Maendeleo ya China yaliletwa na Katiba Mpya?

Maendeleo ya China yaliletwa na Katiba Mpya?

Ndugu August, kama hukukusudia kupotosha kwa bandiko lako hili basi uelewa wako kwenye haya mambo bado ni mdogo.

Naona umetaja tu bila urari wala mantiki USSR ya Gorbachev na Ujerumani ya Hitler kama mifano yako 'bila katiba mpya", tena kwako hata dikteta fisadi Putin pia ni role model wa maendeleo.

Nigependa tuwe na mjadala mpana na sio propaganda, lakini kabla sijaenda mbele, je unajua Maendeleo ya Korea Kusini, Malaysia, Singapore, Ghana na Kenya yalipatikanaje?

Nchi kama Ujerumani na USSR (ulizotaja) na China uliyoitaja kwenye heading ni nchi/tawala/dola za zamani ni sawa sawa na tungesema Ufaransa, Japan na Canada au hata India, hao sio saizi yetu pia sio "rika" letu. Lakini hizo nchi nilizotaja hapo juu ni "rika" moja na sisi hivyo kama ni kujipima hao watatupa matokea halisi na yenye kushabihiana na sisi kama Taifa.
 
Hatuji ila tutasema. Maendeleo ya China yameletwa na uongozi bora. Maendeleo ya Rwanda yameletwa na uongozi bora. Mwalimu alisema: "Ili tuendelee tunahitaji watu siasa safi na uongozi bora." Hakusema na katiba mpya. Maendeleo ya Tanzania yataletwa na uongozi bora. Watu wakiuunga mkono uongozi wa Awamu ya 5, kama walivyounga mkono uongozi wa awamu zote tutapata maendeleo. Tunaona itihada za Raisi wa awamu ya 5 katika kuleta uongozi bora nchini.Bial shaka hatua za kuelekea kupata maendeleo zimekwisha anza kuonekana.
Yaonekana tatizo lako ni uelewa. Katiba imara ndiyo inayowezesha kuwa na siasa safi na hata uongozi bora. Kwenye katiba mbovu kama iliyopo kwetu, panakuwa na siasa za hila na ukandamizaji.
Baada ya Mao kufariki na baadae mkewe kuondolewa madarakani, katiba na sheria iliyokuwapo ilifanyiwa marekebisho makubwa na kuruhusu kwa mara ya kwanza uwekezaji wa ndani na kutoka ndani na nje.
 
Yaonekana tatizo lako ni uelewa. Katiba imara ndiyo inayowezesha kuwa na siasa safi na hata uongozi bora. Kwenye katiba mbovu kama iliyopo kwetu, panakuwa na siasa za hila na ukandamizaji.
Baada ya Mao kufariki na baadae mkewe kuondolewa madarakani, katiba na sheria iliyokuwapo ilifanyiwa marekebisho makubwa na kuruhusu kwa mara ya kwanza uwekezaji wa ndani na kutoka ndani na nje.
Wanafalsafa wana kile wanachokiita "viti vinne vya kweli". Yaani ukweli kutazamwa kutoka pande tofauti za viti vinne. Ni kweli katiba bora yaweza kuleta uongozi ama utawala bora. Lakini lazima serikali ama kiongozi aliye/iliyo madarakani iwe na dhamira bora ya kuongoza ama kutawala katika ubora. Hiyo ndiyo imekuwa hoja gangu.
 
Sijui Masoud Kipanya anamaanisha nini kwenye cartoon yake iliyosema tukiacha mzaha tutakuwa nchi ya viwanda
 
Maendeleo ya Tanzania yataletwa kwa kufungia vyombo vya habari, kuteka na kuua?
 
Demokrasia na mbwembwe za katiba ni vitu ambavyo hutumika katika kuendeleza umasikini wa bara la Afrika.

Rwanda hawana katiba nzuri lakini tazama mambo aliyoyafanya Paul Kagame. Tunaweza kuwa na katiba nzuri kabisa lakini uvivu wetu ukaendelea kuwa ndio chanzo cha umaskini wetu.
 
