mkuu mbona kama hujui unachokitaka katika mapenzi?
kwani wewe huitaji kupendwa?Golden chance never come twice ,huyo ndo wife material
Mkuu mie nina ushauri mzuuri kabisa... Tega sikio.
Ushauri wangu sio wa namna ya kumwacha kabisaaa... Ila ni wa namna ya kumpenda zaidi.
Huyo binti siyo wa kumwacha hata kidogo na ndio wife material ila nikisoma saikolojia yako ni kuwa wewe kuna namna ambayo umemfanyia labelling based on what you have presented.
Kwanza nahisi ya kuwa baada ya kuambiwa kuwa alishawahi kubakwa basi ndio wewe ukaanza kupoteza nae hamu. (Kama ulivyoonesha kwa kuweka red colur as if ni something terrible)
Pili; unataka kuwa na mwanamke ambae atakuwa ni kama label fulani ya kukupambanua kwenye jamii (unataka mwanamke mzuri sana/mwenye shape kali) wakati huyo anaonekana ni wa kawaida sana.
Tatu;- inawezekana baada ya kukidhi haja zako za mapenzi basi unaona you have everything.
Ushauri wangu;
Nakusihi usimwache huyo binti kwani kila unapopendwa basi nawe penda pia na usiwe na mawazo ya kuondoka.
Nikumegee my personal experience kwenye hili ili kukazia ushauri wangu... Mie mke wangu alipewa ujauzito akiwa form three na jamaa akakana. Hadi nakutana nae sikuwa na nia ya kudumu nae ila kwa kadiri alivokuwa ananijali basi nami nikashauriwa na wakubwa zangu kuwa huyo ndio wife material.
Nilijifunza kumpenda na sasa nampenda kuliko chochote na familia yetu kwa sasa ina furaha sana na pia maendeleo as she cares a lot about me and family as well and now we are happy.
So mi ushauri wangu ni kuwa please please stay with that gal.
If you need further advice do not hesitate to send me a pm.