ZeMarcopolo
Platinum Member
- May 11, 2008
- 14,017
- 7,220
Kama Mbowe vile.
Madikteta wote wanafanana; wawe ni wale ambao ni mtu mmoja mmoja au wawe wa chama kimoja; kufanana kwao kunatabiri vitendo vyao. Hufanana katika mambo makubwa matano:
a. Huamini kuwa wao ndio pekee wenye uwezo wa kutawala (Katika fikra zao hawaamini kama kuna mtu au chama kingine kinachoweza kutawala vizuri kuliko wao). Baadhi yao (kama ni mtu mmoja au chama) hujiaminisha kabisa kuwa ni wateule wa Mungu kutawala nchi zao.
b. Huamini kuwa wanapendwa sana kupita kiasi (hili kuelezea kwanini picha, sanamu, n.k zao huenezwa kila kona ya nchi) Hupenda kuimbiwa nyimbo za kusifiwa na kupeperushiwa maua kila wapitapo kama ishara ya "upendo" huu.
c. Hawako tayari kuamini wanaweza kukataliwa; Mara zote inapotokea mtu anawapinga au kuwakataa hutafutiwa sababu ya kuoneshwa kuwa haiwezekani awakate wao kwani (b) wao wanapendwa sana!
d. Hata siku moja hawajawahi kutengeneza mifumo itakayowaondoa wao wenyewe madarakani. Hivyo, hutumia mbinu zote kufanya mabadiliko ya kimapambo tu ambayo kwa watu wasiofuatilia huweza kuvutiwa kuwa ni mabadiliko. HIvyo aidha hujikuta wanaondoka kwa kukimbia au kwa kukimbizwa na wananchi wao au mataifa ya nje!
e. Wako tayari kufanya jambo lolote kubakia madarakani - msisitizo hapa uko kwenye neno "LOLOTE".
Kutokana na hayo matatu tabia za madikteta wote huweza kutabirika (wawe ni mtu mmoja au chama kimoja). Na ili kuhakikisha hayo matatu madikteta wote duniani (wanaovaa nguo za kiraia na wale wanaovaa nguo za kijeshi)
1. Hutumia vitisho kulazimisha kupendwa na kukubalika - silaha ya dikteta ni vitisho (terror). Wakikukamata watakasumbua sana hadi uogope. Lengo ni kukushawishi uone ni kwanini wao wanastahli kupendwa! Hupenda kujiona kama wazazi wa wananchi - nani atamchukia mzazi wake?
2. Hutengeneza masimulizi ya sifa na kuyalazimisha yaaminiwe hata kama msingi wake ni uongo. Madikteta ni mabingwa wa kuunda (manufacture) uongo. Uwezo wao mkubwa wa kufanya hivi hutokana na ukweli kuwa wao humiliki vyombo vya habari vyenye kufikia watu wengi zaidi (radio, TVs n.k)
3. Inapofikia mahali kuwa upendo wa wananchi unapungua au wanaanza kuwa na mashaka nao madikteta huanza kupoteza watu. Yaani, pole pole watu huanza kukamatwa na kuwekwa "vizuizini" ili wasimpinge sana dikteta.
4. Kisingizio pekee cha madikteta wote (wawe wa mtu mmoja au chama kimoja) kuhalalisha kuwanyanyasa, kuwanyima wananchi uhuru na hata kuwatia watu nguvuni ni "kwa ajili ya nchi". Yaani, hutumia "taifa" kama kisingizio cha wao kuendelea kutawala.
Kwanini?
Kwa sababu madikteta wote wanataka kupendwa na kukubaliwa!
Ole wao wananchi wanaposema "hapana"!!!
Na. M. M. Mwanakijiji (BGM)
Bahati nzuri hapa kwetu tumeepuka udikteta ndio maana Mwalimu alishtuka na mapema kwa kuandika katiba inayoweka mipaka ya Rais asizidi miaka 10!
Tangu 1995 uchaguzi huru na wa haki umeendelea kufanyika nchini!