Ndugu August, kama hukukusudia kupotosha kwa bandiko lako hili basi uelewa wako kwenye haya mambo bado ni mdogo.

Naona umetaja tu bila urari wala mantiki USSR ya Gorbachev na Ujerumani ya Hitler kama mifano yako 'bila katiba mpya", tena kwako hata dikteta fisadi Putin pia ni role model wa maendeleo.

Nigependa tuwe na mjadala mpana na sio propaganda, lakini kabla sijaenda mbele, je unajua Maendeleo ya Korea Kusini, Malaysia, Singapore, Ghana na Kenya yalipatikanaje?

Nchi kama Ujerumani na USSR (ulizotaja) na China uliyoitaja kwenye heading ni nchi/tawala/dola za zamani ni sawa sawa na tungesema Ufaransa, Japan na Canada au hata India, hao sio saizi yetu pia sio "rika" letu. Lakini hizo nchi nilizotaja hapo juu ni "rika" moja na sisi hivyo kama ni kujipima hao watatupa matokea halisi na yenye kushabihiana na sisi kama Taifa.
Kwa kifupi urusi walifanya mabadiliko ya kisiasa ndio hiyo Glasnot or openness au ndio democracy yao matokeo Yake nchi ikasambaratika Na uchumi kupokwa Na baadhi Yao, China wao walianza Na economic reforms Na Leo hii wapo hapo walipo.
Ukija Kwa issue ya ujerumani, walikuwa Na Hitler Na maendeleo yao Na Nguvu Za kuzipiga nchi zingine Na baadae kutawala mpaka huku afrika hivyo utaona kiini cha hayo maendeleo Na Nguvu Za kiuchumi zimeanzia na uzalishaji Na sio democracy. Mambo hata ya democracy ya nakuja baada ya kuwa Na maendeleo Na uchumi wenye kuweza kuwapa elimu , matibabu bora watu wetu Na kufadhili hivyovyama Na institution zingine Za nchi.
Ukija Kwa hizo nchi iwe Malaysia, South Korea , Kenya , India nk , maendeleo Yao haya kutokea Kwa sababu ya Democracy Bali sababu zingine, mfano India baada ya kutawaliwa Na uingereza walipata elimu au expose ambao sisi hatukuwa nayo Na elimu nyingine ni brutality iliyokuwepo India kabla ya ukoloni Na baadaya ya ukoloni Ktk uzalishaji .
Ukija Kwa South Korea , Malaysia , Singapore vs Tanzania , Bado tunakuja kwenye historical background zao Na si democracy , Nyerere alijaribu kwenye hilo eneo la uzalishaji lakini miundo mbinu yetu ilikuwa mibovu Na uelewa au expose Za watu wengi ilikuwa bado Na pia kutokuwepo Na changamoto Za kiuchumi Kwa watu wetu kuliwafanya watu wachukulie mambo mengi Poa tu ili mradi mtu ana Ardhi tele Na chakula. Waliokuwa Na expose Tz ni waliokwenda vitani Akina Sykes , Na walioenda Shule nje Kama uingereza nk .Ukija Kwa Ghana Na Kenya ni vizuri ukaelewa historical Za ukoloni Ktk nchi hizo kulinganisha Na huo ukoloni Tz Na sio kwamba democracy ndio imeleta hayo maendeleo. Na ukiongezea uwekezaji wetu kwenye liberation struggle Na pia kubaniwa mambo Fulani ya kibiashara Kwa sababu ya misimamo yetu ya kufinance liberation struggle
 
katiba ya china inasema ataefanya ufisadi adhabu yake ni kunyongwa mpk kufa ....sasa mpk hpo huoni katiba yao imewasaidia kupiga hatua kwa kukomesha ufisadi na rushwa? Tanzania still tunacheka na wezi wetu na wengine tumewapa vyeo bungeni
Lakini pia mafisadi Na wengine wanaopinga democracy tunao Ktk vyama vyetu lakini wao wanataka hiyo democracy iwafikishe kwenye nafasi ya juu ya uongozi ili watumize malengo Yao binafsi Kwa mlango wa Democracy , mfano Katibu wa Cafu, Maalim , Mwenyekiti wa Chadomo Na zaidi ya hapo shule Hana Na sisijui ndio akiwa Raisi ataitisha mwalimu ikulu apate degree, Na masters Kwa mpigo. Au ndio atapata fursa ya kufanya udikteta wake Kama anavyo fanya kwenye Chama Na kuikabidhi nchi Kwa wafadhili wake
 
