Maendeleo ya watu au vitu?

Maendeleo ya watu au vitu?

L7 at work
ndio mimi ni lasaba, Sasa wewe uliesoma mbona unalialia humu, Au ulisomea kupewa pesa? Pambana ujenge nchi sio kulialia. Au wewe ni wale waliosoma ili wapate ajira? Ok karibu kitaa Kuna ajira kibao 😄. Kuna kazi zakupara samaki, hata kuparamiwa ikikupendeza.😎
 
Tatizo lingine la CCM Mpya, watu ndiyo rasilimali kubwa ktk wingi wao wakiwa na elimu ya kujitegemea iliyo bora na afya nzuri ya mwili na akili kipi kitawashinda?

Watu binafsi au makundi wanaweza kuanzisha shirika la ndege, reli , meli kwa kutaja kwa uchache rasilimali watu iliyopata fikra huru ikisapotiwa na elimu bora na afya njema kwanini CCM Mpya hamtaki kuwaamini na kuwarishikisha watu-huru.

Kila mtu huzaliwa mtu-huru ila mfumo ndiyo huwabadilisha mfano mfumo wa CCM Mpya kuwavua fikra huru
Mkuu naamini haupo serious.
 
Maendeleo ya watu ndo kila kitu ,unajenga reli ambayo haina faida kwa nchi, unarudia uchaguzi asubui na jion Rais asiyekuwa na uwezo ndo anafanya hayo.
Wananchi wanapata majanga ya mafuriko njaa anasema hajaleta yeye majanga. Lakini uchaguzi unarudiwa jimbo hilo hilo anatoa bilioni 5 za uchaguzi tena harala sana.

Sijawahi kuona Rais mbinafsi kama Jpm
 
Wananchi wanapata majanga ya mafuriko njaa anasema hajaleta yeye majanga. Lakini uchaguzi unarudiwa jimbo hilo hilo anatoa bilioni 5 za uchaguzi tena harala sana.

Sijawahi kuona Rais mbinafsi kama Jpm
Truly
 
Tahadhari tusiingize sana siasa tujaribu kujenga hoja.

Sio siasa mkuu.
Ni utabiri wa Franz Fannon(The Wretched of the Earth) unatimia.
Ila nalikubali angalizo lako.
 
Kumekuwepo na mjadala mpana sana kuhusu mantiki mbili za maendeleo kwenye mitandao ya kijamii, nami ningependa kutoa maoni yangu kuhusu jambo hili, Kuhusu maendeleo ya watu na maendeleo ya vitu. Jambo la kwanza ambalo tunapaswa kutambua ya kwamba maendeleo ya vitu ni kwaajili ya watu. Watu ndio wanaotumia vitu na ndio walio vitengeneza kwaajili yao. Kwahiyo maendeleo ya vitu ni muhimu sana. Na ndio hasa yanayofanya watu wafanye kazi kwa bidii ili wabadilishe mazingira yao na kuitawala dunia. Maisha yamekuwa rahisi zaidi kuliko karne kadhaa zilizopita kwasababu ya maendeleo ya vitu yaliyoletwa na vumbuzi kadhaa.

Kwahiyo hatuwezi kuyakataa moja kwa moja. Jambo la msingi la kujadili hapa pengine ni jinsi gani tutawekeza kwa watu ili hayo maendeleo wajiletee wao wenyewe badala ya kutegemea watu wengine. Hapa tunazungumzia intellectual + moral development kwa watu wetu. Kama nchi kwa kiwango kikubwa bado ni tegemezi.

Bidhaa nyingi ambazo tunazo katika nchi yetu hatujazalisha sisi wenyewe na hatuna technologia ya kufanya hivyo. Bado ni tegemezi kwa kiwango cha juu kwenye masuala ya technologia kwahiyo tunahitaji kuwekeza kwa watu ili wawe na skills za kutosha ili walete hayo maendeleo ya vitu kutokana na intellectual capability zao. Nadhani huu ndio msingi wa kujitegemea kama nchi na ndio msingi wa kuwekeza kwa watu na maendeleo ya watu. Na Elimu yetu inapaswa kujengwa katika mtizamo huo.

