Madiwani wapendekeza kuigawa Mbeya

Madiwani wapendekeza kuigawa Mbeya

mkuu wakati mwingine me natamani nisiwe mtanzania tena! Yani bila matumaini 2015 ningezamia hata Zambia hawana upuuzi aina hii!

ha ha ha ha...na bahati nzuri ule mpaka wala hata hauna maana. ukitaka kujua we nenda tu pale kwenye soko la Blaki Tunduma kama wanavyopaita wenyewe; sijui hata kama bado panaitwa vile maana nilienda 1989 sijarudi tena. walikuwa wanapanga vijiwe hapo ardhini ndo mpaka eti. kule wanauza mandazi, uku mandazi. mandazi ya kule Kwacha, mandazi ya uku shilingi. A very funny economy. ukinyang'anya mfuko wa sukari upande wa mashariki Tanzania unaruka kijiwe unahamia upande wa pili. tayari upo zambia. hakuna kukamatwa mpaka interpol ije!

Raha ni kwamba Zambia kuna wanyiha 300,000 tanzania wanyiha 300,000. kwa hiyo ukiona umechoka sana we ruka tu kijiwe. utakuta watanzania wenzio kibao kule.
 
Hivi toka awamu ya nne iingie madarakani imeongeza mikoa mingap?
je,katika kuongeza hiyo mikoa ndo kuna unafuu wa maisha
 
Mpaka 2015 nchi itakua haisomeki.....
hivi Tanzania inamikoa mingapi kwa sasa wajameni?
 
kama nia ni kusogeza huduma kwa jamii wakubali sera ya majimbo,na mbona kuna mikoa mikubwa mfano Tabora mbona haigawanywi?kama vipi wafute mipaka ya mikoa nchi nzima then waigawe upya...
 
ha ha ha ha...na bahati nzuri ule mpaka wala hata hauna maana. ukitaka kujua we nenda tu pale kwenye soko la Blaki Tunduma kama wanavyopaita wenyewe; sijui hata kama bado panaitwa vile maana nilienda 1989 sijarudi tena. walikuwa wanapanga vijiwe hapo ardhini ndo mpaka eti. kule wanauza mandazi, uku mandazi. mandazi ya kule Kwacha, mandazi ya uku shilingi. A very funny economy. ukinyang'anya mfuko wa sukari upande wa mashariki Tanzania unaruka kijiwe unahamia upande wa pili. tayari upo zambia. hakuna kukamatwa mpaka interpol ije!

Raha ni kwamba Zambia kuna wanyiha 300,000 tanzania wanyiha 300,000. kwa hiyo ukiona umechoka sana we ruka tu kijiwe. utakuta watanzania wenzio kibao kule.

hahahaaa! Mkuu Highlander umenichekesha me naishi sana hapa Tunduma lakini mara nyingi nashinda ng'ambo (nakonde) au Mbala (mbele ya nakonde) kuna Wazambia wanyakyusa kibao tunapiga sana story za siasa.

Kiukweli wao hawana hizi mambo za kipuuzipuuzi kama hizi, nainjoi sana kushinda kule ninapokua mapumziko!
 
Last edited by a moderator:
HABARI

Na Godfrey Kahango, Mbarali. (email the author)

Posted Ijumaa,Mei24 2013 saa 21:56 PM

KWA UFUPI

  • Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali, mkoani Mbeya, wametoa mapendekezo yao juu ya mchakato wa kuugawa Mkoa wa Mbeya, ili kupata mikoa miwili kwa lengo la kusogeza huduma kwa wananchi.




Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali, mkoani Mbeya, wametoa mapendekezo yao juu ya mchakato wa kuugawa Mkoa wa Mbeya, ili kupata mikoa miwili kwa lengo la kusogeza huduma kwa wananchi.

Mchakato huo unakuja baada Serikali ya Mkoa wa Mbeya, kumwomba Rais Jakaya Kikwete kuugawa mkoa huo, ili kutoa unafuu kwa watendaji wa Serikali katika kuwahudumia wananchi.

Habari zilisema tayari Rais Kikwete ameridhia maombi hayo na kuagiza kufanyika kwa mchakato huo.

Kw upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro, amewataka madiwani wa hamashauri zote kuketi na kuanza mchakato wa mapendekezo kuhusu namna ya kuugawa mkoa huo.

Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali walitoa mapendekezo yao juzi katika kikao chao.

Akisoma taarifa ya mapendekezo hayo katibu wa baraza hilo, Brown Mwakibete, alisema timu

ya wataalamu iliketi na kutafakari kwa kina namna ya kuugawa mkoa huo kwa kuzingatia maagizo ya mkuu wa mkoa.

Diwani Mwakibete, alisema madiwani wa halmashauri hyo wamependekeza jina la mkoa mpya liwe Rungwe ukiwa na Wilaya za Kyela, Rungwe,

Ileje na Mbozi na makao makuu ya yawe Tukuyu.

Alisema pia wametaka jina la mkoa wa zamani libaki kuwa Mbeya ukiwa na Wilaya za Momba, Chunya, Mbeya na Mbarali na Makao makuu yakiwa Mbeya.

Alisema kamati hiyo haikuona haja yaa kuanzisha wilaya mpya kutokana na sababu za kijiografia.

Naunga mkono hoja kasoro hapo kwenye red nafikiri makao makuu mkoa huu mpya yangekuwa katikati ambapo ni UMALILA na pengine jina lake lingechukua sura ya wilaya zinazohusika ktk kuunda mkoa huo. pia naona wilaya ya Momba kuiacha kwa mkoa wa mbeya itapelekea utawala wake kuwa mgumu sana kwani italazimika mkuu wa mkoa mbeya kupita mkoa mwwingine na ndipo aifikie wilaya yake ya momba.
 
