Madeni ya Taifa: Kuna Kitu Very Serious CAG Amekisema!. Hii kitu haiko sawa and it’s not Right. Je, tunakwenda wapi?!

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,498
113,604
Wanabodi,

Hili ni bandiko kuhusu kitu very serious kuhusu mustakabali wa taifa letu na vipaumbele vyetu ambapo CAG Prof. Mussa Asad amekisema!. Kama hii ni kweli, then, this is not right at all, hivyo kama mambo yenyewe ni haya, hala hala huko mbele tusije tukashikana mashati, swali linabaki "Jee Tanzania Tunakwenda Wap?!".

Kwenye ripoti ya CAG kuna madeni ya nchi nchi yetu ya muda mrefu ambayo tunadaiwa na wadai kutoka nchi za nje. Madeni haya ni a very bad liabilities kwa nchi, haswa kwa upande wa landed national properties.

Nchi yetu tumepata fedha, badala ya kwanza ku clear liabilities za madeni yetu hatarishi ya nje ya nchi, sisi tunajikita kununua properties ambayo mwisho wa siku, zitakumbwa na risk ya kuja kakamatwa na wadeni wetu as attachment kushinikiza kulipwa madeni yao.

Hili jambo la madeni hakuna anayelizingatia kwa sasa kwa sababu Tanzania hatuna landed movable property popote inayokamatika as attachment, lakini hii midege tunayoinunua sasa kwa misifa ya kuinunua kwa cash, itakapoanza kakamatwa as attachments kwa madeni yetu, tukashikana mashati na kwanza kumtafuta mchawi, kumbe mchawi wetu anayetuloga ni sisi Watanzania wenyewe!.

Tanzania ni nchi yetu sote na sio mali ya mtu na inaendeshwa kwa msingi mkuu wa katiba kwa mujibu wa sheria, taratibu kanuni, haiwezekani jambo lililopitishwa na Bunge kwa mujibu wa sheria, taratibu na kanuni, halafu lisitekelezwe kama sheria ilivyoelekeza, halafu wakati huo huo kuna jambo jingine ambalo halijajadiliwa na Bunge, halijatengewa budget na serikali, hivyo halijaombewa hiyo budget, ikatengwa, ikawasilishwa Bungeni, ikajadiliwa, ikapitishwa, lakini likaibuka from nowhere jambo jingine kubwa linalohitaji fedha ndefu, ambalo sio la dharura, likajiibukia tuu from nowhere, budget yake haijatengwa popote, haijaombwa popote, lakini kwa vile fedha zimo ndani ya chungu chetu, kwenye hazina yetu, ukapitishwa uamuzi, fedha hizo zichotwe bila idhini ya Bunge, na jambo hilo likatekelezwa na huku tunamtazama mzigo wa madeni chachefu na hatarishi ya muda mrefu na hayajalipwa!. Jee jambo hili jipya limetekelezwa kwa fedha kutoka votes gani, iliyoidhinishwa na nani na kwa mamlaka gani, au sheria ipi?!.

Ninavyofahamu mimi ( I stand to be corrected), serikali hutekeleza majukumu yake yote kupitia bajeti iliyoombwa, kuwasilishwa Bungeni, na iliyoidhinishwa na Bunge kupitia vifungu mbalimbali yaani Votes na Sub Votes. Hizi ni fedha za umma, zinapaswa kutumika kwa mujibu wa sheria, taratibu na kanuni za fedha umma, ambapo bajeti baada ya kupitishwa, hutungiwa sheria, finance bill, na kuidhinishwa na CAG na ndipo huanza kutumika.

Kabla fedha zozote za serikali zilizopitishwa na Bunge haziwezi kutumika kwanza Kabla hazijaidhinishwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali, na hii ndio role ya CAG kama Mdhibiti Mkuu wa Matumizi ya serikali, kudhibiti matumizi ya serikali yaliyoidhinishwa na Bunge, na kisha baada ya matumizi, CAG hurejea kufanya ukaguzi wa matumizi ya fedha hizo kama zilitumika kama zilivyokusudiwa na hii ndio role ya CAG kama Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali. Ripoti ya CAG ndio the most important report kuliko ripoti nyingine yoyote, kila mwaka ripoti inaonyesha urari wa madeni na deni la taifa, sisi badala ya kulipa madeni, tunafanya manunuzi, ukifika muda wa madeni chachefu haya kututokea puani ndipo tutajifunza kuwa dawa ya deni ni kulipa.