Watu hawajaendelea kama hawawezi kujenga madaraja kwa kutumia watu wao wenyewe, kujenga reli kwa kutumia watu wenyewe, ndege kwa kutumia watu wao wenyewe, barabara, bunduki na vifaa vya kijeshi kwa kutumia watu wao wenyewe na mambo mengine mengi wanayotumia kwa maisha yao wenyewe ya kila siku. Tunapima uwezo wa nchi na maendeleo yake kwa uwezo wa raia wake kutengeneza vitu wanavyotumia kila siku na sio kutumia wasichozalisha.

Kuna kauli inazungumzwa na watu nchi yetu ni tajiri ina mali ghafi wanasahau kwamba ili malighafi iwe mali ugunduzi wa vitu unatakiwa ufanyike. Petroli bila ugunduzi wa magari isingekuwa na thamani. Gunduzi ndio zinazofanya malighafi kuwa mali. kwa mantiki hiyo tusidhani kwamba malighafi zetu zitatufaidisha zaidi ya wale waliofanya malighafi kuwa mali, waliofanya malighafi kuwa mali ndio wenye nguvu zaidi. Katika uhalisia wake malighafi haiwezi kuwa mali pasipo gunduzi. Tusipokuwa na aina hii ya fikra tusitegemee kuendelea kama taifa. Maendeleo ya kweli ni uwezo wa watu kujiletea maendeleo yao wenyewe kwa kutumia watu wao wenyewe .

Above all else tunahitaji watu wenye skills na maarifa ya kutosha miongoni mwa watu wetu kuliko kitu kingine ili maendeleo yetu tujiletee wenyewe bila kusubiri watu wengine waje watuletee. So tunahitaji watu wenye nidhamu, skills , uzalendo na maarifa ya kutosha kama tunataka kuendelea na kuwa na dira kama taifa.
Well stated mkuu
 
Jamani eleweni hakuna maendeleo bila vitu pitieni kipindi cha industrial revolution ulaya na mataifa mengine. China,Malysia,vietnam,South Korea zimeendelea kwa ajili ya miundo mbinu nk ingawa pia elimu, afya, maji navyo vilipewa umuhimu. Watu na vitu huwezi kuvitenganisha. Awamu hii ya tano vyote vimeshughulikiwa ipasavyo, na tusichukulie pesa mfukoni zilizozagaa wakati wa awamu ya nne kutokana na rushwa kubwa,ufisadi,etc ndiyo pesa mnayotaka irudi. Haitawezekana. Mzunguko wa pesa una kanuni zake ili kuzuia inflation etc
 
Unajua sio kila jema analolifanya usiempenda ulitangaze kwa ubaya
Hii ni kutokuwa na uzalendo
Ndugu zangu maendeleo ya vitu nchini kwetu ni mwanzo mzuri wa kufikia hatua kubwa ya maendeleo ya watu
Tuseme ukweli miundombinu ya vitu ikaachwa honyo tutakawa fedha kwa kila mtu tutafikiaje maendeleo kama nyie si waongo
Muacheni mh rais asimamie miradi ya maendeleo.
 
Hakuna maendeleo ya watu bila vitu. Dunia ilianza na vitu na hata Mungu alianza kuumba dunia na kisha mtu. Meli itasaidia watu kusafiri na kupunguza adha ya kusafiri kwa mateso hata kama wana pesa kama hamna vitu utazifanyia nini ingawaje ili uwe na vitu unahitaji watu na pesa kama mtaji tu kuzalisha ikiwemo ardhi.

Hospitali na madawa zikitumiwa na madaktari zitatibu watu na kuwapa afya na kisha kuzalisha kuitafuta hiyo pesa. Fedha tunazozitaka kwa wingi za kuzagaa hazipo tena kutokana na mianya ya rushwa madawa ya kulevya etc kuzibwa. We playing with formal source of income na controlled economy inayohitaji uchape kazi.

Inabidi tuseme ni vitu gani ambavyo hatuvitaki na havina multplier effect! Hii ni issue tu ya kanuni za uchumi haya mambo yanategemeana mwisho wa siku. Mjadala huu ni mpana.
bravo.
 
