Madereva wa Malori 'wagoma'

Madereva wa Malori 'wagoma'

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Hali ni tete katika Mizani ya Mailimoja Kibaha,Pwani ambapo madereva wa malori wamefunga barabara. Kufungwa kwa barabara hiyo kwa makusudi kunasababisha adha kubwa kwa magari na abiria wanaosafiri kutoka au kwenda Dar es Salaam kupitia Mizani hiyo ya Kibaha. Madereva wa malori ya kusafirisha mizigo kwenda nchi jirani kama Rwanda,Burundi,Zambia na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Mgomo huo umefuatia kupunguzwa ghafla na bila taarifa kwa uzito unaostahili kupita kiuhalali katika Mizani hiyo. Taarifa toka eneo la tukio ambapo nilikuwepo zinaonesha kuwa Serikali imepunguza uzito kwa mizito inayopimwa hapo. Hatahivyo,madereva wote na matajiri yao hawakuujua uamuzi huo na hivyo kujikuta leo wakionekana kuwa wamezidisha uzito. Hii ni karibu kwa kila lori.

Taarifa zinaonesha kuwa kwa sasa,muda si mrefu, Serikali imetangaza na kuamuru barabara ya Morogoro ifunguliwe haraka iwezekanavyo. Madereva wa malori walioyazima kwa kuziba barabara hawapatikani. Hakuna wakuyaendesha. Wamegomea uamuzi wa ghafla wa Serikali kwa kupunguza uzito unaoruhusiwa kisheria.

Taarifa zinaonesha kuwa kwasasa foleni ya magari iko Ubungo,Dar es Salaam na Ruvu Sekondari,mkoani Pwani. Mamia ya wananchi wanatembea kwa umbali mrefu leo kurejea makwao. Ni adha kuu. Ni hatari. Hali si vutizi. Ni ya kuogofya.

Kwanini mambo haya? Waziri Mwakyembe na Waziri Magufuli mko wapi?

Mzee Tupatupa(safarini kwa pikipiki kurudi Dar)

 
pumbaf wote wanaohusika kwa kuwanyima fursa ya kutumia barabara watu wengine....pumbaf sana
 
Ina maana wizara inayo husika na Miundo mbinu na uchukuzi hai fahamu matumizi ya vyombo vya habari? au waziri wa ile wizara pamoja na naibu wake ni wahuni?
 
:A S-confused1:MMMHHH, HATUHITAJI NGUVU KUKOMESHA OVERLOADING, TUNAHITAJI UTAFITI WA KINA NA MAAMUZI YA BUSARA, KWANI HATA BABA WA TAIFA HAKUTUKIA NGUVU KUUPA UHURU NA KWA WAKATI ULE WATU WALIKUA WAOGA NA YUMKINI ALIONEKANA KUBAKI MWENYEWE LAKINI ALISHINDA KWA HOJA NA BILA YA LAZIMA
 
Sasa wanaoenda moshi jamani watafika saa ngapi
 
Barabara zinajengwa kwa Gharama kubwa, hivyo ni wajibu wetu kwa pamoja tuzilindw.

Hongera serikali kwa uamuzi sahihi wa kupunguza UZITO. Lengo likiwa ni kuzilinda barabara zetu.

Pia nawalaumu kwa kushindwa kuwasiliana na wadau. Mawasiliano ni kitu cha msingi sana.

Ushauri:
Nawashauri kwasasa viwango vibaki vile vile vya mwanzo wakati mnawasiliana na Wadau.

.
 
Kuna umuhimu gan wa kukomalia usafiri wa barabara ili hali tunaweza kuboresha reli yenye kubeba uzito mkubwa na gharama ndogo? Mathalan mizan ya mikese inafanya kaz n moja tu inasababisha foleni kubwa sana na usumbufu usio wa lazima
 
Serikali ijitahidi kufufua reli ya mizigo itapunguza kero kubwa na msongamano wa magari barabarani.
Najua wamiliki wa malori wanaomba usiku na mchana reli ya mizigo isifanye kazi ipasavyo; lakini ni jukumu la serikali kuleta mapinduzi ya kiuchumi kwa kufufua reli
 
Ndo mana mjini leo hakuna foleni kabisa! Kuwe na mpango wa kuwajengea barabara yao huko porini.
 
Magufuli apunguze kujishrbedua na kujifanya anajua kila kitu....
 
Nyambaf. Wameishiwa fedha sasa wameanza kubuni njia haramu za kujipatia fedha. Mafisadi wakubwa!
 
Hali ilikuwa mbaya sana jana, nilikwama picha ya ndege Kibaha kuanzia saa kumi jioni hadi nilipokodisha bodaboda kwa bei kubwa iliyonifikisha jijii saa 4 za usiku.

Serikali ni lazima iachane na mzaha na ifanyie marekebisho makubwa njia za reli ya kati, reli ya Moshi/Arusha na reli ya tazara, pamoja na kununua mabehewa na injini za kutosha kusafirisha mizingo mikubwa na abiria,
 
Hans Pope alishatoa tahadhari mapema sana. Na kuamzia kesho jumatatu transporters wote wanagoma. Hiyo ndo itakuwa kimeo balaa. Magufuli inabidi asiwe anakurupuka ovyo kutoa amri. Ina cost nchi nzima na za jirani.
 
Usagara Mwanza kimenuka hakuna kutoka wala kuingia Mwanza malori yameziba njia yote hi yo kama unaungia Mwanza jitayarishe Kulala Usagara CCM oyee
 
Waacheni wagome wajinga sana. Wanataka kutuharibia barabara. Wabebe uzito mdogo. Na speed lit iwe 60km/hr
 
kuna 5% allowance ya uzito walikua wanaitoa kama favour kwa transporters sasa wameiondoa ndio mana magar mengi yanaonekana kuzidisha ...mfano kweny axels za mbele gar hutakiwa kusoma kg 8000...pamoja na allowance inakua 8400...sasa hivi wametoa hio 400... so kila far inatakiwa kusoma 8000 net
 
Hapo Magufuli kakosea, angewatangazia kwa muda angalau wa siku 21 kuwa ile allowance inaondolewa.
 

Wana Jamii


Mgomo wa wamiliki wa malori ( Tanzania Truck Owners Association) umeanza rasmi leo nchini kote....hii ni kufuatia uamuzi wa ghafla wa Waziri wa Ujenzi Mh. John Pombe Magufulu kufuta weighbridge tolerance allowance ya 5 percent.


Nimetembelea katika depots zifuatazo na hakuna kinachoendelea yaani ni kimya.

1. Oil Com

2. Total

3. Camel

4. PUMA

5. KOBIL

5.WORLD OIL

6.LAKE OIL
 
Back
Top Bottom