Naomba umsikilize kwa makini hapa, CAG, Prof. Mussa Assad kuna kitu very very serious anakizungumza kupitia Habari ya Channel Ten.

CAG Prof. Assad amesema, huku nchi ikiwa na mzigo mkubwa wa madeni, kuna wizara mpaka sasa the final quoter of the budget year, zimeishapewa mgao wa asilimia 16% tuu ya bajeti zake zilizoidhinishwa na Bunge, kwa hoja kuwa serikali haina fedha, lakini at the same time, ndani ya serikali hiyo hiyo, kuna wizara nyingine zimefanya matumizi ya ziada ya zaidi ya asilimia 230% outside the budget!.

Hii maana yake kuna maeneo serikali imefanya matumizi makubwa ambayo hayakuwepo kwenye budget ya serikali, hayakuletwa bungeni, hayakujadiliwa wala kuidhinishwa na Bunge na hivyo hayana Vote wala hayakudhibitiwa na CAG, lakini serikali ikafanya matumizi hayo kinyume cha sheria, taratibu na kanuni za matumizi ya fedha za serikali.

Maswali ni
1. Kama serikali imeshindwa kulipa madeni, imeshindwa kulipa OC za baadhi ya taasisi kwa hoja kuwa haina fedha, jee hizo fedha zilizotumika kufanya hayo matumizi ambayo they were not budgeted for, zimetoka wapi?!. It is as if kulikuwa na pot fulani yenye fedha ambazo zilifanyiwa ring fencing mapema kabla ya budget zikachimbiwa mahali na kufukiwa na sasa ndio zimefukuliwa, zinachotwa, tuelezwe tuu, tutaelewa.

Kwenye hili serikali iwe very open na transparent kama sehemu ya utekelezaji wa Open Government Initiatives, vinginevyo kuna double standards za hali ya juu sana katika kupanga vipaumbele vyetu vya kibajeti, haiwezekani huyu apewe 16% na mwingine 230% na wote ni watoto wa baba mmoja!. Unless kuna wizara ni watoto wa ndani na kuna wengine au ni wanaharamu au watoto wakufikia!.

2. Matumizi yoyote ya serikali lazima yaidhinishwe na Bunge na kuidhinishwa na CAG katika the Principles of Check and Balance and Separation of Powers. Hii maana yake kuna mtu yeye amejifanya ndio serikali akapanga budget, kisha akajifanya Bunge akaipitisha hiyo budget, akajifanya CAG, akaidhinisha hiyo budget na kujifanya PPRA kwa kutotangaza tenda yoyote ya manunuzi makubwa na kumalizia kwa kufanya matumizi na kuitumia fedha za umma bila idhini ya Bunge, na bila kudhibitiwa na CAG, bila kutangazwa Tenda, na bila kuulizwa na yeyote !. How can this be?!. Jee Tanzania tuna Bunge la namna gani ambalo moja ya majukumu yake ni kuisimamia serikali, halafu serikali inayafanya yote haya, na Bunge lipo na limenyamaza?!, ukiliita Bunge kama hili kuwa ni Bunge dhaifu kuwahi kutokea, utakuwa umelionea?.

3. Aliyefanya hayo kuidhinisha matumizi ya serikali bila kibali cha Bunge, yupo, ameulizwa?, na jee katika kufanya matumizi hayo makubwa bila kuidhinishwa na Bunge, ametumia mamlaka ipi na sheria ipi ndani ya katiba yetu? . Naomba niwakumbushe kwa mujibu wa katiba ya JMT ya mwaka 1977, hakuna aliye juu ya katiba wala juu ya sheria, na japo Rais wa JMT ana kinga ya kutokushitakiwa mahakamani kwa kosa lolote linalohusu utekelezaji wa majukumu yake, lakini rais hayuko juu ya katiba wala hayuko juu ya sheria, atatekeleza majukumu yake kwa mujibu wa katiba na sheria, na hata rais akikiuka Katiba ya JMT, anaweza kuondolewa madarakani na Bunge na kushitakiwa!. Hivyo rais pia yuko chini ya Katiba na atatekeleza majukumu yake yote kwa mujibu wa katiba, sheria, taratibu na kanuni. Kama katiba inasema Bunge ndilo litaidhinisha matumizi ya serikali, then matumizi yote ya serikali, ukiondoa matumizi ya dharura kama majanga, lazima yataidhinishwa na Bunge and no one else!.