Labda WanaJF mtasaidia kujibu swali langu hili, Je, wapiga kura, wengi wao (70%) wanaishi vijijini, watapenda kusikia nini kutoka kwa Wagombea, ili waridhie kuwapa kura yao?
Vijijini Sasa hivi hawahitaji kuambiwa ili wampigie kura mtu wanahitaji kuonyeshwa siasa za kuwaambia watu kitu ili wakupigie kura zimepitwa na wakati

CCM tukienda hatuwaambii tunawaonyesha kuwa barabara hiyo imnaiona? Hospital hiyo nzuri mnaiona tumejenga.Umeme huo mnauona hapa kijijini ? Shule hizi nzuri watoto wenu wanasoma bure mnaziona? Na watoto wanaenda kusoma bure mnaona? Miradi hii ya maji ya hapa kijijini mnaiona? Nk ndio tunatamka tunwomba kura zenu tufanye makubwa zaidi

Ambaye hajafanya kitu ndie ahangaike kutunga vitu hewa ambavyo Watu wa vijijini wala hawana muda navyo[/QUOTE]
 
kila mtu yupo sahihi.. ila tunatofautiana usahihi kulingana na muda na hali halisi ya kimazingira.. kuna wakati maendeleo ya vitu ni sahihi zaidi kuliko maendeleo ya watu and vice versa is true too.
kwa uchumi tulionao sasa tukiwekeza kwa watu pekee tutajikuta tuna jopo la wataalamu ambao watabaki kuhangaika na elimu zao bila kuepo na nyenzo au mazingira rafiki ya wao kutumia huo uwezo wao binafsi hivo kupelekea lengo la maendeleo kutofikiwa ipasavyo ndani ya kuda stahiki,. ila pia tukiwekeza kwenye vitu kama ilivyo sasa inarahisisha na kujenga mazingira rafiki kwa watu kufika mbali kiuchumi maana shughuli zao hazitakua zikikwama kwa kisingizio cha miundombinu.

mimi naona maendeleo ya vitu ni urahisishaji wa maendeleo ya watu hvyo hzi concept 2 zinatakiwa ziende sambamba kisianze kimoja kifate kingine. maendeleo ya watu kwa ajili ya nchi yanahitaji kujituma ari na uzalendo, vinginevyo tutaishia kupiga kelele maendeleo yetu huku tumekaa kwenye vijiwe vya kahawa kusubiria kila kitu.
 
Hili ni Tatizo lingine la CCM Mpya hawafahamu kuwa , watu ndiyo rasilimali kubwa ktk wingi wao wakiwa na elimu ya kujitegemea iliyo bora na afya nzuri ya mwili na akili kipi kitawashinda?

Watu binafsi au makundi wanaweza kuanzisha shirika la ndege, reli , meli kwa kutaja kwa uchache rasilimali watu iliyopata fikra huru ikisapotiwa na elimu babadilisha, mfano kwa Tanuharibu uchumi wa nchi na kuwatia umasikini watu wengi.
Hakuna ccm mpya ndugu ila ccm yasasa imerudi ya azimio la Arusha, CCM yakati hapo ilikuwa ccm ya wapenda ufisadi, wala rushwa nk kiukweli ccm ndan ya miaka 30 nyuma ilikosa uongozi imara na iliyumba na kuchukiwa sana na wanaochi mmoja wapo mi mwenyewe.

Kuhusu maendeleo ya vitu:- Miundombinu ndiyo kichocheo kikubwa cha uchumu Duniani, na kipindi cha JK wachumi wote wanakubaliana kuwa hakukuwa na udhibiti wa fedha, fedha nying zillikuwa haramu kias zilikuwa haziingii kwenye mzunguko wa uchumi zaid zikizagaa tu.
 
Vijijini Sasa hivi hawahitaji kuambiwa ili wampigie kura mtu wanahitaji kuonyeshwa siasa za kuwaambia watu kitu ili wakupigie kura zimepitwa na wakati

CCM tukienda hatuwaambii tunawaonyesha kuwa barabara hiyo imnaiona? Hospital hiyo nzuri mnaiona tumejenga.Umeme huo mnauona hapa kijijini ? Shule hizi nzuri watoto wenu wanasoma bure mnaziona? Na watoto wanaenda kusoma bure mnaona? Miradi hii ya maji ya hapa kijijini mnaiona? Nk ndio tunatamka tunwomba kura zenu tufanye makubwa zaidi

Ambaye hajafanya kitu ndie ahangaike kutunga vitu hewa ambavyo Watu wa vijijini wala hawana muda navyo
[/QUOTE]
Kama amhitaji kuwaambia Bali kuwaonyesha nguvu mnazotumia kuwadhibiti wapinzani ni za Nini??

