka solor,usipowaleta maji kwakuwa wana fedha mifukoni watanunua bolzer au watachimba visima!!!
Hizo flyovers, lami, madaraja etc yanajengwa na robot?

Sio raia wa kawaida tena wengi tu? Nenda kaombe kazi upate kitu cha kukukwamua sababu Hakuna serikali inayowagawia wananchi wake pesa ya bure
 
Kila kijiji kiwe na tractor moja, kuwe na mazao ya kimkakati, halafu kila mkulima awezeshwe pembejeo na kulima minimum heka 3.
Hivyo ulivyovitaja mbona vyote ni vitu? Au ni mimi siwaelewi?
 
Mimi kama hakuna uwekezaji wa kweli kwenye kilimo, hayo maendeleo mengine naona ni ya vitu zaidi.

Kilimo Kwanza sijui ilifia wapi hawa CCM Mpya? Huko ndipo wapo 70% ya waTanzania vijijini.

Maono ya Mizengo Pinda waziri mkuu wa serikali ya CCM Orignal awamu ya 4 :

Kilimo Kwanza ni kauli mbiu ni inatokana na mkakati wa kusukuma na kuendeleza kilimo.

Kuvuta sekta binafsi iingie pia ktk sekta ya kilimo ili kuongeza uzalishaji wa mazao pamoja na wananchi wakulima wadogo wadogo.

Kilimo ni chanzo muhimu cha wananchi kuondokana na umasikini. Hivyo mapinduzi toka kilimo cha mkono kwenda kwa wanyama kazi, matrekta madogo na hatimaye matrekta makubwa.

 
CCM Orignal na mkakati wa Kilimo Kwanza

19 Jan 2018
Rais mstaafu Jakaya Kikwete atekeleza kwa vitendo sera ya kilimo kwanza katika eneo la Kiwangwa Bagamoyo Mkoa wa Pwani kwa kulima Nanasi na Papai
 
Hoja ya Maendeleo ya Vitu dhidi ya Maendeleo ya Watu : wananchi walilia Maendeleo ya Watu toka mwaka 2017 wamejiongeza kwa kufanya harambee 89 lakini serikali haioni juhudi zao za kutaka huduma ya afya kwa Maendeleo ya Watu .

4 Julai 2020
Mbeya, Tanzania

Kina Mama Inawalazimu Kusafiri Kilometa 70 kupata Huduma za Afya


VIFO vya MAMA na MTOTO Wananchi Wamlilia RAIS MAGUFULI, -"Tusaidie Tumechanga Mill 102"



WANANCHI wa Kijiji cha Ifupa Wilaya ya Mbeya wamemwomba Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Albert Chalamila kufikisha maombi yao kwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Magufuli ili kuwasaidia ujenzi wa kituo cha Afya.

Source : Global TV Online
 
2 Nov 2019
Same, Kilimanjaro
Tanzania

Uwajibikaji na Ahadi kwa Wananchi
Tizama kipindi cha Ajenda 2020 Alloyce Nyanda akiwa na Mkurungezi wa halmashauri ya wilaya ya Same Ndugu. Anna-Claire Shija.. akijibu changamoto kibao za wananchi wa wilaya ya Same na juhudi za kutafuta ufumbuzi hakuna madawati hata shule iliyopewa jina Shule ya msingi Mkapa, maji , barabara...afya ya jamii...



Source : Alloyce Nyanda
 
Watu wanataka pesa mfukoni(maendeleo ya watu) ,hata ukijenga lami hadi mlangoni,flyover hadi kushukia sebuleni etc kama watu hawana fedha,mzunguko hovyo wa pesa kamwe watu hawawezi kukukubali.

Watu wakiwa na Mpunga usipowajengea barabara watajiorganise na kujenga hata ya moramu ,usipowaleta umeme kwakuwa wana fedha wataweka solor,usipowaleta maji kwakuwa wana fedha mifukoni watanunua bolzer au watachimba visima!!!
Miundombinu ndiyokichocheo kikubwa cha ukuaji wa uchumi kuanzia kwa watu wenyewe, hakutakuwa na pesa mifukoni kama miundombinu mibovu itashamili.
 
Hizo flyovers, lami, madaraja etc yanajengwa na robot?

Sio raia wa kawaida tena wengi tu? Nenda kaombe kazi upate kitu cha kukukwamua sababu Hakuna serikali inayowagawia wananchi wake pesa ya bure
Kwani Awamu ya kikwete ilikuwa inagawa fedha kwa wananchi wake? Utawala wa kikwete kulikuwa na maisha bora kwa kila mtz!! Utawala wa JK kulikuwa na mzunguko mkubwa sana wa fedha,sie madalali tulikuwa tunapata fedha daily kwa kupangisha nyumba ,kuuza magari ,kuuza viwanja etc

Ila alivyoingia huyo jamaa wenu aka disturb equilibrium ya uchumi kwa kujifanya mjuaji hivyo akaondoa mzunguko wa fedha na wananchi wakaanza kukosa pesa,biashara kufungwa etc!!
 
Miundombinu ndiyokichocheo kikubwa cha ukuaji wa uchumi kuanzia kwa watu wenyewe, hakutakuwa na pesa mifukoni kama miundombinu mibovu itashamili.
Mnasema jamaa ndio kafanya miundombinu ya kutisha kuliko JK na kama miundombinu ndio kichocheo cha uchumi mbona wakati wa JK GNI ilikuwa USD 200+ ndani ya miaka mi5 lakini utawala wa JIWE GNI ni 54 tu kwa miaka mi5 hiyo inamaanisha utawala wa JIWE ukuaji wa uchumi ni NEIIIII.
 