Ingekuwa ni nchi za wenzetu kamwe wasingekubali hili lifanyike huku na wao wapo tuu na wanaangalia!. Kiukweli kabisa, sijawahi kushuhudia Bunge dhaifu kama hili tulililo nalo sasa, tangu kuanza kwa mfumo wa vyama vingi vya siasa!.

To be honest, nina mashaka sana na Ripoti ya CAG ya mwaka huu itakayotoka, kama ni kweli itaweza kuelezea madudu hayo haswa kwa kuzingatia kabla Ripoti ya CAG haijawasilishwa Bungeni na kuwa public document, lazima kwanza ipitishwe mahali mtu fulani aione, aridhike ndipo iende Bungeni. Kwa vile Ripoti hii itaonyesha haya madudu ya jinsi Bunge linavyokuwa undermined na jinsi CAG anavyokuwa undermined!. Ripoti hiyo ikitoka na hiki kinachozungumzwa hapa kama kitakuwepo, hiki ndicho kitakuwa kipimo halisi cha udhaifu au uimara wa Bunge letu,

Maswali ni Jee Ripoti ya CAG ya mwaka huu, itapitishwa hivyo hivyo ilivyo? ,au itagomewa au itarudishwa na CAG kulazimishwa kuficha madudu haya kwa kuandaa Ripoti nyingine safi isiyo muonyesha huyo anayejifanya serikali, kisha anajigeuza Bunge na kujigeuza CAG kwa kufanya matumizi bila kuidhinishwa na Bunge na CAG, huku nchi ikidaiwa?.

Ningekuwa mimi ndiye GAG, baada ya kufanyiwa madudu kama haya, sijui saa hizi ningekuwa wapi maana zamani angeishaikuta barua yangu mezani kwake kitambo kulinda heshima yangu!.

Ila kama matumizi haya unbudgeted for ni ya fedha zake binafsi kutoka mfukoni mwake, then it's ok, lakini kama ni fedha umma, fedha za serikali, ni fedha za Watanzania, Watanzania wazalendo wa kweli, hatuwezi kuacha fedha zetu zikatumika bila kufuata taratibu za matumizi ya fedha za umma no matter how matumizi hayo ni mazuri kiasi gani, unless ni dharura kama Tetemeko la Bukoba, lakini kwa nchi inayojitapa ni nchi yenye kufuata katiba, sheria na kanuni na kuheshimu the rule of law, lazima ifuate sheria, taratibu na kanuni. Sasa kama hili ni kweli, huu nao sio ufisadi?.

NB. Kama matumizi yenyewe haya ziada yasiyoidhinishwa na Bunge ni yale yaliyotumika kununulia zile Bombardier zetu za ATC na haya yaliyotumika kuhamia Dodoma, then huu ni ufisadi mzuri, ni ufisadi wa kimaendeleo ambao mimi nauunga mkono kama ninavyounga mkono udikiteta ukifanyika kwa nia njema ushauri wangu ni ndege hizo zisiruke nje kabla ya kulipa madeni ya watu, ndege zetu zisije zikashikwa kama attachments

Jumatano Njema.
Paskali
Rejea
Tangazo hili la serikali halimhusu CAG.
Mawaziri Watakaolalamikia OC Ndogo!, Waache Kazi!. Ni Kauli ya Kujenga Nidhamu au Udikiteta Tuu?!.

Prof. Assad amlipua Magufuli kwa ufisadi uuzaji wa nyumba za Serikali
Update
Serikali ya Rais Dk. John Pombe Magufuli imekiri kukabiliwa na ukosefu wa fedha, hali inayoathiri utekelezaji wa shughuli zake za kila siku.

