Wana jamvi naomba kuleta hoja hapa ili mwisho wa siku niwaelewe hawa watu nijue jinsi ya kushughulika nao
Julai mwaka jana nilimtuma mwenzangu kulipia kodi ya nyumba miezi sita, akafatiliwa na vibaka wakakwapua mkoba wenye hela na simu na vitambulisho mpaka vile vya benki. Wakakimbia lakini kule mbele baada ya kuchukua hela vitu vingine walivitupa. Nilipo kaa na kutafakari nikagundua palikuwa na mahusiano kati ya kibaka na dalali.
Mwezi wa nane mwaka huu ndugu tupo ofisi moja alipelekwa na dalali kulipia kodi ya nyumba, akalipa akapata dharula akasafiri amerudi akakuta dalali karudi kwa mwenye nyumba akachukua ile hela eti jamaa kaahirisha hatakuja tena. Wamepelekana polisi".halipaswi kujadiliwa lipo polisi"
Wiki mbili zilizopita mwingine tena tupo ofisi moja kapelekwa kwenye nyumba sijui ndiyo mikocheni sijui masaki lakini kalipia mwaka mmoja jana anakwenda kuhamia eti katapeliwa " mshike mshike ikaanza " wamepelekana polisi. Sasa wanajamvi nisaidieni hawa watu wakoje!
Julai mwaka jana nilimtuma mwenzangu kulipia kodi ya nyumba miezi sita, akafatiliwa na vibaka wakakwapua mkoba wenye hela na simu na vitambulisho mpaka vile vya benki. Wakakimbia lakini kule mbele baada ya kuchukua hela vitu vingine walivitupa. Nilipo kaa na kutafakari nikagundua palikuwa na mahusiano kati ya kibaka na dalali.
Mwezi wa nane mwaka huu ndugu tupo ofisi moja alipelekwa na dalali kulipia kodi ya nyumba, akalipa akapata dharula akasafiri amerudi akakuta dalali karudi kwa mwenye nyumba akachukua ile hela eti jamaa kaahirisha hatakuja tena. Wamepelekana polisi".halipaswi kujadiliwa lipo polisi"
Wiki mbili zilizopita mwingine tena tupo ofisi moja kapelekwa kwenye nyumba sijui ndiyo mikocheni sijui masaki lakini kalipia mwaka mmoja jana anakwenda kuhamia eti katapeliwa " mshike mshike ikaanza " wamepelekana polisi. Sasa wanajamvi nisaidieni hawa watu wakoje!