Maendeleo ya watu ndo kila kitu ,unajenga reli ambayo haina faida kwa nchi, unarudia uchaguzi asubui na jion Rais asiyekuwa na uwezo ndo anafanya hayo.
Maendeleo ya watu ndio yakoje hayo?
 
Maendeleo ya watu ndio yakoje hayo?

Ndiyo tatizo la CCM Mpya, Maendeleo ya Watu ni katika kipato halisi, huduma bora za kijamii kama elimu na afya bora halafu wananchi hao wenye afya njema kufuatia shibe ya chakula bora na elimu watafanya Maendeleo ya Vitu.

Mnachofanya CCM Mpya ni kama kumuwekea punda mkokoteni mbele yake ausukume huku hukufanya mazingira bora ya Maendeleo ya mnyama-kazi ( Maendeleo ya Watu) achape kazi na bata.
 
Kwani Awamu ya kikwete ilikuwa inagawa fedha kwa wananchi wake? Utawala wa kikwete kulikuwa na maisha bora kwa kila mtz!! Utawala wa JK kulikuwa na mzunguko mkubwa sana wa fedha,sie madalali tulikuwa tunapata fedha daily kwa kupangisha nyumba ,kuuza magari ,kuuza viwanja etc

Ila alivyoingia huyo jamaa wenu aka disturb equilibrium ya uchumi kwa kujifanya mjuaji hivyo akaondoa mzunguko wa fedha na wananchi wakaanza kukosa pesa,biashara kufungwa etc!!
Fedha za kifisadi na haramu

Zilikuwa zinatokana na kuiba dawa za serikali
Ujangili
Dawa za kulevya
Wizi pesa za halmashauri
Ufisadi bandarini
Ufisadi miradi ya serikali
Rushwa
Utapeli na mambo mengine kama Hayo
 
Fedha za kifisadi na haramu

Zilikuwa zinatokana na kuiba dawa za serikali
Ujangili
Dawa za kulevya
Wizi pesa za halmashauri
Ufisadi bandarini
Ufisadi miradi ya serikali
Rushwa
Utapeli na mambo mengine kama Hayo
Sasa kwa taarifa yako katika awamu hii ndio imevunja rekodi ya ufisadi,wizi,rushwa ,wateule wa jiwe ndio wapiga deal,Bashite utawala wa kikwete alikuwa anaganga njaa tu lakini alivyoingia JIWE Bashite ni Bilionea , Sitaki kumtaja DED mmoja ni tajiri balaa ,anajenga Ghorofa sehemu tatu tofauti kwa wakati mmoja anaanza mwanzo mpaka mwisho non stop na material ananua mapya hakuna kukodi marine wala 2x4 wala mirunda kwa sites zote!!

Unajua utajiri wa Mnyeti umeongezeka sana baada ya kuingia JIWE? Unajua utajiri wa Ally Hapi?

Bunge lilibariki ujenzi wa Chattle EYAPOtI? Bunge lilibariki ununuzi wa midege ? Unajua kwa nini mtu mmoja ndiye aliyeamua hayo? Ni 10% ambao ni UFISADI na WIZI.

Kangi na Andegengenye kwanini walitumbuliwa? WAPIGA DEAL.....Na kwanini walitumbuliwa? Hawajamshilikisha KIRANJA Mkuu kwenye deal lao.
 
Asante, mpuuzi mmoja wewe. Bila maendeleo ya vitu hakuna maendeleo ya watu! Mfano siku izi unaenda mbwinde kwenu na kurudi mjini kuendekea na shughuri nyingine mjini kwa wakati sababu ya njia zimeboreshwa. Unataka upate pesa ukae nazo matakoni ili watu wakunyenyekee kuomba usafiri? Selfish!
Zero brain
 
Ndiyo tatizo la CCM Mpya, Maendeleo ya Watu ni katika kipato halisi, huduma bora za kijamii kama elimu na afya bora halafu wananchi hao wenye afya njema kufuatia shibe ya chakula bora na elimu watafanya Maendeleo ya Vitu.

Mnachofanya CCM Mpya ni kama kumuwekea punda mkokoteni mbele yake ausukume huku hukufanya mazingira bora ya Maendeleo ya mnyama-kazi ( Maendeleo ya Watu) achape kazi na bata.
Kwa maana hiyo watu wakiendelea watajenga madaraja wenyewe, watanunua matreni wenyewe n.k.... Au unamaanishaje?
 
Asante, mpuuzi mmoja wewe. Bila maendeleo ya vitu hakuna maendeleo ya watu! Mfano siku izi unaenda mbwinde kwenu na kurudi mjini kuendekea na shughuri nyingine mjini kwa wakati sababu ya njia zimeboreshwa. Unataka upate pesa ukae nazo matakoni ili watu wakunyenyekee kuomba usafiri? Selfish!
L7 at work
 
Kwa maana hiyo watu wakiendelea watajenga madaraja wenyewe, watanunua matreni wenyewe n.k.... Au unamaanishaje?

Hili ni Tatizo lingine la CCM Mpya hawafahamu kuwa , watu ndiyo rasilimali kubwa ktk wingi wao wakiwa na elimu ya kujitegemea iliyo bora na afya nzuri ya mwili na akili kipi kitawashinda?

Watu binafsi au makundi wanaweza kuanzisha shirika la ndege, reli , meli kwa kutaja kwa uchache rasilimali watu iliyopata fikra huru ikisapotiwa na elimu bora na afya njema kwanini CCM Mpya hamtaki kuwaamini na kuwashirikisha watu-huru.

Kila mtu huzaliwa mtu-huru ila mfumo ndiyo huwabadilisha, mfano kwa Tanzania mfumo huu mbovu wa CCM Mpya kuwavua fikra-huru wananchi hivyo kuharibu uchumi wa nchi na kuwatia umasikini watu wengi.
 
Back
Top Bottom