Steven Robert Masatu
JF-Expert Member
- Aug 7, 2009
- 2,458
- 1,821
Kosa la Muhando liko wapi hapo sasa?
umeongea kidoogo sana
hebu jaza thread aisee
Hapana ndugu yangu, mengi yashasemwa tayari, nime edit kidogo kumwomba mzee Mhando anywe chai apishe uchunguzi uendelee kama hana kosa la kujibu atarudi tu....
nami nina the same swali,
hiyo kampuni kama imefuata taratibu zote na imeshindanishwa kama sheria za manunuzi zinavyotaka mimi sion ubaya wowote wa mhando.
ebu mleta mada na wachangiaji wenzagu mnifafanulie hili suala.
Mhando anahujumiwa na vigogo wizarani ilo lipo wazi..na hii stor imeletwa na wahusika jamaa alikuwa anasimamia haki na ukweli apa tanesco dat y anapgwa vta.
Kiranga ktk sheria hakuna kosa la Conflic of interest, linaweza kuwa tatizo lakini sio kosa. Viongozi wote wanatumia nyadhifa zao kuendesha biashara kupitia watoto, wake, ndugu namarafiki maadam hawaibi..Tatizo hapa kuna conflict of interest. Mhando hawezi kuwa na kampuni ya familia yake inashindania zabuni katika kampuni ya umma anayoiongoza halafu tukasema "kampuni imefuata taratibu zote na imeshindanisha kama sheria za manunuzi zinavyotaka".
Wakati Wizara ya Nishati na Madini ikitarajiwa kuwasilisha bajeti yake kwa mwaka wa Fedha 2012/2013, mvutano miongoni mwa wabunge umezidi kutanuka kiasi cha kuhatarisha mjadala wa bajeti ya wizara hiyo.
Lakini wakati hali hiyo ya mvutano ikibainika miongoni mwa wabunge, kile kinachoelezwa kuwa ni mvutano kati ya viongozi wa Wizara ya Nishati na Madini kwa upande mmoja na viongozi wa TANESCO waliosimamishwa umechukuwa sura mpya, ikielezwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO (aliyesimamishwa), William Mhando, ana maslahi katika zabuni ya kusambaza vifaa vya ofisi ya kampuni ya mkewe, Eva Mhando inayoitwa Santa Clara Supplies Co. Ltd.
Kampuni hiyo ya Santa Clara Supplies Limited inadaiwa kupewa mkataba wa Sh.884,550,000 na TANESCO kwa ajili ya kusambaza vifaa hivyo.
Lakini akizungumza ofisini kwa Raia Mweam jana Jumanne, Mhando alikiri kuitambua kampuni hiyo si mali ya familia yake bali mkewe, Eva ambaye awali alikuwa akifanya kazi TANESCO ndiye ameajiriwa na kampuni hiyo.
KAMPUNI KUPEWA ZABUNI:
Taarifa zilizotufikia zinaeleza kuwa Mhando, akiwa Mkurugenzi wa TANESCO, bila kujali mgingano wa kimaslahi aliacha mchakato wa kuipa zabuni kampuni hiyo uendelee na hatimaye kampuni hiyo ikashinda zabuni hiyo ya kusambaza vifaa vya ofisi kwa TANESCO.
Mhando anadaiwa kuipa kampuni hiyo iliyosajiliwa April 04, 2011, taarifa zaidi zikieleza kuwa, kampuni hiyo ilianza na mataji wa Sh. Miliomi kumi na wanahisa wake ni Fred Willliam, Veronica William na Steven William na kwa mujibu wa usajili wa kampuni hiyo, wanahisa hao pia ni makaimu wakurugenzi.
Maelezo ya usajili wa kampuni hiyo ya Santa Clara Supplies Co. Ltd, ambayo Raia Mwema imefanikiwa kuyaona, yanaonyesha kuwa ipo katika kitalu namba 204, Wilaya ya Ilala jijini Dar es salaam.
Kwenye orodha ya wanahisa na makaimu wakurugenzi wa kampuni hiyo majina ya Fred na Veronica, yamebainika kuwa ni watoto wa Mhando.
MAJIBU YA MHANDO.
Katika kufafanua kuhusu suala hilo, Mhando alisema wakati akiwa TANESCO katika ngazi za chini alikuwa akifanya kazi katika shirika hiloo na mkewe, Eva.
Hata hivyo kwa mujibu wa maelezo yake, mara baada ya kuteuliwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa shirika hilo pekee la kusambaza umeme nchini, Wizara ya Nishati na Madini, ilimwandikia barua ya kutaka mkewe aachishwe kazi ili kuepusha uwezekano wa kuwapo kwa mgongano wa kimaslahi.
Mke wangu aliacha kazi, lakini tulikuwa na kampuni hiyo ya stationery Kariakoo na kwa sababu biashara haikuwa nzuri kutokana na uwezo mdogo wa kifedha, tuliuza kampuni hiyo mwaka jana.
Mke wangu aliajiriwa tu katika kampuni hiyo baada ya kununuliwa ili waweze kutumia uzoefu wake katika kuiendesha.
