Madiwani Kwa Lowassa Wasusa

Madiwani Kwa Lowassa Wasusa

Fukara

JF-Expert Member
Joined
Dec 28, 2013
Posts
1,624
Reaction score
930
Kata zao zakosa watia nia, Wasema wanasubiri kauli yake, kikao cha kamati ya siasa chaitishwa kwa dharura leo.

Mh.Edward Lowassa.
Kasi ya wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuomba nafasi za udiwani na ubunge katika Jimbo la Monduli, inasuasua na tayari chama hicho kimeitisha kikao cha dharura cha Kamati ya Siasa kitakachokutana leo kukuna vichwa kutafuta ufumbuzi wa hali hiyo.

Katibu wa CCM Wilaya ya Monduli, Elisante Kimaro, alisema jana kuwa kusuasua kwa wanachama kuchukua fomu za kuomba kugombea nafasi hizo kunatokana na kushuka kwa morali ya wanachama baada ya Mbunge wa zamani, Edward Lowassa, aliyekuwa akiwania kuteuliwa na chama chake kugombea urais, kukatwa jina lake.

Alizitaja kata hizo kuwa Engaruka, Engutoto, Esilalei, Lepurko, Loksale, Majengo, Makuyuni, Meserani, Nalalani, Lemooti, Moita, Monduli Juu, Monduli Mjini, Mfereji, Mswakini, Mto wa Mbu, Migungani,


Chanzo:
Nipashe
 
Nipashe wanatumika vibaya...ina maana hao wote matumbo yao yanamtegemea lowasa?
 
Wangemkata kihalali hamna shida ila njia waliotumia.
 
Nipashe wanatumika vibaya...ina maana hao wote matumbo yao yanamtegemea lowasa?

Je inatosha kusema tu Nipashe inatumika au ulipaswa kutuambia ukweli wa kinachotokea huko ka EDO ili tuona jinsi Nipashe inavyo tumika.Mbona mahaba yatakutoa makengeza
 

Attachments

  • 1437126222057.jpg
    1437126222057.jpg
    25.6 KB · Views: 1,797
Kikwete aliwaambia wasiokubaliana na CC wamrudishie kadi. Sasa wao wanangoja nini? Au wanapima homa kwa mkono???
 
walikuwa 38, mbona wengine hatusikii kelele zao huko wanapotoka mikoani....mwizi mkubwa huyo...mwambie aendelee kuchukia umaskini...wanamonduli ni matajiri maana kawatumikia kitambo sana..
Nchi haiongozwi na mafisadi hii...haturudii makosa.
 
Kikwete aliwaambia wasiokubaliana na CC wamrudishie kadi. Sasa wao wanangoja nini? Au wanapima homa kwa mkono???

Tunaondoka na kadi haturudishi HAKUNA mahali sheria inasema kuwa kadi ni mali ya chama
 
Nipashe wanatumika vibaya...ina maana hao wote matumbo yao yanamtegemea lowasa?
Kwako wewe tumbo ni muhimu sana..kweli wagaagaa na pwani ni shida..ndio maana waliiachwa na wauza watumwa
 
Wangemkata kihalali hamna shida ila njia waliotumia.

na wewe naye vipi? kuna mtu anasema amekatwa kiharali hata mwanafunzi akifeli anasema ameonewa sembuse yy uwiiiiiiiii
 
Back
Top Bottom