Madiwani wa CHADEMA Dodoma kujiunga na CCM

Madiwani wa CHADEMA Dodoma kujiunga na CCM

Yeyote mwenye nia ifananayo na hiyo ya hao waliorubuniwa mlango uko wazi kuondoka, CDM haitishwi na hilo, bado tutasonga mbele pamoja na mbinu chafu ya ccm na act.
 
chadema yaendelea kuhujumiwa,madiwani wake wake dodoma wanunuliwa kujiunga na ccm.

wakuu hii habari sio tetesi tena ,naiweka hapa jukwaani kama habari kamili.


madiwani wa chadema mkoani dodoma wamedaiwa kunuliwa na ccm ili kuisaliti chadema siku yoyote kuanzia sasa,madiwani hao 3 wanaotajwa kutoka ji,bo la mtera na 1 hajatajwa anatokea jimbo wala kata gani ndani ya mkoa huo, mpango huo unaoendelea kuratibiwa na viongozi wa ccm mkoa dodoma kwakwa ushirikiano wa karibu na viogozi wa act pamoja na aliyekuwa mgombea wa chadema jimbo la mtela mwaka 2010 bwana john lameck robote/lugose,mpango ulioratibiwa kwa mda wa takribani mwezi 1 sasa.


kwa mujibu wa chanzo cha taarifa hii,awali wasaliti hao walikuwa wamepanga wajiuzuru baada ya mfungo wa mwezi mtukufu wa ramadhan,kutokana na mpango huo haramu kugunduliwa na intelegensia ya chadema,wameamua kuuharakisha na sasa hautasubiri mwezi mtukufu uishe na mda wowote kuanzia sasa wataitisha mkutano wa waandishi wa habari,ama watarudisha kadi kwenye mkutano wa hadhara unaoandaliwa na ccm dodoma ,mkutano utakaofanyika mda wowote kuanzia sasa na wamependekeza jk awepo.


kwa mujibu wa chanzo cha taarifa hii kilichopo miongoni mwa waratibu wa mpango huo muovu dhidi ya cdm,kinadokeza vikao vya awali vilifanyikia katika mikoa ya daressalam,morogoro na sasa waratibu wa mpango huo, wapo mkoani dodoma wakiendelea na uratibu huo kikao kilichoandsliwa kufanyikia dodoma hotel,


mpango huu unaratibiwa na samwel malichela (mtoto wa john samwel malichela ambaye anaungwa mkono na viongozi wa ccm jimbo la mtera na dodoma katika jitihada zake za kuhakikisha mbunge wa sasa jimbo la mtera livingstone lusinde”kibajaji”anang’olewa kwenye kiti cha ubunge uchaguzi ujao) kwa kushirikiana na viongozi wa ccm mkoa dodoma kupitia kwa katibu mwenezi wa mkoa, katibu mkuu wa ccm mkoa wa dodoma bwana mgumba ambaye mpaka sasa ndiye alieidhinisha malipo ya kugharamia nauli ya kuwaleta madiwani wa cdm kutoka jimboni mtera,gharama za ukumbi, malazi jumla ya fedha hiyo ni shili laki 4 na elfu 70(470,000)


na miongoni mwa magari yaliyotumiwa katika safari za kuratibu shughuli zote hizo za kutaka kuihujumu cdm ni gari namba t 645 cug aina ya nadia, nyaraka zinaonesha mmliki wa gari hilo ni bwana kyamani elpidius, ambaye hadi sasa haijulikani anajishughulisha na nini, hata hivyo, mtoa taarifa anaendelea kupasha kuwa ccm hadi sasa wameingizwa mkenge kwani mpango uliopo ni kuwa, madiwani hao watajiunga na ccm kwa muda tu, baadae watarudi kujiunga na chama kipya cha act wakati wa uzinduzi wake mwezi wa 9 mwaka huu.

na mwisho wa siku wameahidiwa kupewa pesa yote ambayo wangelipwa kama madiwani kwa kipindi cha kuanzia siku watakayojiudhuru mpaka mwakani,pia katika sakata hili kuna mtu mmoja anatajwa kwa majina ya gwakisa burton anatajwa kuwa nyuma ya mpango huu.

  • :angry:
laana inawaaandama na bado
 
mbona lubote alikuwa jembe saana?du ccm imeamua kutumia sabuni ya roho kununulia watu?sijawahi kuona mahali huo mtindo umefanikiwa duniani.
 
Kwa nini ukimbilie kusema wanunuliwa badala ya kusema kuwa wameshtuka kuwa misukule.
Wewe utajitambua baada ya Kikwete kuondoka madarakani 2015! Utajiunga chama gani ili umshambulie Nyerere kwa amani?
 
CHADEMA YAENDELEA KUHUJUMIWA,MADIWANI WAKE WAKE DODOMA WANUNULIWA KUJIUNGA NA CCM.