Tatizo Lenu munapotajiwa Ujerumani, munaunganisha moja kwa moja Hitler. Hamujui kuwa Enzi za Hitler wajerumani wengi walikuwa wahanga kama walivyo wahanga Watanzania wengi kwenye utawala huu wa awamu ya tano.
Baada ya Vita vya Dunia Wjerumani walipoteza Kila kitu walichokua nacho na Wakaanza tena upya. Kama unakumbuka Ujerumani iligawanya na West Germany iliokuwa na Demokrasia na East Germany ya Kina Mkuruzia. Sasa hapo ndio ungelipima ipi iliendelea?
Kuna documentary moja ya Muscolini inaitwa My Italia inavyoelezea uongozi wake Na sio democracy ulivyoweza kuleta maendeleo Italia na kubadili sehemu zenye matete kuwa Na Ma ghorofa.
Kuhusu ujerumani lete historia ya ujerumani kabla ya hitler ikionyesha kwamba democracy ndio iliwafikisha hapo Na pia Kama upatikanaji wa Hitler ulikuwa wa kimapinduzi Na sio Kwa njia ya kidemocracia Na Kama alivunja katiba Yao Ktk kuleta vita ya kwanza Na ya pili
 
Lakini pia mafisadi Na wengine wanaopinga democracy tunao Ktk vyama vyetu lakini wao wanataka hiyo democracy iwafikishe kwenye nafasi ya juu ya uongozi ili watumize malengo Yao binafsi Kwa mlango wa Democracy , mfano Katibu wa Cafu, Maalim , Mwenyekiti wa Chadomo Na zaidi ya hapo shule Hana Na sisijui ndio akiwa Raisi ataitisha mwalimu ikulu apate degree, Na masters Kwa mpigo. Au ndio atapata fursa ya kufanya udikteta wake Kama anavyo fanya kwenye Chama Na kuikabidhi nchi Kwa wafadhili wake

stick kwenye mada please!!!!! mada ni mchango wa demokrasia ktk kuleta maendeleo na umetolea mfano china!! sasa wakina mbowe na maalim seif wameingiaje hpa?
 
Kuna documentary moja ya Muscolini inaitwa My Italia inavyoelezea uongozi wake Na sio democracy ulivyoweza kuleta maendeleo Italia na kubadili sehemu zenye matete kuwa Na Ma ghorofa.
Kuhusu ujerumani lete historia ya ujerumani kabla ya hitler ikionyesha kwamba democracy ndio iliwafikisha hapo Na pia Kama upatikanaji wa Hitler ulikuwa wa kimapinduzi Na sio Kwa njia ya kidemocracia Na Kama alivunja katiba Yao Ktk kuleta vita ya kwanza Na ya pili
oK; SASA nakupa dondoo Za Hitler.
Kwanza Hitler sio Mjerumani , Alizaliwa Austria, Jina lake hasa akiitwa Schickelgrube. Yeye Alikuwa ni Myahudi, na ndio Ukweli uliofichwa ambao hausemwi. Alikuwa na ugomvi tokea udogo wake na Mama yake ambaye alikuwa Kahaba. Baada ya Kukua akaanza kujifunza Uchawi (Jinsi ya Kumanipulate watu). Alipomaliza skuli alienda Italy kusoma Zaidi Mambo ya Uchawi na Uchoraji. Hile Nembo yao aliichora mwenyewe.. Kutoka na na Ugonvi na Mama yake alikuwa akiwachukia sana Wayahudi. Wakati Ujerumani Mabenki yote, na Maduka ya dhahabu yakimilikiwa na wayahudi.
Gia aliyoingilia Ujerumani ni kuwa yeye ni Mtetezi wa Wanyonge, anataaka kuwakomboa Wajerumani kutoka kwa Wayahudi. Jambo kubwa lilikuwa likiwaudhi wajerumani Unapotaka kukopa Lazima uwende kwa Wayahudi na lazima uweke vitu vyako vya Thamani rehani. Wakati mwengine baada ya mwaka unazirudisha zile Pesa, malizako unazikosa Pengine unadaiwa kwa Riba.
Hapo ndipo Hitler alipoweza kuwamanipulate Wajerumani.
Sasa hii Hadithi ya Hitler inanikumbusha ya Babu yenu Munayemtetea hapo TZ , yeye ni mtetezi wa Wanyonge lakini huthubutu kumhoji, ukihoji umepotea.
Waulize watu walioku Austria watakuelza kua nyumba aliozaliwa Hitler mpaka Leo ipo imewekwa Ukumbusho
 
