Madudu mengine ya William Mhando wa TANESCO!

Status
Not open for further replies.
Hapana ndugu yangu, mengi yashasemwa tayari, nime edit kidogo kumwomba mzee Mhando anywe chai apishe uchunguzi uendelee kama hana kosa la kujibu atarudi tu....

hii imani kuwa atarudi naona imetawala sana
najiuliza why..?
 
nami nina the same swali,

hiyo kampuni kama imefuata taratibu zote na imeshindanishwa kama sheria za manunuzi zinavyotaka mimi sion ubaya wowote wa mhando.

ebu mleta mada na wachangiaji wenzagu mnifafanulie hili suala.

Tatizo hapa kuna conflict of interest. Mhando hawezi kuwa na kampuni ya familia yake inashindania zabuni katika kampuni ya umma anayoiongoza halafu tukasema "kampuni imefuata taratibu zote na imeshindanisha kama sheria za manunuzi zinavyotaka".
 
Azimio La Zanzibar limetoa ruksa na mwanya kwa viongozi kufanya biashara.. hakuna kosa hata kama shirika hilo lingekuwa kla Mhando mwenyewe maadam amefuata masharti ya Tanesco. Na ndio maana Mkapa alifungua ofisi yake Ikulu kabisaaa isiwe taabu.. Hadi siku mtakapo badilisha sheria hizi sidhani kaa tunayokesi ya kujibu..

Na mgogoro huu siku zote nasema Tanesco mnawaonea sana tu kwa sababu kama hivi. Bajeti mwapangie nyie wizara na sio Tanesco wenyewe kutengeneza, madeni hamtaki kulipia, umeme hamtaki kulipia ofisi zote za serikali nchini na sasa Zanzibar wamegoma nao kulipa halafu mnategemea Tanesco watakuwa na viongozi genius ambao wataweza kuliokoa shirika mnalolinyonya wenyewe.

Ni nyie mloingia mkataba wa IPTL ambao Tanesco leo wana matumizi zaidi ya mapato! Kuna mashirka mengine yalikuwa ya dharura tu copntarct za miaka miwili waondoke wakati tunajiandaa kuzalisha umeme wa uhakika,hakuna kitu wote wanavuta mabillioni toka Tanesco wakisingizia mafuta ghali kuliko gas tuwaletee nayo..

Hii ni mitambo yao sii ya Tanesco kwa nini tuvute gas kuendesha mitambo ya haya mashirika ya dharura badala ya kujenga mitambo yetu na kuikabidhi tanesco ili kujiondoa ktk mikataba mibovu ya IPTL na meingineyo iliyokuwa ya dharura?. Hivi kweli tunavuta gas kutoka Songo na Mtwara ili ku feed mitambo ya hawa jamaa wanaotumaliza kila siku na bei za ajabu halafu mnasema Tanesco ndio wapiga ma deal. Nani atakayelipia gharama za ujenzi wa bomba hilo kama sio Tanesco na wananchi hayo mashirika hayatalipa hata senti maana yapo kwa dharura tu miaka inaondoka. Kina nani waloyachugua haya mashirika yanayozalisha umeme kwa mafuta?.
 
Mhando anahujumiwa na vigogo wizarani ilo lipo wazi..na hii stor imeletwa na wahusika jamaa alikuwa anasimamia haki na ukweli apa tanesco dat y anapgwa vta.

Risasi vitani humpata aliye mbele ya mtutu......naye kakaa upande huho huo

So hata kama alikuwa anasimamia haki kwa kupiga mstri chini ya majina saa mbili kasorobo asubuhi huku tenda zikiwa za mchongo huu......bado man kazi ya kutuelewesha vinginevyo
 
Tatizo hapa kuna conflict of interest. Mhando hawezi kuwa na kampuni ya familia yake inashindania zabuni katika kampuni ya umma anayoiongoza halafu tukasema "kampuni imefuata taratibu zote na imeshindanisha kama sheria za manunuzi zinavyotaka".
Kiranga ktk sheria hakuna kosa la Conflic of interest, linaweza kuwa tatizo lakini sio kosa. Viongozi wote wanatumia nyadhifa zao kuendesha biashara kupitia watoto, wake, ndugu namarafiki maadam hawaibi..
Hii ndio Bongo yetu karibu sana!.
 
Wakati Wizara ya Nishati na Madini ikitarajiwa kuwasilisha bajeti yake kwa mwaka wa Fedha 2012/2013, mvutano miongoni mwa wabunge umezidi kutanuka kiasi cha kuhatarisha mjadala wa bajeti ya wizara hiyo.

