Chaimaharage
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 211
- 78
Kuna taarifa kutoka vyanzo vyetu vilivyo Wizara ya Maliasili na Utalii kuwa ile stock ya meno ya tembo ambayo serikali ilikataliwa kuiuza na shirikisho linalo simamia wanyama walio katika hatari ya kutoweka Duniani(CITES) imeanza kutoweka kinyemela.
Kilichofanyika awali ni kwamba watumishi wote walipewa amri ya kutokuwa ofisini ifikapo saa moja jioni ambapo ni mwisho wa kuonekana mazingira yale. Kumbuka kuwa kuna wengine ambao wanakuwa wana kazi za kiofisi ambapo huweza kukaa hata saa 2 usiku ili kuweza kuzimaliza kwa wakati.
Lakini cha ajabu baadhi ya viongozi hasa wa Idara ya wanyamapori wamekuwa wakionekana maeneo ya ofisi hata baada ya saa 2 usiku tofauti na amri waliyowekewa watumishi wa ngazi za chini inayo onekana kuwalenga zaidi wao.
Sasa mchezo unaofanywa ni kwamba linaingia lori usiku na kuondoka na mzigo. Mtandao wenyewe unaohusika ni mkubwa na siyo kwa viongozi wa Idara hiyo peke yao. Zimefungwa hadi camera kwenye ma-godown yenye meno hayo ili hata kiasi cha mzigo unaoondoshwa kionekane ili katika mgao kusiwepo kuthulumiana. sababu mtu anaweza kusema tumetoa contena moja kumbe ni mawili.
Kwa kawaida meno ya tembo yanapokamatwa iwe porini kutoka kwa majangiri au kwingineko huwa yana pigwa muhuri maalumu kama utambulisho ili yakitoweka ijulikane. Mihuri yenyewe hupigwa upande wa mwisho wa jino na juu. Na ndivyo askari wote wa wanyamapori wanavyoelekezwa kufanya. Sasa jiulize kwanini hawa ruhusiwi kupiga mihuri hiyo sehemu za katikati ya meno? Hebu ona sababu yenyewe;
Wanachofanya hawa jamaa wana kata sehemu ya juu ya meno yenye muhuri na ya chini pia. Kwahiyo sehemu yote ya katikati inabaki haina alama yoyote kiasi hata yakikamatwa mbele ya safari isijulikane kuwa yametokea pale kwenye yale maghala.
Hivyo mwisho wa siku mzigo wote utakwisha na hatujui wa kumkamata ni nani.
Kilichofanyika awali ni kwamba watumishi wote walipewa amri ya kutokuwa ofisini ifikapo saa moja jioni ambapo ni mwisho wa kuonekana mazingira yale. Kumbuka kuwa kuna wengine ambao wanakuwa wana kazi za kiofisi ambapo huweza kukaa hata saa 2 usiku ili kuweza kuzimaliza kwa wakati.
Lakini cha ajabu baadhi ya viongozi hasa wa Idara ya wanyamapori wamekuwa wakionekana maeneo ya ofisi hata baada ya saa 2 usiku tofauti na amri waliyowekewa watumishi wa ngazi za chini inayo onekana kuwalenga zaidi wao.
Sasa mchezo unaofanywa ni kwamba linaingia lori usiku na kuondoka na mzigo. Mtandao wenyewe unaohusika ni mkubwa na siyo kwa viongozi wa Idara hiyo peke yao. Zimefungwa hadi camera kwenye ma-godown yenye meno hayo ili hata kiasi cha mzigo unaoondoshwa kionekane ili katika mgao kusiwepo kuthulumiana. sababu mtu anaweza kusema tumetoa contena moja kumbe ni mawili.
Kwa kawaida meno ya tembo yanapokamatwa iwe porini kutoka kwa majangiri au kwingineko huwa yana pigwa muhuri maalumu kama utambulisho ili yakitoweka ijulikane. Mihuri yenyewe hupigwa upande wa mwisho wa jino na juu. Na ndivyo askari wote wa wanyamapori wanavyoelekezwa kufanya. Sasa jiulize kwanini hawa ruhusiwi kupiga mihuri hiyo sehemu za katikati ya meno? Hebu ona sababu yenyewe;
Wanachofanya hawa jamaa wana kata sehemu ya juu ya meno yenye muhuri na ya chini pia. Kwahiyo sehemu yote ya katikati inabaki haina alama yoyote kiasi hata yakikamatwa mbele ya safari isijulikane kuwa yametokea pale kwenye yale maghala.
Hivyo mwisho wa siku mzigo wote utakwisha na hatujui wa kumkamata ni nani.