Kumekuwepo na kelele kiasi toka kwa baadhi ya Watu ambao wanataka kufunganisha maendeleo ya Nchi yetu na Katiba Mpya au kwa kifupi maendeleo yanaendana na Katiba wanazofikiria wao zitawapa ''fursa''

Kwa mfano ndani ya KKKT tumeshihudia migogoro kadha sasa sijui wao Hiyo katiba mpya wataianzisha lini?

Na kuna viongozi wa Kiroho ambao utajiri wao unatokana na kuwadhulumu waumini wao kwa njia moja au nyingine ndio Maana hutakuta vitabu vyao vya mahesabu kuwa wazi zaidi ya kuwa somea waumini wao taarifa wanazo taka wao.

Ukija kwenye vyama vya siasa hadithi ni Hiyo Hiyo wakati wao wenyewe demokrasia wanayo ipigia kelele hawaienzi.

Ukija kwenye Suala la Maendeleo mfano china na mabadiliko Yao ya kiuchumi tunaona wame weza kufanya hivyo bila vyama vingi Bali kwa kuimarisha mifumo Yao ya kiutendaji wakati urusi walikwenda na Glasnot matokeo yake sote tunayajua Gorbachev akakosa nchi na Yeltsin na ulevi wake Ndio aka tawala nchi , matokeo yake nchi ilipojitambua wakamleta Putin ambaye Yupo madarakani kwa miongo miwili sasa.

Ukija hizo nchi za ulaya iwe Germany ya Hitler na wengineo tuangalie walivyo piga hatua za maendeleo ilikuwa kwa sababu ya katiba mpya au demokrasia au lilikuwa ni suala la uzalishaji na usimamiaji wa itikadi inayolenga ktk maendeleo.

Mimi nionavyo tupate maendeleo kwanza Ndio tutaweza kuweka hizo rangi zingine kulemba maendeleo yetu na sio kulemba kitu ambacho hatuna.


Kuna nchi gani ina maendeleo bila katiba?

Shida yako ni katiba au katiba mpya?

Katiba na Katiba Mpya ni concept mbili ambazo ni contradiction!

Sijui "umri" wa katiba ya nchi una shida gani na maendeleo ya nchi?

Ubora wa katiba ndio topic hapa...

Sijui kwanini Ccm wanapenda kupaka mavi mahali ambapo sio lazima!
 
Umeenda mbali mpk china....embu jaribu kuchek katiba ilivyobadilisha kila kitu hapo Kenya
We unadhan tunahitaj katiba mpya kwa ajil ya uchumi tu
 