Dah hii kali, ko wilaya ya BUSOKELO itakuwa katika mkoa upi katika hayo mapendekezo yao.walikula kitu cha MWAKALELI hao.

Hapa kuna njama za kuvuruga mpango wa Mwandosya wa kupeleka wilaya yake ya Busokelo mkoa wa Njombe kwani iko jirani na Makete!!! Acheni ujinga huo wa kuwaongezea wananchi wenu mizigo ya kodi kwa manufaa yenu binafsi kwani uwingi wa mikoa na wilaya sio kigezo cha kuleta maendeleo kama hakuna mipango makini na dhabiti!!
 
Hakuna kuwa na mkoa kama Pwani ndani ya Dar. Hakuna kiungo cha Rungwe na Mbozi kupitia Ileje lazma utokee Mbeya. Labda makao makuu yawe katka Wilaya ya Ileje na kuchukua baadhi kata za Mbeya Vijijini
​Madiwani wetu wameacha kujadili maendeleo wanajadili kuongeza matatizo!
 
Naunga mkono hoja kasoro hapo kwenye red nafikiri makao makuu mkoa huu mpya yangekuwa katikati ambapo ni UMALILA na pengine jina lake lingechukua sura ya wilaya zinazohusika ktk kuunda mkoa huo. pia naona wilaya ya Momba kuiacha kwa mkoa wa mbeya itapelekea utawala wake kuwa mgumu sana kwani italazimika mkuu wa mkoa mbeya kupita mkoa mwwingine na ndipo aifikie wilaya yake ya momba.

siungi mkono hoja! Hata hivyo UMALILA ni sehemu ya Mbeya vijijini ambayo inapendekezwa kubaki Mbeya!
 
hahahaaa! Mkuu Highlander umenichekesha me naishi sana hapa Tunduma lakini mara nyingi nashinda ng'ambo (nakonde) au Mbala (mbele ya nakonde) kuna Wazambia wanyakyusa kibao tunapiga sana story za siasa.

Kiukweli wao hawana hizi mambo za kipuuzipuuzi kama hizi, nainjoi sana kushinda kule ninapokua mapumziko!

Ni kweli vilevile wanyakyusa wapo wengi sana kule; wanyamwanga ndo kabsaaa; lugha ya kibemba na kinyamwanga vina maneno mengi yanaingiliana ni rahisi sana ku-assimilate.... ule mpaka wala hata hauna maana.
 
siungi mkono hoja! Hata hivyo UMALILA ni sehemu ya Mbeya vijijini ambayo inapendekezwa kubaki Mbeya!

Ni kweli lakini ktk proposal yao mbeya vijini haipo mkuu!! na pili kama ni swala la wapi makao makuu yawe haiwezi kuwa tukuyu kwani ni pembezoni kwa jiografia ya wilaya zinazounda mkoa mpya, chukulia Mbozi kwenda tukuyu?? ni heri basi mbarali waende tukuyu na mbozi ibaki kama zamani!
 
Ni kweli lakini ktk proposal yao mbeya vijini haipo mkuu!! na pili kama ni swala la wapi makao makuu yawe haiwezi kuwa tukuyu kwani ni pembezoni kwa jiografia ya wilaya zinazounda mkoa mpya, chukulia Mbozi kwenda tukuyu?? ni heri basi mbarali waende tukuyu na mbozi ibaki kama zamani!

Mkuu Mbugi ee, unajua ukisema hivyo ni kama unakubaliana na dhana ya kuongeza mkoa. Wazo zima ni upuuzi wa kuongeza gharama za uendeshaji wa serikali. Halina maana kabisa.

Hapa kinachotafutwa ni upuuzi wa kuongeza bajeti kwa ajira mpya ya Mkuu wa Mkoa mpya, mashangingi mengine FFU kulinda mkuu wa mkoa mpya na gharama nyingine lukuki ambazo zinahusiana na uendeshaji wa serikali ya Mkoa. Wazo hilo ni economically unreasonable kabisa. Mi hata naliona kama jitihada ya kuwagawa watu wa Mbeya.
 
Ni bora kuongeza watumishi wawe wengi na kuiboresha miundo mbinu kuliko kuugawa mkoa kuondokana na gharama zisizo za lazma
 
serikali ya CCM inakosea sana, kugawa mkoa si haki ya madiwani pekee ni wananchi wote. tunatakiwe tupewe nafasi ya kura ya maoni kama tunataka au laa. Wanambeya tunatakiwa tupinge kugawanywa. Sisi sio mbulula kama wanavyofikiria wao.
 
Mimi ni mwana mbeya naomba tufahamu hathali za ugawanywaji wa mikoa mwisho wa siku ni kuleta vita za kikabila huo ni mtazamo wa tofauti kimsingi watu wawajibike na si kua na visingizio mkoa mkubwa sijuh nini ni visingizio vya wapenda madaraka tu mbeya tusipojiangalia mh sijuh ila hakuna haja ya kugawa mkoa je mipaka wanajua au ndio usumbufu kwa vizazi vijavyo?
 
Mkuu NDOMYANA watumishi wanatumia halmashauri ya wilaya ya BUSOKELO,

Naomba tofauti ya halmashauri na wilaya mkuu.
 
Mkuu mi sio mtaalamu sana ila katika kufuatilia nliambiwa busokelo sio wilaya ila walichokifanya ni kuigawa tukuyu kua halmashauti mbili ambayo kati ya hizo busokelo nu halmashauri inayojitegemea na rungwe nayo ni halmashauri,. Ila uneza uliza zaidi ukaelekezwa na wataalam
 
Back
Top Bottom