Lakini wakati hali hiyo ya mvutano ikibainika miongoni mwa wabunge, kile kinachoelezwa kuwa ni mvutano kati ya viongozi wa Wizara ya Nishati na Madini kwa upande mmoja na viongozi wa TANESCO waliosimamishwa umechukuwa sura mpya, ikielezwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO (aliyesimamishwa), William Mhando, ana maslahi katika zabuni ya kusambaza vifaa vya ofisi ya kampuni ya mkewe, Eva Mhando inayoitwa Santa Clara Supplies Co. Ltd.

Kampuni hiyo ya Santa Clara Supplies Limited inadaiwa kupewa mkataba wa Sh.884,550,000 na TANESCO kwa ajili ya kusambaza vifaa hivyo.

Lakini akizungumza ofisini kwa Raia Mweam jana Jumanne, Mhando alikiri kuitambua kampuni hiyo si mali ya familia yake bali mkewe, Eva ambaye awali alikuwa akifanya kazi TANESCO ndiye ameajiriwa na kampuni hiyo.

KAMPUNI KUPEWA ZABUNI:

Taarifa zilizotufikia zinaeleza kuwa Mhando, akiwa Mkurugenzi wa TANESCO, bila kujali mgingano wa kimaslahi aliacha mchakato wa kuipa zabuni kampuni hiyo uendelee na hatimaye kampuni hiyo ikashinda zabuni hiyo ya kusambaza vifaa vya ofisi kwa TANESCO.

Mhando anadaiwa kuipa kampuni hiyo iliyosajiliwa April 04, 2011, taarifa zaidi zikieleza kuwa, kampuni hiyo ilianza na mataji wa Sh. Miliomi kumi na wanahisa wake ni Fred Willliam, Veronica William na Steven William na kwa mujibu wa usajili wa kampuni hiyo, wanahisa hao pia ni makaimu wakurugenzi.

Maelezo ya usajili wa kampuni hiyo ya Santa Clara Supplies Co. Ltd, ambayo Raia Mwema imefanikiwa kuyaona, yanaonyesha kuwa ipo katika kitalu namba 204, Wilaya ya Ilala jijini Dar es salaam.

Kwenye orodha ya wanahisa na makaimu wakurugenzi wa kampuni hiyo majina ya Fred na Veronica, yamebainika kuwa ni watoto wa Mhando.

MAJIBU YA MHANDO.

Katika kufafanua kuhusu suala hilo, Mhando alisema wakati akiwa TANESCO katika ngazi za chini alikuwa akifanya kazi katika shirika hiloo na mkewe, Eva.

Hata hivyo kwa mujibu wa maelezo yake, mara baada ya kuteuliwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa shirika hilo pekee la kusambaza umeme nchini, Wizara ya Nishati na Madini, ilimwandikia barua ya kutaka mkewe aachishwe kazi ili kuepusha uwezekano wa kuwapo kwa mgongano wa kimaslahi.

“Mke wangu aliacha kazi, lakini tulikuwa na kampuni hiyo ya stationery Kariakoo na kwa sababu biashara haikuwa nzuri kutokana na uwezo mdogo wa kifedha, tuliuza kampuni hiyo mwaka jana.

Mke wangu aliajiriwa tu katika kampuni hiyo baada ya kununuliwa ili waweze kutumia uzoefu wake katika kuiendesha.

“Sasa kwa nafasi ya mke wangu, yeye ni Mtendaji wa hiyo kampuni lakini shughuli zote za kutafuta shughuli zote za kutafuta zabuni zinafanywa na wakurugenzi wa kampuni hiyo, si mke wangu.

“Kwahiyo, walipoomba kazi TANESCO hatua zote zilifanyika kwa mujibu wa taratibu, kanuni na sharia na kampuni hiyo ilishandanishwa na kampuni nyingine na hatimaye ikashinda,” alisema Mhando.


NB: KWA MAELEZO ZAIDI, UKITAKA KUFAHAMU SINTOFAHAMU YA BUNGE NA SAKATA LA MHANDO, SOMA SOURCE YA HABARI HII-GAZETI LA RAIA MWEMA, July 25,2012.

MY TAKE:
Wale wanaomtetea Fisadi Chipukizi William Mhando, jaribuni kutetea na uozo huu....!!