chief kuna mahusiano makubwa kati ya katiba bora na maendeleo!. Marekani ndyo taifa tajiri duniani lkn ukiangalia siri ya mafanikio yao, utagundua ubora wa katiba yao umechangia pakubwa . katiba inayosisitiza nchi kwanza hlf maslahi ya mtu mmoja mmoja ndyo yanafuata sio huku bongo rais kapewa madaraka makubwa mpk anaamua kujenga airport kwao ambayo ni useless huku wanafunzi wanasomea nje kwa kukosa madarasa
Mkuu pamoja na hoja zako kuwa afadhali,lakini bado hata hiyo marekani inayoipigia chapua humu ndani fikra za mti mmoja bado ndio msingi wa uongozi.
Nitakutolea mfano,hakuna ibara ye yote ya katiba ya marekani inayotaka mipaka yake izungudhiwe ukuta ili kunyima fulsa watu wa mataifa mengine wasiingie nchi hiyo.
Kuanzia wakati wa kampeni mpaka kuingia white house rais trump ameweka ukuta kutenganisha nchi mbili jirani,sio katiba iloliyoweka sharti bali mtu.
Kuingia mfumo wa vyama vingi tanzania wanachi waliukataa kwa kupiga kura.
Lakini mtu anayeitwa mwalimu nyrere akasema wakati umefika wa kuwa na vya vingi ikawa halikuwa takwa la kikatiba bali mtu.

Tulipokosa ndege kwa muda mrefu,serikali zilizopita pamoja na kuona umuhimu wa nchi kuwa na ndege hawakufanya hivyo,alipoingia rais magufuli ameleta ndege,halikuwa takwa la kikatiba bali mtu.
Kwa hiyo kuna uhusiano mkubwa sana kati ya maendeleo na mtu aliyeko juu kuamua mustakabali wa hali ya nchi.
 
Kama kuna nchi wanatakiwa wakajifunze democrasia ni wamarekani. Maana democrasia wao ni kwa ngozi nyeupe, black amerikan wanahesabika kama mbwa fu. Ndo maana mzungu haoni shidha kumshut black american kuliko kumshut mbwa. Na ukitoka nje ya mipaka ya marekani wao they are more wrose than african dictators
 
Ukija Kwa South Korea , Malaysia , Singapore vs Tanzania , Bado tunakuja kwenye historical background zao Na si democracy , Nyerere alijaribu kwenye hilo eneo la uzalishaji lakini miundo mbinu yetu ilikuwa mibovu Na uelewa au expose Za watu wengi ilikuwa bado Na pia kutokuwepo Na changamoto Za kiuchumi Kwa watu wetu kuliwafanya watu wachukulie mambo mengi Poa tu ili mradi mtu ana Ardhi tele Na chakula. Waliokuwa Na expose Tz ni waliokwenda vitani Akina Sykes , Na walioenda Shule nje Kama uingereza nk .Ukija Kwa Ghana Na Kenya ni vizuri ukaelewa historical Za ukoloni Ktk nchi hizo kulinganisha Na huo ukoloni Tz Na sio kwamba democracy ndio imeleta hayo maendeleo. Na ukiongezea uwekezaji wetu kwenye liberation struggle Na pia kubaniwa mambo Fulani ya kibiashara Kwa sababu ya misimamo yetu ya kufinance liberation struggle

Nani aliyekudanganya kuwa "ideology furtherance" ni economic investment? Mwl. Nyerere alikosea sana na leo hii tunakula na kuvuna alichopanda iwe kisiasa au kiuchumi. Yeye alikuwa anapeleka/anaeneza Ujamaa kwa kutumia bendera/slogan ya "ukombozi", lakini je hivi huoni upungufu wa kujaribu kukomboa wengine wakati wewe mwenyewe hujajikomboa? Hebu nikuulize, kati ya Tanzania na Kenya je ni nani anayefaidika SASA na Angola au Mozambique kisiasa au kibiashara? Na je ukienda South Africa wewe na Mkenya je kuna privileges zozote utakazopewa tofauti na Mkenya? Acheni kuishi kwenye ndoto na masimulizi ya ki-Abunuwasi. Sera ya "Ukombozi" ilikuwa ni political miscalculation na pia economic suicide.