Wekeni uwanjani uliosawa katika siasa tuone haya mnayoyasema Kama Yana ukweli.
 
Yanategemeana bila kujenga barabara miji itapanuka polepole bila kuwa umeme wakutosha kukiwa na migao ya umeme unarudisha biashara zinazotumia umeme nyuma watu wanakosa mapato bila hospitali watu wanaishi kwa afya mbovu bila miradi ya maJi watu wanapoteza muda kupata maji na kufikiria anapata wap maji ya kutumia badala ya kuwaza mawazo ya kimaendeleo au kufanya na hii miradi inasaidia pia kukuza ajira sababu waendeshaji ni sisi sisi wa tz hii ni mada chonganishi kutoka kwa wapinzani ila ukikaa chini ukawaza inasaidia sana ni nyenzo za kimaendeleo
Maendeleo watu hujiletea wenyewe kupitia miuondo mbinu wezeshi na rafiki na wakishaendelea uchangia maendeleo ya Taifa Kama kulipa Kodi vizuri na stahiki zitakazotumika kujenge miradi mikubwa Kama inayoendelea lakini tukianza mwisho ndiyo turudi nyuma yaani kwa wananchi Basi tutakuwa tumeendeleza vitu badala ya watu! Maana huyo mtu atakalia kulipia mikopo ya miradi iliyojengewa!!
 
Nakupa formula waliyo tumia mataifa

Kodi = maendeleo.

Vitu (havilipi kodi)
Watu (wanalipa)

Wanalipa watu gani? Wazalishaji

Mzalishaji ni yupi? Mwenye ujuzi wa kuzalisha yaani mwenye elimu.

Je tunaweza kutoa elimu kwa kila mtu? Ndio, si lazima iwe formal, hata non-formal. Yaani ya vyuo vya kati.

Vyuo vya ufundi vitazalisha wajuzi wengi; kodi nyingi, serikali itajenga vitu kwa namna itakayo. Rejea Uchina
 
Maendeleo ya vitu ni muhimu ili watu watumie hivyo vitu kupata maendeleo ya watu
 
Kumekuwepo na mjadala mpana sana kuhusu mantiki mbili za maendeleo kwenye mitandao ya kijamii, nami ningependa kutoa maoni yangu kuhusu jambo hili, Kuhusu maendeleo ya watu na maendeleo ya vitu. Jambo la kwanza ambalo tunapaswa kutambua ya kwamba maendeleo ya vitu ni kwaajili ya watu. Watu ndio wanaotumia vitu na ndio walio vitengeneza kwaajili yao. Kwahiyo maendeleo ya vitu ni muhimu sana. Na ndio hasa yanayofanya watu wafanye kazi kwa bidii ili wabadilishe mazingira yao na kuitawala dunia. Maisha yamekuwa rahisi zaidi kuliko karne kadhaa zilizopita kwasababu ya maendeleo ya vitu yaliyoletwa na vumbuzi kadhaa.

Kwahiyo hatuwezi kuyakataa moja kwa moja. Jambo la msingi la kujadili hapa pengine ni jinsi gani tutawekeza kwa watu ili hayo maendeleo wajiletee wao wenyewe badala ya kutegemea watu wengine. Hapa tunazungumzia intellectual + moral development kwa watu wetu. Kama nchi kwa kiwango kikubwa bado ni tegemezi.

Bidhaa nyingi ambazo tunazo katika nchi yetu hatujazalisha sisi wenyewe na hatuna technologia ya kufanya hivyo. Bado ni tegemezi kwa kiwango cha juu kwenye masuala ya technologia kwahiyo tunahitaji kuwekeza kwa watu ili wawe na skills za kutosha ili walete hayo maendeleo ya vitu kutokana na intellectual capability zao. Nadhani huu ndio msingi wa kujitegemea kama nchi na ndio msingi wa kuwekeza kwa watu na maendeleo ya watu. Na Elimu yetu inapaswa kujengwa katika mtizamo huo.

Watu hawajaendelea kama hawawezi kujenga madaraja kwa kutumia watu wao wenyewe, kujenga reli kwa kutumia watu wenyewe, ndege kwa kutumia watu wao wenyewe, barabara, bunduki na vifaa vya kijeshi kwa kutumia watu wao wenyewe na mambo mengine mengi wanayotumia kwa maisha yao wenyewe ya kila siku. Tunapima uwezo wa nchi na maendeleo yake kwa uwezo wa raia wake kutengeneza vitu wanavyotumia kila siku na sio kutumia wasichozalisha.

