beth
JF-Expert Member
- Aug 19, 2012
- 3,877
- 6,326
Madereva wa pikipiki, maarufu kama bodaboda na wale wa bajaji, wameonywa kujiingiza katika maandamamo yasiyo na vibali kutoka polisi katika kipindi cha kampeni za uchaguzi.
Onyo hilo lilitolewa jana na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Wilbroad Mutafungwa, wakati wa kikao cha pamoja na madereva hao kwa lengo la kuwatahadharisha juu ya wanasiasa ambao wanalenga kuwatumia vijana vibaya katika kufanya siasa zao.
Alisema katika kipindi cha hivi karibuni, kumezuka tabia ya baadhi ya wanasiasa kuwarubuni madereva wa vyombo hivyo kwa kuwanunulia mafuta kisha kuwaingiza katika maandamano yasiyo na vibali.
“Hakikisheni hamshiriki katika maandamano ya kisiasa ambayo hayana kibali maalumu kutoka polisi kwani kufanya hivyo ni kinyume cha sheria kwa sababu watawanunulia mafuta lita moja kisha mkajiingiza katika vitendo vya uvunjifu wa sheria,” alisema Mutafungwa.
Aliwataka madereva hao kufanya kazi zao kwa kuzingatia sheria na endapo watatakiwa kusafirisha makada wa vyama kwenda katika mikutano ya siasa, wahakikishe hawajiingizi katika vitendo vya uvunjifu wa amani.
Kwa upande wao, madereva hao waliliomba jeshi hilo kusimamia sheria bila upendeleo hasa wakati huu ambao nchi inaelekea katika uchaguzi mkuu na kubaini wahalifu ambao wanalenga kuichafua kazi yao.
Walisema katika kipindi hiki cha kampeni, baadhi ya watu ambao si waaminifu hujitokeza na kufanya vurugu kwa kutumia pikipiki au bajaji, kitendo ambacho walisema kinachafua taswira ya kazi wanayoifanya.
Onyo hilo lilitolewa jana na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Wilbroad Mutafungwa, wakati wa kikao cha pamoja na madereva hao kwa lengo la kuwatahadharisha juu ya wanasiasa ambao wanalenga kuwatumia vijana vibaya katika kufanya siasa zao.
Alisema katika kipindi cha hivi karibuni, kumezuka tabia ya baadhi ya wanasiasa kuwarubuni madereva wa vyombo hivyo kwa kuwanunulia mafuta kisha kuwaingiza katika maandamano yasiyo na vibali.
“Hakikisheni hamshiriki katika maandamano ya kisiasa ambayo hayana kibali maalumu kutoka polisi kwani kufanya hivyo ni kinyume cha sheria kwa sababu watawanunulia mafuta lita moja kisha mkajiingiza katika vitendo vya uvunjifu wa sheria,” alisema Mutafungwa.
Aliwataka madereva hao kufanya kazi zao kwa kuzingatia sheria na endapo watatakiwa kusafirisha makada wa vyama kwenda katika mikutano ya siasa, wahakikishe hawajiingizi katika vitendo vya uvunjifu wa amani.
Kwa upande wao, madereva hao waliliomba jeshi hilo kusimamia sheria bila upendeleo hasa wakati huu ambao nchi inaelekea katika uchaguzi mkuu na kubaini wahalifu ambao wanalenga kuichafua kazi yao.
Walisema katika kipindi hiki cha kampeni, baadhi ya watu ambao si waaminifu hujitokeza na kufanya vurugu kwa kutumia pikipiki au bajaji, kitendo ambacho walisema kinachafua taswira ya kazi wanayoifanya.