Kwa maelezo ya magazeti yetu ni vema unaposoma ujitahidi kukaa jirani na maziwa maana sumu ni nyingi unaweza kupandisha presha. na pili sioni kwa nini unamchukuliaa kuwa ni mhalifu kwa mtazamo wa wajasilimali (magazeti) hebu tumuone kama mtuhumiwa.
 
Kiranga ktk sheria hakuna kosa la Conflic of interest, linaweza kuwa tatizo lakini sio kosa. Viongozi wote wanatumia nyadhifa zao kuendesha biashara kupitia watoto, wake, ndugu namarafiki maadam hawaibi..
Hii ndio Bongo yetu karibu sana!.

Ni busara tu ya kufanya haya unayoyasema sio makosa na ukipungukiwa busara basi ndo conflict hutokea na kuonekana..............so it is upon the one in position to be wise or to figure out and paint the so called conflict of interest
 
mtotowamjini
ku manage tanesco kwanini wasiibinafsishe?

Mkuu! Heshima yako! Kuibinafsisha TANESCO ni kama kumpa huyo mwekezaji bunduki akupige ufe. Uliona wapi nchi za wenzetu wanakabidhi Shirika kama hilo lichezewe na mtu binafsi? Atatamba kama wanavyotamba wauza mafuta na bei atapanga yeye na wauza mafuta. Wakati huo hata JF itakuwa haifanyi kazi. Mi niko Kenya kwa sasa. Wenzetu huku wanalisimamia Kenya Electric Power bila matatizo na hakuna kitu kama mgawo. Na hawana sources za umeme nzuri kama tulivyo nazo sisi. Sema hivi, kama wanashindwa kuimanage TANESCO waachie ngazi! Si wameshindwa?
 
Ni busara tu ya kufanya haya unayoyasema sio makosa na ukipungukiwa busara basi ndo conflict hutokea na kuonekana..............so it is upon the one in position to be wise or to figure out and paint the so called conflict of interest
Lakini mkuu wangu tuseme ukweli Conflict of interest haina busara wala kutokuwa na busara. Hiatakiwi kumpa mnmtu nafasi ya kufanya madudu haya na ndio maana ya kuwepo miiko na maadili ya Uongozi sio kuwa na tume ya maadili.. Sisi Watanzania tunafanya kila kitu kinyume cha busara halafu tunaitafuta busara kweli hiyo busara itapatikana wapi?
 
NasDaz,

..nadhani huyu jamaa kawanyima wenzake ulaji ndiyo maana yote haya yanaibuka.

..kuna mahali nimesoma kwamba Katibu Mkuu Nishati naye ana "watu wake" ambao wana-supply mafuta mazito Tanesco.

..ninachoona sasa hivi ni juhudi za kulipuana tu kati ya Wizara na Tanesco. Sioni mahali popote ambapo wahusika wamejielekeza kutatua tatizo la MGAO WA UMEME ambao umedumu toka miaka ya 90.

Mkuu wangu JokaKuu,
Uyasemayo yanaweza kuwa ya kweli lakini ili mradi ni yeye aliyewahiwa kuvikwa shada la miba; basi mie kwa sasa nitakayekazana kumtupia mawe ni huyu huyu kwanza hadi pale nitakaposikia tuhuma zisizo shaka dhidi ya hao wenzake!!

Kuhusu hilo la Katibu Mkuu, hata nami nimelisikia. Hata hivyo, utetezi uliotolewa na Katibu Mkuu huyo nauunga mkono hadi pale itakapothibitishwa vinginevyo!! Kimsingi, inasemekana kwamba; Vigogo wa TANESCO walitoa tenda ya uuzaji mafuta kwa kampuni nyingine kabisa. Lakini kilichokuwa kinafanywa na kampuni hiyo ya walaji wa TANESCO ni kwamba; walikuwa wananunua mafuta mazito toka kampuni ya Puma Energy kisha nao ndo wanakuja kuiuzia TANESCO kwa bei ya juu! Hiyo kampuni ya Puma Energy ilishindwa kwenye mchakato wa kumpata supplier wa hayo mafuta! Sasa alichokifanya Maswi(Katibu Mkuu), ni kuamua kununua mafuta moja kwa moja toka kwa hao Kampuni ya Puma Energy....hivyo basi; kosa la kwanza hapa ambalo labda tunaweza kuliona kwa Maswi; ni kuipa tenda ya ku-supply mafuta kampuni ambayo ilishindwa! Lakini uzuri uliopo ni kwamba; hao Puma Energy hivi sasa wanauza mafuta kwa bei ya chini kuliko ile iliyokuwa inatolewa na kampuni zilizoteuliwa na TANESCO....wanauza bei ya chini kwavile kampuni za akina Mhando zilikuwa zina-act kama middle men wa Puma Energy katika ku-supply mafuta kwa TANESCO! So, hata kama Maswi amefinyanga sheria; kwangu naona ni bora mara 1000 kufinyanga sheria kwa ajili ya maslahi ya taifa(ya wengi) kuliko kufuata sheria in favor of watu wachache! Ni hadi pale Mhando na watu wake watakavyothibitisha kwamba Maswi ana maslahi binafsi kutokana na hatua yake ya kuipa tenda Puma inayoiuzia TANESCO mafuta kwa bei ndogo; vinginevyo bado kwangu nitaona kitendo alichofanya kina maslahi kwa taifa!
 
