Tatizo la ajira na mfumo mbaya sana wa Elimu vimesababisha nchi nyingi za kuwa na watu wasiofaa kwenye nafasi walizonazo katika jamii. Kuanzia viongozi wa siasa , madaktari,walilimu, maaskari, wahasibu, wachungaji,mashakhe n.k.
Kitendo cha Serikali kuongeza mishahara ya madaktari na kuahindwa kuweka Mfumo wa kuwapata madaktari wenye wito halisi badala ya madakatari wanaokimbilia maslahi,sifa baada ya kukosa ajira zinazoendana na wito wao kumeifanya tasnia ya udaktari na manesi kuvamiwa na genge la wahalifu wa kibinadamu kama yalivyo maeneo mengine. Hii ni kwa sababu kila mzazi anamlazimisha mtoto kusomea udaktari kwa sababu ndiyo sekta yenye ajira na rahisi kujiajiri wakati ukweli ni kwamba udaktari na unesi ni sekta inayowafaa watu wapole sana ,wenye kujiheshimu, watulivu, wasio na majivuno, wasiri, wenye utu na upendo wa hali ya juu. Kwa karne hii kuna madaktari na manesi wakorofi kuliko wavuta bhangi wa vijiweni.
Mfumo mbaya wa Elimu unawafanya watu waliopaswa kuwa mabondia na wanakeshi kuwa madaktari na wahudumu kwenye nyumba za ibada.
Kisa tu mtu ana A au B kwenye masomo ya Sayansi. Mtu aliyepaswa kuwa daktari wa wanyama pori anakimbilia ajira ya udakatari wa binadamu.
Mfumo wa Elimu ungekua bora tungewaandaa watu tangu shule ya Msingi kwa kuspecialize kwenye taaluma anayoonekana kuipenda na kuifanya kwa uaminifu na kwa uhakika . Nyota njema huonekana asubuhi.
Kuna wakati Watu walikimbilia sana kwenye Uhasibu na manunuzi sio kwa sanabu wana wito bali kwa sababu palikua na magumashi mengi na mapesa ya kifisadi. Ukaja wakati fulani watu wakakimbilia Kuwa mawakili kwa sababu ya makesi ya mafisadi waliokua wanaishitaki serikali na kushinda kwa kulipwa mabilioni ya fedha.
Serikali ya Tanzania wanadili mfumo wa Elimu na kuweka mitaala inayowaandaa watu tangu wakiwa wadogo.
Sio mtu anamaliza kidato cha sita ndipo anaenda kusoma taaluma maalumu chuo kikuu. Huko chuoni anaanza kuwaza kichongo, mademu , wizi wa mali za umma na kazi ipi yenye madili ya kuhujumu uchumi wa nchi tena wanakua ni mtandao kabisa wa uhalifu wa mali za umma.
Iwekwe sheria kali inayowadhibiti wahuni kuajiriwa serikalini ili kuondokana na tabia ya watu wasiofaa kukimbilia kwenye ajira za umma.
Pia ajira za kujauana serikalini ni tatizo kubwa linalowaweka watu wasiofaa kwenye ofisi za umma