Kauli hiyo imetolewa leo mjini Dodoma na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Dk. Khatibu Kazungu, wakati akijibu hotuba ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Prof. Mussa Juma Assad, kwenye Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi.

“Ukosefu wa fedha haupo kwenu (CAG) tu, upo serikalini kote; nikubaliane na ushauri wa Prof. (Assad), kwamba tunatakiwa kujiongeza kwa kubuni vyanzo vipya vya mapato ya serikali na kusimamia vizuri makusanyo yake,” alisema Kazungu.

Prof. Assad, alisema ofisi yake inakabiliwa na wakati mgumu kiutendaji, kutokana na serikali kuchelewa au kutoipelekea fedha zinazoidhinishwa na Bunge kwenye bajeti hivyo kufanya kazi ya ukaguzi wa fedha kwenye halmashauri kuwa ngumu.

Alitoa mfano wa bajeti ya ofisi hiyo katika fungu la OC kwa Mwaka 2016/17, kwamba ilikuwa Shilingi Bilioni 18 lakini mpaka Agosti mwaka jana kiasi kilichokuwa kimepokewa hakikuzidi Shilingi Bilioni 2.

“Nililazimika kuzungumza na Mheshimiwa mwenyewe (Rais John Magufuli), kwamb bila kupata Shilingi Bilioni 10 wataalamu wasingeenda kufanya ukaguzi, akaahidi kulishughulikia,” alieleza.

Prof. Assad, aliongeza kwamba Mwezi Septemba walipatiwa Shilingi Bilioni 5 na baadaye Oktoba wakapatiwa Shilingi Bilioni 4, ambapo wataalamu walianza ukaguzi kwenye halmashauri mbalimbali mwezi Novemba 2016. CAG ameweka bayana kuwa mpaka Februari mwaka huu baadhi yao walikuwa hawajamaliza kazi hiyo, hali ambayo ni tofauti na kawaida, ambapo Desemba hutakiwa wote wawe wamerejea kutoka kwenye maeneo ya ukaguzi, ili waandae taarifa ambayo huwasilishwa kwenye Bunge la Bajeti.

Prof Assad amesema kuwa mikoa na halmashauri zinazokaguliwa na CAG zimekuwa zikiongezeka; kutoka mikoa 25 hadi 26 na halmashauri 170 hadi 173. Pia bajeti inayowasilishwa na ofisi ya CAG Bungeni imekuwa ikiongezeka lakini kiasi ambacho amekuwa akipitishiwa na kupewa kimekuwa kikishuka kila mwaka.

Prof Assad ameweka bayana kuwa miaka mitatu iliyopita, ofisi yake ilianzisha utaratibu wa kuwaongezea ujuzi wataalamu wake ili waendane na matakwa ya kimataifa, lakini sasa utaratibu huo umekwama kwa ukosefu wa fedha.

“Tumeomba msaada kwa baadhi ya nchi, ikiwemo China, zimekubali kutusaidia kusomesha wataalamu wetu kwa awamu, angalau watano watano lakini ikumbukwe hata kusafirisha mtu mpaka China na kuishi huko kuna gharama, bado serikali imeshindwa kumudu gharama hizo,” alieleza Prof. Assad

Alibainisha kuwa hata watumishi 129 walioajiriwa na ofisi hiyo, hawajapatiwa mafunzo elekezi, hali inayosababisha kufanya kazi bila ufahamu wa hakika wa taratibu za kazi zao.

Miradi ya gesi na mafuta inayoendelea kutekelezwa nchini, pia haiwezi kunufaisha taifa kwa kiwango cha kutosha kutokana na taifa kutokuwa na wataalamu waliobobea katika ukaguzi wa rasilimali hizo.

Prof Assad pia ameiomba Hazina ipeleke fedha kwa wazabuni wanaoidai serikali. Bila kutaja majina ya wazabuni wala kiasi wanachodai, Prof. Assad alisema, “Naomba Hazina mpeleke fedha zinazotakiwa kupelekwa ofisini kwetu, hawa watu walipwe na sitegemei baada ya kutoa kauli hii, nipigiwe simu au nifuatwe tena na wazabuni hawa.”