Kiranga ktk sheria hakuna kosa la Conflic of interest, linaweza kuwa tatizo lakini sio kosa. Viongozi wote wanatumia nyadhifa zao kuendesha biashara kupitia watoto, wake, ndugu namarafiki maadam hawaibi..
Hii ndio Bongo yetu karibu sana!.

Angalia "The Public Procurement Act, 2004" 37 (6) halafu utuambie kama Mhando ali declare conflict of interest according to this law.

Sheria imesema wazi, sielewi unaposema "hakuna kosa la conflict of interest" una maana gani.
 
Wakati Wizara ya Nishati na Madini ikitarajiwa kuwasilisha bajeti yake kwa mwaka wa Fedha 2012/2013, mvutano miongoni mwa wabunge umezidi kutanuka kiasi cha kuhatarisha mjadala wa bajeti ya wizara hiyo...........................................“Mke wangu aliacha kazi, lakini tulikuwa na kampuni hiyo ya stationery Kariakoo na kwa sababu biashara haikuwa nzuri kutokana na uwezo mdogo wa kifedha, tuliuza kampuni hiyo mwaka jana.

Mke wangu aliajiriwa tu katika kampuni hiyo baada ya kununuliwa ili waweze kutumia uzoefu wake katika kuiendesha.

“Sasa kwa nafasi ya mke wangu, yeye ni Mtendaji wa hiyo kampuni lakini shughuli zote za kutafuta shughuli zote za kutafuta zabuni zinafanywa na wakurugenzi wa kampuni hiyo, si mke wangu.

“Kwahiyo, walipoomba kazi TANESCO hatua zote zilifanyika kwa mujibu wa taratibu, kanuni na sharia na kampuni hiyo ilishandanishwa na kampuni nyingine na hatimaye ikashinda,” alisema Mhando.

Mbona hajajibu lolote kuhusu majina ya wanaye kuhusishwa na hiyo kampuni ya mkewe???? Sintofahamu kwa kwenda mbele!!!!
 
Angalia "The Public Procurement Act, 2004" 37 (6) halafu utuambie kama Mhando ali declare conflict of interest according to this law.

Sheria imesema wazi, sielewi unaposema "hakuna kosa la conflict of interest" una maana gani.
Kwangu haifunguki sijui kwa nini?..Kwani inasemaje hiyo 37 (6)
 
Kiranga ktk sheria hakuna kosa la Conflic of interest, linaweza kuwa tatizo lakini sio kosa. Viongozi wote wanatumia nyadhifa zao kuendesha biashara kupitia watoto, wake, ndugu namarafiki maadam hawaibi..
Hii ndio Bongo yetu karibu sana!.

Mkuu Mkandara,
Naona umewaka sana hili Mhando lina tofauti gani na mwenyekiti Mbowe alipojipa tenda ya zaidi mil.300?

Chama
Gongo la mboto DSM
 
Lakini mkuu wangu tuseme ukweli Conflict of interest haina busara wala kutokuwa na busara. Hiatakiwi kumpa mnmtu nafasi ya kufanya madudu haya na ndio maana ya kuwepo miiko na maadili ya Uongozi sio kuwa na tume ya maadili.. Sisi Watanzania tunafanya kila kitu kinyume cha busara halafu tunaitafuta busara kweli hiyo
busara itapatikana wapi?

1. Umesoma utetezi wake kaka?????
2. Umeona composition ya directors wa hiyo santa director's family and supplies????
3. Umeona muajiri wa mke wa director na rationale ya ajira??????

"........Sisi Watanzania tunafanya kila kitu kinyume cha busara halafu tunaitafuta busara kweli hiyo
busara itapatikana wapi?..........."
(Mkandara; 2012)
 
Status
Not open for further replies.
8 Reactions
Reply
Back
Top Bottom