Kuna kauli inazungumzwa na watu nchi yetu ni tajiri ina mali ghafi wanasahau kwamba ili malighafi iwe mali ugunduzi wa vitu unatakiwa ufanyike. Petroli bila ugunduzi wa magari isingekuwa na thamani. Gunduzi ndio zinazofanya malighafi kuwa mali. kwa mantiki hiyo tusidhani kwamba malighafi zetu zitatufaidisha zaidi ya wale waliofanya malighafi kuwa mali, waliofanya malighafi kuwa mali ndio wenye nguvu zaidi. Katika uhalisia wake malighafi haiwezi kuwa mali pasipo gunduzi. Tusipokuwa na aina hii ya fikra tusitegemee kuendelea kama taifa. Maendeleo ya kweli ni uwezo wa watu kujiletea maendeleo yao wenyewe kwa kutumia watu wao wenyewe .

Above all else tunahitaji watu wenye skills na maarifa ya kutosha miongoni mwa watu wetu kuliko kitu kingine ili maendeleo yetu tujiletee wenyewe bila kusubiri watu wengine waje watuletee. So tunahitaji watu wenye nidhamu, skills , uzalendo na maarifa ya kutosha kama tunataka kuendelea na kuwa na dira kama taifa.
Hizi ni fikra chanya kabsa. Pongezi kwako mheshimiwa
 
Ni hoja ambayo imegeuzwa na Wanasiasa kama mtaji wa kisiasa na huenda ikatumika kama agenda kuu katika kampeni za Uchaguzi Mkuu mwaka huu. Kuna dalili ya kuelekea huko kutokana na jinsi Wanasiasa wanavyotafsiri taarifa ya Benki ya Dunia kuitambua Tanzania kama moja ya nchi yenye Kipato cha Kati.

Labda WanaJF mtasaidia kujibu swali langu hili, Je, wapiga kura, wengi wao (70%) wanaishi vijijini, watapenda kusikia nini kutoka kwa Wagombea, ili waridhie kuwapa kura yao?
1. Nadhani tunahitaji barabara nzuri zaidi kuliko ndege. Barabara zetu za vumbi hasa zile zinazounganisha wilaya ni mbaya sana. Na ubaya wa barabara hizi zinaleta matatizo mtambuka. Tulidhani baada ya mh. Kikwete kuunganisha mikoa kwa lami, tulifikiri dhana hiyo ingehamia kuunganisha wilaya kwa lami
2. Wananchi na serikali wamejenga zahanati, vituo vya afya na sekondari za kutosha. Tulidhani kuajiri watumishi wa taasisi hizi ni bora kuliko SGR
3. Huko nyuma wanafunzi wote wa elimu ya juu walipata mkopo kwa sasa ni tofauti. Tulidhani mikopo kwa wanafunzi hawa ni muhimu kuliko fly over.
Nk. Nk.
Na hapa lawama ni kwa wabunge wetu ambao hupitisha bajeti ambazo haziakisi mahitaji ya wapiga kura wao.
 
1. Nadhani tunahitaji barabara nzuri zaidi kuliko ndege. Barabara zetu za vumbi hasa zile zinazounganisha wilaya ni mbaya sana. Na ubaya wa barabara hizi zinaleta matatizo mtambuka. Tulidhani baada ya mh. Kikwete kuunganisha mikoa kwa lami, tulifikiri dhana hiyo ingehamia kuunganisha wilaya kwa lami
2. Wananchi na serikali wamejenga zahanati, vituo vya afya na sekondari za kutosha. Tulidhani kuajiri watumishi wa taasisi hizi ni bora kuliko SGR
3. Huko nyuma wanafunzi wote wa elimu ya juu walipata mkopo kwa sasa ni tofauti. Tulidhani mikopo kwa wanafunzi hawa ni muhimu kuliko fly over.
Nk. Nk.
Na hapa lawama ni kwa wabunge wetu ambao hupitisha bajeti ambazo haziakisi mahitaji ya wapiga kura wao.
ITAPENDEZA pia ukashuri aina ya chanzo cha mapato endelevu kugharamia mahitaji hayo uliyoyataja
 
Back
Top Bottom