Nchi zote makini zilijikita kujijenga kiuchumi, kisiasa na kidplomasia baada ya uhuru. Sisi tulikuwa kama mtu asiyejali nyumba yake bali aliyejihusisha na mambo ya jirani zake. Baada ya muda kupita, waliowekeza kwenye uchumi na diplomasia wakatupita mbali na sisi tukabaki na tambo za kishamba. Maisha ni leo na sio jana, kuishi jana leo ni mentality za losers. Mipango ni ya kesho sio ya juzi, hivyo kuishi kwa historia inamaanisha wewe ni mfu, NO FUTURE.

NB: Samahani kama nimekukwaza kwa matumizi ya baadhi ya maneno, kwani hilo halikuwa lengo langu.
 
Kumekuwepo na kelele kiasi toka kwa baadhi ya Watu ambao wanataka kufunganisha maendeleo ya Nchi yetu na Katiba Mpya au kwa kifupi maendeleo yanaendana na Katiba wanazofikiria wao zitawapa ''fursa''

Kwa mfano ndani ya KKKT tumeshihudia migogoro kadha sasa sijui wao Hiyo katiba mpya wataianzisha lini?

Na kuna viongozi wa Kiroho ambao utajiri wao unatokana na kuwadhulumu waumini wao kwa njia moja au nyingine ndio Maana hutakuta vitabu vyao vya mahesabu kuwa wazi zaidi ya kuwa somea waumini wao taarifa wanazo taka wao.

Ukija kwenye vyama vya siasa hadithi ni Hiyo Hiyo wakati wao wenyewe demokrasia wanayo ipigia kelele hawaienzi.

Ukija kwenye Suala la Maendeleo mfano china na mabadiliko Yao ya kiuchumi tunaona wame weza kufanya hivyo bila vyama vingi Bali kwa kuimarisha mifumo Yao ya kiutendaji wakati urusi walikwenda na Glasnot matokeo yake sote tunayajua Gorbachev akakosa nchi na Yeltsin na ulevi wake Ndio aka tawala nchi , matokeo yake nchi ilipojitambua wakamleta Putin ambaye Yupo madarakani kwa miongo miwili sasa.

Ukija hizo nchi za ulaya iwe Germany ya Hitler na wengineo tuangalie walivyo piga hatua za maendeleo ilikuwa kwa sababu ya katiba mpya au demokrasia au lilikuwa ni suala la uzalishaji na usimamiaji wa itikadi inayolenga ktk maendeleo.

Mimi nionavyo tupate maendeleo kwanza Ndio tutaweza kuweka hizo rangi zingine kulemba maendeleo yetu na sio kulemba kitu ambacho hatuna.
China watu kama kina Chenge hawapewi uenyekiti na nafasi za ubunge wananyongwa
 
Kumekuwepo na kelele kiasi toka kwa baadhi ya Watu ambao wanataka kufunganisha maendeleo ya Nchi yetu na Katiba Mpya au kwa kifupi maendeleo yanaendana na Katiba wanazofikiria wao zitawapa ''fursa''

Kwa mfano ndani ya KKKT tumeshihudia migogoro kadha sasa sijui wao Hiyo katiba mpya wataianzisha lini?

Na kuna viongozi wa Kiroho ambao utajiri wao unatokana na kuwadhulumu waumini wao kwa njia moja au nyingine ndio Maana hutakuta vitabu vyao vya mahesabu kuwa wazi zaidi ya kuwa somea waumini wao taarifa wanazo taka wao.

Ukija kwenye vyama vya siasa hadithi ni Hiyo Hiyo wakati wao wenyewe demokrasia wanayo ipigia kelele hawaienzi.

Ukija kwenye Suala la Maendeleo mfano china na mabadiliko Yao ya kiuchumi tunaona wame weza kufanya hivyo bila vyama vingi Bali kwa kuimarisha mifumo Yao ya kiutendaji wakati urusi walikwenda na Glasnot matokeo yake sote tunayajua Gorbachev akakosa nchi na Yeltsin na ulevi wake Ndio aka tawala nchi , matokeo yake nchi ilipojitambua wakamleta Putin ambaye Yupo madarakani kwa miongo miwili sasa.

Ukija hizo nchi za ulaya iwe Germany ya Hitler na wengineo tuangalie walivyo piga hatua za maendeleo ilikuwa kwa sababu ya katiba mpya au demokrasia au lilikuwa ni suala la uzalishaji na usimamiaji wa itikadi inayolenga ktk maendeleo.