Kwa mujibu wa maelezo ya Prof. Assad, mmoja kati ya wadai amesema akilipwa ndani ya mwezi huu (Machi) atapokea kiasi anachodai lakini zaidi ya muda huo, ataanza kutoza riba ya asilimia 15 ya deni hilo kwa kila mwezi.

Alisema wameshaandika barua tatu Hazina, kuhusu madai hayo bila kujibiwa; huku fedha zilizoidhinishwa na Bunge mwaka jana kwa ajili ya miradi ya maendeleo ya ofisi hiyo, Sh. Bilioni 8, haijapekwa hata Shilingi moja.
 
Last edited:
Tatizo ni kwamba wabunge wanafikiria wajibu wa serikali kuhudumia wananchi ni favor.

Hizi wizara zilizozidishiwa fedha zichunguzwe kwa matumizi mabaya ya fedha.

CAG nae atusaidie kwa kuresign.
Mbona hukushangaa siku ile pesa ya sherehe ya uhuru ilipoenda kupanua barabara ya Ali Hasan Mwinyi pamoja na malalamiko kuwa taratibu hazikufuatwa? Naomba usitujazie saver kwa jambo ambalo huko nyuma lilitokea na ukalinyamazia. MAYALLA=NJAA.
 
Wanabodi,
Wanabodi, hili ni bandiko kuhusu Kitu Very Serious CAG Prof. Mussa Asad Amekisema!. Kama Hii ni Kweli, This is Not Right At All, Hivyo Kwa Mambo Kama Haya, Jee Tanzania Tunakwenda Wap?!.

Tanzania ni nchi yetu sote na sio mali ya mtu na inaendeshwa kwa misingi ya katiba kwa mujibu wa sheria, taratibu kanuni, haiwezekani jambo lililopitishwa na Bunge kwa mujibu wa sheria, taratibu na kanuni, halafu lisitekelezwe kama sheria ilivyoelekeza, halafu wakati huo huo kuna jambo jingine ambalo halijajadiliwa, halijatengewa budget, hivyo halijaombewa budget, ikawasilishwa bungeni, ikajadiliwa, ikapitishwa, lakini likatekelezwa. Jee limetekelezwa kwa fedha kutoka vote gani, ikiyoidhinishwa na nani?.

Ninavyofahamu mimi serikali hutekeleza majukumu yake yote kupitia bajeti ikiyoidhinishwa na Bunge kupitia vifungu mbalimbali yaani Vote na Sub Vote. Hizi fedha hutungiwa sheria na kupitishwa na Bunge kama sheria ya fedha/budget.

Kabla fedha zozote za serikali zilizopitishwa na Bunge haziwezi kutumika kwanza Kabla hazijaidhinishwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali, na hii ndio role ya CAG kama Mdhibiti Mkuu wa Matumizi ya serikali, kudhibiti matumizi ya serikali yaliyoidhinishwa na Bunge, na kisha baada ya matumizi, CAG hurejea kufanya ukaguzi wa matumizi ya fedha hizo kama zilitumika kama zilivyokusudiwa na hii ndio role ya CAG kama Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali.

Naomba umsikilize kwa makini hapa, CAG, Prof. Mussa Assad kuna kitu very very serious anakizungumza kupitia Habari ya Channel Ten. (Nafuatilia video clip).

Nilichokisikia mimi kwa masikio yangu ni... katika bajeti ya serikali iliyopitishwa na Bunge, kuna baadhi ya taasisi mpaka sasa the final quoter of the the budget year, zimeishapewa mgao wa asilimia 18% tuu ya bajeti zake, kwa hoja kuwa serikali haina fedha, lakini at the same time, kuna wizara nyingine zimefanya matumizi ya ziada ya zaidi ya asilimia 200%!.

Hii maana yake kuna maeneo serikali imefanya matumizi makubwa ambayo hayakuwepo kwenye budget ya serikali, hayakuletwa bungeni, hayakujadiliwa wala kuidhinishwa na Bunge na hivyo hayana Vote wala hayakudhibitiwa na CAG, lakini serikali ikafanya matumizi hayo kinyume cha sheria, taratibu na kanuni.