Sasa kwa nafasi ya mke wangu, yeye ni Mtendaji wa hiyo kampuni lakini shughuli zote za kutafuta shughuli zote za kutafuta zabuni zinafanywa na wakurugenzi wa kampuni hiyo, si mke wangu.
Kwahiyo, walipoomba kazi TANESCO hatua zote zilifanyika kwa mujibu wa taratibu, kanuni na sharia na kampuni hiyo ilishandanishwa na kampuni nyingine na hatimaye ikashinda, alisema Mhando.
NB: KWA MAELEZO ZAIDI, UKITAKA KUFAHAMU SINTOFAHAMU YA BUNGE NA SAKATA LA MHANDO, SOMA SOURCE YA HABARI HII-GAZETI LA RAIA MWEMA, July 25,2012.
MY TAKE:
Wale wanaomtetea Fisadi Chipukizi William Mhando, jaribuni kutetea na uozo huu....!!
Kiranga ktk sheria hakuna kosa la Conflic of interest, linaweza kuwa tatizo lakini sio kosa. Viongozi wote wanatumia nyadhifa zao kuendesha biashara kupitia watoto, wake, ndugu namarafiki maadam hawaibi..
Hii ndio Bongo yetu karibu sana!.
mtotowamjini
ku manage tanesco kwanini wasiibinafsishe?
Lakini mkuu wangu tuseme ukweli Conflict of interest haina busara wala kutokuwa na busara. Hiatakiwi kumpa mnmtu nafasi ya kufanya madudu haya na ndio maana ya kuwepo miiko na maadili ya Uongozi sio kuwa na tume ya maadili.. Sisi Watanzania tunafanya kila kitu kinyume cha busara halafu tunaitafuta busara kweli hiyo busara itapatikana wapi?Ni busara tu ya kufanya haya unayoyasema sio makosa na ukipungukiwa busara basi ndo conflict hutokea na kuonekana..............so it is upon the one in position to be wise or to figure out and paint the so called conflict of interest
NasDaz,
..nadhani huyu jamaa kawanyima wenzake ulaji ndiyo maana yote haya yanaibuka.
..kuna mahali nimesoma kwamba Katibu Mkuu Nishati naye ana "watu wake" ambao wana-supply mafuta mazito Tanesco.
..ninachoona sasa hivi ni juhudi za kulipuana tu kati ya Wizara na Tanesco. Sioni mahali popote ambapo wahusika wamejielekeza kutatua tatizo la MGAO WA UMEME ambao umedumu toka miaka ya 90.
Kiranga ktk sheria hakuna kosa la Conflic of interest, linaweza kuwa tatizo lakini sio kosa. Viongozi wote wanatumia nyadhifa zao kuendesha biashara kupitia watoto, wake, ndugu namarafiki maadam hawaibi..
Hii ndio Bongo yetu karibu sana!.
Wakati Wizara ya Nishati na Madini ikitarajiwa kuwasilisha bajeti yake kwa mwaka wa Fedha 2012/2013, mvutano miongoni mwa wabunge umezidi kutanuka kiasi cha kuhatarisha mjadala wa bajeti ya wizara hiyo...........................................Mke wangu aliacha kazi, lakini tulikuwa na kampuni hiyo ya stationery Kariakoo na kwa sababu biashara haikuwa nzuri kutokana na uwezo mdogo wa kifedha, tuliuza kampuni hiyo mwaka jana.
Mke wangu aliajiriwa tu katika kampuni hiyo baada ya kununuliwa ili waweze kutumia uzoefu wake katika kuiendesha.
Sasa kwa nafasi ya mke wangu, yeye ni Mtendaji wa hiyo kampuni lakini shughuli zote za kutafuta shughuli zote za kutafuta zabuni zinafanywa na wakurugenzi wa kampuni hiyo, si mke wangu.
Kwahiyo, walipoomba kazi TANESCO hatua zote zilifanyika kwa mujibu wa taratibu, kanuni na sharia na kampuni hiyo ilishandanishwa na kampuni nyingine na hatimaye ikashinda, alisema Mhando.
Kwangu haifunguki sijui kwa nini?..Kwani inasemaje hiyo 37 (6)Angalia "The Public Procurement Act, 2004" 37 (6) halafu utuambie kama Mhando ali declare conflict of interest according to this law.
Sheria imesema wazi, sielewi unaposema "hakuna kosa la conflict of interest" una maana gani.
Kwangu haifunguki sijui kwa nini?..
Kiranga ktk sheria hakuna kosa la Conflic of interest, linaweza kuwa tatizo lakini sio kosa. Viongozi wote wanatumia nyadhifa zao kuendesha biashara kupitia watoto, wake, ndugu namarafiki maadam hawaibi..
Hii ndio Bongo yetu karibu sana!.
Lakini mkuu wangu tuseme ukweli Conflict of interest haina busara wala kutokuwa na busara. Hiatakiwi kumpa mnmtu nafasi ya kufanya madudu haya na ndio maana ya kuwepo miiko na maadili ya Uongozi sio kuwa na tume ya maadili.. Sisi Watanzania tunafanya kila kitu kinyume cha busara halafu tunaitafuta busara kweli hiyo
busara itapatikana wapi?