...Na mwisho wa siku wameahidiwa kupewa pesa yote ambayo wangelipwa kama madiwani kwa kipindi cha kuanzia siku watakayojiudhuru mpaka mwakani,pia katika sakata hili kuna mtu mmoja anatajwa kwa majina ya Gwakisa Burton anatajwa kuwa nyuma ya mpango huu.

  • :angry:

Huyu Gwakisa aliwahi kuanzisha thread moja humu kuhusu uhusiano wa Zitto, Kikwete, Ridhiwan, Omar Ilyas, Salim A nk. Baada ya thread hiyo alipotea kabisa humu JF hadi wengine tukapata mashaka kwamba huenda thread ile ilimsababishia matatizo. Amekuja kuibuka tena siku za karibuni akiwa mtu aliyeuona mwanga mpya. Si yule Burton huru tuliyemzoea. Mapesa ya Zoka si mchezo.
 
Wewe utajitambua baada ya Kikwete kuondoka madarakani 2015! Utajiunga chama gani ili umshambulie Nyerere kwa amani?

Gwalihenzi hapa mada sio Kikwete, rejea mada husika mkuu. Punguza chuki Kikwete ndo rais kwa sasa.


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Bwana Lameck namjua sana, ila siamini kama kafikia kiwango hicho cha usaliti, japo siwezi kushangazwa maana kuna watu niliowaamini zaidi yake ambao wamefanya usaliti wa kutisha!
 
gealihenzi hapa mada sio Kikwete, rejea mada husika mkuu. Punguza chuki Kikwete ndo rais kwa sasa.


Sent from my iPhone using JamiiForums
Kwanza jaribu kuheshimu majina ya watu kabla hujaanza kumwaga pumba zako, pili, hata kama wewe ni mke wa Ritz hukustahili kumjibia yeye kwani kijembe hicho yeye binafsi amekipokea kwa raha mstarehe!
 
Bora wale bata ukiwa cdm kumbe uko kama almasi kweli vile mbona wccccm hawanunuliwi au cdm njaaa kali sana;;;; kuwa cdm kumbe dili.

Ni chama kipi imara katika historia za siasa kimefanikiwa kwa kuwanunua member wa chama kingine? Hizi ndizo siasa za vyama vipya eti pamoja na chama kikongwe! Ongelea sera na vitendo vyako ili watu wakufuate na siyo kuwanunua! So shame...........
cc Malecela mtafuta kacheo kupitia c.....
 
Wakazi wa Dodoma hawajui chama kingine zaidi ya ccm!!! Acheni kusema Dodoma kuna chadema ili kupata sifa!!!
Chadema itatoa wapi madiwani ndani ya himaya ya ccm???

Kuna uhusiano wowote na maendeleo hafifu ya mkoa huo?
 
ImageUploadedByJamiiForums1405429064.514094.jpg
Hapa angekuwa sio mchaga/mjukuu wa Mtei yuko na Mwamba wa Kaskazini uwiiiii yaaani ungesikia kashanunuliwa...ila ni huyu ndio wenye chadema yao...atokee sisimizi wa-chadema hapa aseme chochote aone kama hatujamfukuza chama
 
Hata wakati wa Mtume Mussa, kuna baadhi ya wana wa Islaeli waliamua kurudi utumwani Misri na kuachana na mpango wa Mwenyezi Mungu wa kuwarudisha kwenye nchi yao ya ahadi Kanani. Sababu kubwa ikiwa ni NJAA na KIU tu. Uvumilivu ukawashinda kabisa.

Mambo haya hayawezi kuwarudisha nyuma watanzania kufikia uhuru wa kweli ifikapo 2015, Ndugu zangu, kwenye msafara kama hii haya mambo lazima yawepo, wacheni wachukue RUPIA wakamtumikie wanayeona anawafaa, sisi tunasonga mbele....
 
mkuu naomba utengue kauli ya uelewa!
-kinacho sumbua ni dodoma viongozi wangu wa chadema naomba mfike vijijini na mijini kwaajili ya kujenga misingi bora ya chama.
-maeneo kama mvumi,nhinhi,mlowa,makang'wa,mpunguzi,mpwayungu,bahi,chigwe na kwingineko.
Nasisitiza makamanda nendeni mkahamasishe zaidi,dodoma imeamka zaidi ya kawaida wanakosa muhamasishaji tu!,
hii ni kweli maana mimi mwenyewe nimejionea.

Usijali tutakuja Kamanda tupo wa ST.JOHNS UNIVERSITY NA UDOM kwa hilo nikutoe hofu hapa ni suala la muda tu but si muda mrefu tulikuwa Mvumi
 
mbona lubote alikuwa jembe saana?du ccm imeamua kutumia sabuni ya roho kununulia watu?sijawahi kuona mahali huo mtindo umefanikiwa duniani.

lubote ni jembe la wapi?
-huyu huyu tuliyesoma nae mpenda sifa na majivuno ya kijinga?
 
Kama kuna hata watu waliomsaliti Bwana Yesu, sembuse Chadema? acha watumikie tamaa ya nafsi zao!
 
Back
Top Bottom