Vyama vya siasa kuendesha kampeni zao kwa huru ingawa kasoro za hapa na pale zinakuwepo!
Mahakama iliyohuru na inayoendesha kesi bila kuingiliwa na Serikali!
Uhuru wa Magazeti na haki ya kujieleza wa waandashi na Wananchi kwa ujumla!
Ushahidi ni nchi za Kidemokrasia za magharibi kama vile EU na Amerika kutambua utawala wa sheria TZ na hivyo kumimina misaada na kuwa na uhusiano mzuri kinyume na enzi za Utawala wa chama kimoja!
Nadhani TZ kwa kiasi fulani tumejitahidi ukilinganisha na nchi kama Uganda, Zimbabwe, Egypt, Libya, Tunisia, Burundi,nk
hujaza ndugu zao wa damu katika nafasi nyeti kama SHEMEJI kuwa IGP,watoto wao huogopwa sana na wakuu wa idara za serikali na chama mfano ni bora umpe mkulu neno live kuliko mtoto wake maana ataenda kuongeza chumvi na utaambiwa wewe sio raia,wake zao hutumia pesa za umma bila ukaguzi na hutoa ushauri wa kisayansi hata kama si Mwalimu wa sekondari.
Hutumia dini ili kuficha udhaifu wao kiutendaji, hawapendi vijana wawe na elimu sahihi, huteua mvivu atakayejifanya anashida kama za kwenu kuwa mkuu wa utendaji au waziri mkuu kuwazuga wanaichi.
Ushahidi ni nchi za Kidemokrasia za magharibi kama vile EU na Amerika kutambua utawala wa sheria TZ na hivyo kumimina misaada na kuwa na uhusiano mzuri kinyume na enzi za Utawala wa chama kimoja!
Nadhani TZ kwa kiasi fulani tumejitahidi ukilinganisha na nchi kama Uganda, Zimbabwe, Egypt, Libya, Tunisia, Burundi,nk
5... Robert Mugabe wa ZimbabweVyema, na Kweli kabisa. Sasa tuanze kuwaorodhesha madikteta wa dunia hii hapa. Mimi naanza na wachache ninaowafahamu. Wadau tusaidiane kutaja hadi wakamilike:
1) Gbagbo wa Ivory Coast ni Dikteta
2) Hosni Mubarak wa Egypt ni Dikteta
3) Yoweri Museveni wa Uganda ni Dikteta
4) Chama cha Mapinduzi cha Tanzania ni cha Kidikteta
5) ...
Duh!Kilichoandikwa kimeandikwa. Kalamu haimtupi mwandishi wake. Lakini, to be frank, Mzee Mkjj bado hajaenda mbali. Post yake ya kiingereza jana imeeleza juu ya udikteta japo alikuwa anauma na kupuliza. We need original Mwkjj back.
Vyema, na Kweli kabisa. Sasa tuanze kuwaorodhesha madikteta wa dunia hii hapa. Mimi naanza na wachache ninaowafahamu. Wadau tusaidiane kutaja hadi wakamilike:
1) Gbagbo wa Ivory Coast ni Dikteta
2) Hosni Mubarak wa Egypt ni Dikteta
3) Yoweri Museveni wa Uganda ni Dikteta
4) Chama cha Mapinduzi cha Tanzania ni cha Kidikteta
5) ...
Mohamed Shein wa ZnzVyema, na Kweli kabisa. Sasa tuanze kuwaorodhesha madikteta wa dunia hii hapa. Mimi naanza na wachache ninaowafahamu. Wadau tusaidiane kutaja hadi wakamilike:
1) Gbagbo wa Ivory Coast ni Dikteta
2) Hosni Mubarak wa Egypt ni Dikteta
3) Yoweri Museveni wa Uganda ni Dikteta
4) Chama cha Mapinduzi cha Tanzania ni cha Kidikteta
5) ...
Yaani wewe unamwita JK dikteta?Mh alhaji muadhama mufti dr dr dr Kikwete ! Madictator huwa wanapenda tittles ndefu kwenye majina yao ili kuonyesha wanapendwa!