Maswali ni
1. Kama serikali imeshindwa kulipa OC za baadhi ya taasisi kwa hoja kuwa haina fedha, jee hizo fedha zilizotumika kufanya matumizi ambayo they were not budgeted, zimetoka wapi?!. Kama kulikuwa na pot fulani yenye fedha ambazo ziliwafanyiwa ring fencing mapema zikafukiwa na sasa ndio zimefukuliwa, tuelezwe serikali iwe very transparent katika hili kama sehemu ya utekelezaji wa Open Government Initiatives.

2. Matumizi yoyote ya serikali lazima yaidhinishwe na Bunge na kuidhinishwa na CAG katika the Principles of Check and Balance and Separation of Powers. Hii maana yake kuna mtu yeye amejifanya ndio serikali akapanga budget, kisha akajifanya Bunge akaipitisha hiyo budget, akajifanya CAG, akaidhinisha hiyo budget na kuitumia!. How can this be?.

Ingekuwa ni nchi za wenzetu kamwe wasingekubali hili lifanyike huku na wao wapo tuu na wanaangalia!.

To be honest, nina mashaka sana na Ripoti ya CAG itakayotoka kuelezea madudu hayo haswa kwa kuzingatia kabla Ripoti ya CAG haijawasilishwa Bungeni na kuwa ni public document, lazima kwanza ipitishwe mahali mtu fulani aione, aridhike ndipo iende Bungeni. Kwa vile Ripoti hii itaonyesha haya madudu ya jinsi Bunge linavyokuwa undermined na jinsi CAG anavyokuwa
undermined!. Jee Ripoti hiyo ikapitishwa hivyo hivyo ilivyo? ,au itarudishwa na CAG kulazimishwa kuficha madudu haya kwa kuandaa Ripoti nyingine isiyo muonyesha huyo anayejifanya serikali, kisha anajigeuza Bunge na kujigeuza CAG kwa kufanya matumizi bila kuidhinishwa na Bunge na CAG, ningekuwa mimi GAC, baada ya kufanyiwa haya, sijui ningekuwa wapi maana zamani angeishaikuta barua yangu mezani kwake kitambo kulinda heshima yangu.

Ila kama matumizi haya unbudgeted ni ya fedha zake binafsi kutoka mfukoni mwake, then it's ok, lakini kama ni fedha za serikali, fedha za Watanzania, hatuwezi kuacha fedha zetu zikatumika bila kufuata taratibu za matumizi ya fedha za umma no matter how matumizi hayo ni mazuri kiasi gani, unless ni dharura kama Tetemeko la Bukoba, lakini kwa nchi inayojitapa ni nchi yenye kufuata katiba na kuheshimu the rule of law, lazima ifuate sheria, taratibu na kanuni. Sasa kama hili ni kweli, huu nao sio ufisadi?.

NB. Kama matumizi haya yaliyoidhinishwa na Bunge ni yale yaliyotumika kununulia zile Bombardier za ATC na haya yaliyotumika kuhamia Dodoma, then huu ni ufisadi mzuri, ufisadi wa kimaendeleo ambao mimi naaunga mkono kama ninavyounga mkono udikiteta ukifanyika kwa nia njema.

Jumatano Njema.
Pakali
Rejea
Tangazo hili la serikali halimhusu CAG.
Mawaziri Watakaolalamikia OC Ndogo!, Waache Kazi!. Ni Kauli ya Kujenga Nidhamu au Udikiteta Tuu?!.

Prof. Assad amlipua Magufuli kwa ufisadi uuzaji wa nyumba za Serikali
Hapo Ndio ninapoona umuhimu wa katiba kubadilishwa Ili bunge lifutwe. Maana bunge letu la sasa halina Maana , hata mahakama pia zifutwe badala yake wakuu wa mikoa Ndio wawe majudge wa maeneo husika. Wenyewe wanakwambia wao sio wanasiasa Lkn cha kushangaza kwanini hawakajiunga Na jeshi halafu wakaja kupindua tu nchi na badala yake wakajiunga Na chama cha siasa, wakagombea vyeo vya kisiasa Na wakatoa ahadi za kisiasa (viwanda kila kona) .kama kuendesha nchi kiubabe Ndio maendeleo yatakuja basi Korea kaskazini ingelikuwa tajiri.
 
Back
Top Bottom