Madiwani wapendekeza kuigawa Mbeya

Madiwani wapendekeza kuigawa Mbeya

Pole sana ndugu yangu, Ishu ni U - DC, RC, RPC, RCO, n.k Kwani wajomba wamekuwa wengi kuliko idadi iliyopo. Kulilia uongozi pabaya usiombe, Wilayani niliko kuna Kata imegawanywa kutoka vijiji 3 hadi sita. Kila kijiji kina chini ya kaya 300 na eneo la kijiji upana haufiki hata 500m huku urefu ukiwa chini ya 1km. Kisa hiyo kata Imeshikwa na CUF, wanajaribu kugawa wapate walau kijiji kimoja.

Cha kusikitisha kuna watu wanashabikia mikoa kugawanywa bila kuangalia gharama mpya zitakazoongezeka kuendesha serikali.
Watanzania tunapenda kushupalia mambo yasiyo na tija.
 
Kuna kitu kinaitwa Central Government; makao makuu ya uongozi kitaifa. Kila mikoa inaenda pale. watu wanazaliana kila mwaka kiasi kwamba watu milioni tisa waliokuwapo wakati tunapata uhuru wameongezeka hadi kufikia milioni kama 45 hivi kwa sasa.

Kama uingi wa watu ni kigezo cha kugawa mkoa, kuna ubaya gani kugawa Central government kusogeza huduma kwa watu?
 
Nilijua ni rahisi kueleweka!
Nimetoa data za Rwanda na Burundi kuonesha ni kwa jinsi gani Mbeya ilivyo kubwa uko kwengine mbeya ni inchi kama tatu kwa ukubwa wake.
Na pia nimetoa mgawanyiko Toka Southern Highland province mpaka Mbeya Iringa na Rukwa na sasa Katavi kuonesha kuwa kuigawa Mbeya ni inevitable
Ni hayo tuu maana nimeona watu wanachanganya
 
sasa wameshinda kufanya kazi wanadani dawa ni kugawa mikoa tu, huo ndi uroho wa madaraka, sioni haja ya kuugawa mkoa wa mbeya ni kongeza gharama tu

Mi hapa nina miaka zaidi ya 30 lakini sijawahi kwenda kupata huduma kwa mkuu wa mkoa/ofisi yake sasa najaribu kufikilia sijui huyu mkulima wa Mbigili, Vwawa, Itaga, Matema sijui anahitaji kumuona mkuu wa mkoa Tukuyu ili kutatua kero zake!?
 
Hapana mkoa wa morogoro ndio mkoa mkubwa kwa sasa

Ukubwa wa mkoa unapimwa kwa vigezo vipi? ninavyojua mimi kuna idadi ya watu, ukubwa wa eneo, kiwango cha uchumi na ahitaji ya kisiasa kwa wakati huo. Maana Mkuu wa Mkoa lengo lake kuhudumia watu siyo mashamba ya miwa na mkonge, mbuga na misitu kama ilivyo kwa Morogoro.
 
Sikubaliani na kasumba inayo zidi kupamba moto hapa Tanzania.Kugawa gawa mikoo na wilaya ni ukosefu wa fikra chanya.Maendeleo hayapatikani kwa udogo wa eneo husika bari ni kwa kufanya kazi kwa bidii,kama maendeleo yangekuwa ni kutokana na ukubwa wa eneo naamini GAMBIA ingekuwa nchi ya kwanza kimaendeleo.Mbona kugawa nchi kimajimbo imepingwa kwa kudai kuwa tunawagawa watanzania sasa hizi hoja za kugawa mkoa zinatoka wapi?
 
Badala ya kuimarisha huduma za jamii na miundombinu wanaongeza gharama za utawala kwa kuongeza mikoa na wilaya mpya.
 
MADIWANI wa Halmashauriya Wilaya Kyela mkoani Mbeya, wamepitisha azimio la kuugawa Mkoa wa Mbeya nakupendekeza mkoa mpya uitwe Rungwe ambao makao makuu yake yatakuwa Tukuyu.Akiwasilisha pendekezo hilo, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya WilayaKyela, Joseph Njau alisema kufuatia agizo la Rais la kuugawa mkoa ili kuwa namikoa miwili, Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango katika kikao chakekilichofanyika Juni 7, mwaka huu ilikubaliana na suala hilo.

Alisema katika kikao hicho, kamati hiyo ilijaribu kupitia mapendekezoyaliyotolewa na kamati ya wataalamu ambayo ilizingatia vigezo kadhaa kama vilejiografia ya eneo lenyewe, historia ya wilaya husika, shughuli za kiuchumizilizopo.

“Mapendekezo yaliyofikiwa katika baraza hilo, ni kuwa mkoa mpya uitwe Rungwe namakao yake makuu yawe katika mji wa Tukuyu na kuwa mkoa huo mpya utaundwa naWilaya za Kyela, Rungwe na halmashauri ya Busokelo na Ileje sambamba nakuifanya halmashauri ya Busokelo kuwa wilaya kamili,” alisema.

Alisema Mkoa Mbeya, utabaki kuwa na Halmashauri ya Jiji, Halmashauri ya WilayaMbeya, Mbozi, Momba, Mbarali na Wilaya Chunya kwa sababu wilaya hizo zinauhusiano wa kijiografia tofauti na hizi za kusini.

Kwa upande wake, Diwani Kata ya Ngonga, Kileo Kabomonga alisema Mkoa wa Mbeyandio uliokuwa umebakia kuwa na ukubwa kati ya mikoa yote nchini.

Katika kikao hicho, madiwani asilimia 99 walikubali kuwa mkoa uwe Rungwa nabaadhi yao walitaka mkoa uitwe Rungwe, jambo ambalo waliliafiki.

Source: Gazeti la Nipashe 10 Juni 2013
My Take: Hivi kwa nini hawasubiri tuandike Katiba ya Tanganyika? Mfumo huu wa utawala unaweza kubadilika. Haraka yao ni ya nini au ndiyo yale kuwa wao walitakalo ndio linakuwa?

 
Back
Top Bottom