Mimi nionavyo tupate maendeleo kwanza Ndio tutaweza kuweka hizo rangi zingine kulemba maendeleo yetu na sio kulemba kitu ambacho hatuna.
 
Demokrasia na mbwembwe za katiba ni vitu ambavyo hutumika katika kuendeleza umasikini wa bara la Afrika.

Rwanda hawana katiba nzuri lakini tazama mambo aliyoyafanya Paul Kagame. Tunaweza kuwa na katiba nzuri kabisa lakini uvivu wetu ukaendelea kuwa ndio chanzo cha umaskini wetu.

..China na Rwanda "wamefanikiwa" huku wakiwa na katiba mbaya na sheria kandamizi.

..Tanzania tuna katiba mbaya. Pia mfumo wa vyama vingi upo ktk makaratasi tu, but in practice tunaendeshwa kama nchi ya chama kimoja--CCM.

..Kwa msingi huo basi unapozungumzia katiba, demokrasia, haki, na utawala bora, Tanzania inafanana na China na Rwanda.

..Sasa mfumo tulionao umekuwepo tangu miaka ya 60. Sote tunajua kwamba mfumo huo umeikwamisha nchi ktk tope la UMASIKINI. JE, kwanini tusibadilike?
 
Hatuji ila tutasema. Maendeleo ya China yameletwa na uongozi bora. Maendeleo ya Rwanda yameletwa na uongozi bora. Mwalimu alisema: "Ili tuendelee tunahitaji watu siasa safi na uongozi bora." Hakusema na katiba mpya. Maendeleo ya Tanzania yataletwa na uongozi bora. Watu wakiuunga mkono uongozi wa Awamu ya 5, kama walivyounga mkono uongozi wa awamu zote tutapata maendeleo. Tunaona itihada za Raisi wa awamu ya 5 katika kuleta uongozi bora nchini.Bial shaka hatua za kuelekea kupata maendeleo zimekwisha anza kuonekana.
Uanjua maana ya neno siasa? Kama hulijui basi katiba ndio msingi mkuu wa siasa yenyewe. Kama unadhani kusimama majukwaani na kupiga kelele tu ndio siasa basi unahitaji kuelimishwa zaidi! Hata huko kusimama majukwaani na kupiga kelele kwa viongozi wa nchi na wa vyama vya siasa na hata asasi za kiraia ni kwa mujibu wa katiba. Katiba ndio inawapa huo uhuru wa kuongea! Katiba ndiyo kiini au msingi wa nchi katika kuendesha mambo yake yote ya nchi kuanzia uongozi, demokrasia, elimu, afya, uchumi, utamaduni, michezo & burudani, miundombinu, uchumi wa nchi n.k.

Hivyo SIASA (ambayo ni mfumo wa kuendesha nchi kwa ujmla wake) ni zao la katiba. Huu mfumo wa kuendesha nchi aka S.I.A.S.A imebebwa na katiba ya nchi. Uongozi wa nchi yetu unaongozwa na katiba yetu ya sasa bila kujali ni nzuri ama si nzuri maana ndiyo katiba iliyopo na inayotumika kwa hiyo siasa ya nchi yetu imebebwa au imeanishwa na katiba ya nchi.

Kama katiba isingekuwa na umuhimu kwa maendeleo na usitawi wa taifa letu kwa nini ipo? Kwa nini Rais wa nchi na viongozi mbalimbali wa serikali na hata waheshimiwa wabunge wanaapa kuilinda katiba ya nchi yetu kama haina umuhimu kwa taifa letu? Wanaapa kulinda kitu ambacho hakina umuhimu kwa maendeleo ya taifa? Loooh ama kweli ukistaajabu ya Musa utayaona ya Firauni!

NDUGU FUNGUKA KUTOKA HUKO KIFUNGONI KWENYE LINDI LA UTAPIA MLO WA KIKATIBA!
 
Back
Top Bottom