Naungana na wewe mkuu.
Tatizo ni kwamba wengine tumeshapoteza marafiki zetu mbali na hayo Napinga kwa nguvu zote Posho za vikao iwe kwa wabunge, watumishi wa Umma au madaktari. Siwezi kubalisisha msimamo wangu kwa sababu wabunge wanapewa na nitaendela kuupinga hata kama Chadema wote watabadilika na kuunga mkono posho za vikao. Ujinga huu sintouunga mkono hata kidogo. Kubadilisha msimamo kwa wananchi kunaonyesha wazi tulivyo wanafiki hata ktk maswala muhimu tunayoyapinga toka serikali hii.naunga mkono mgomo wenu..chonde chonde msiache kuwapa huduma mama wajawazito,watoto na wagonjwa walio ktk critical condition
all the best
serikali imetuma watu 3 wamekwenda hoteli ya starlight mahali amabpo madaktari wamekodi ukumbi na kuzuia kuwa kesho hakuna madaktari kukutana hapo na ukumbi kwa sasa uko chini ya serikali.......ukumbi ulikuwa umeshalipiwa.....
Hapa ndiyo penyewe sasa. Mbona wabunge walipodai ongezeko la posho ya kukaa hapakutolewa amri? Zaidi tulipewa habari za kukubaliwa madai yao kwa kile kilicho elezwa gharama za maisha zimepanda mjini Dodoma.
MaDr. komaeni na msilegeze kamba. Haki haipigiwi magoti.
BRAVO kwa msimamo.
Nawasilisha.
|
| Pinda alikoroga posho za wabunge na Janet Josiah na Ratifa Baranyikwa Tanzania Daima |
Madaktari na serikali wote ni vimeo. I hate them.
Nimeonja chungu ya jeuri yao unafikiri Mkuchika, Pinda, Kikwete n.k wanatibiwa humu nchini. Wanaoumia ni tabaka la chini kabisa ambalo pengine hakuna hata wa kuwasemea humu zaidi yangu mimi na wewe ambaye umeipenda comment hii.
Wengi tunaoingia JF tunao uwezo wa kwenda HINDU MANDAL, AGHAKAN, REGENCY n.k Lakini hao ambao wataumia kwa migomo ya madaktari hata uhakika wa milo miwili kwa siku hawana.
Hivi unafikiri kama kuna mtu ndugu yake atakufa; kwa hiyo migomo atawachukuliaje hao madaktari?
Ndiyo hapo walalahoi wengi ambao wanahongwa kanga na ubwabwa na hao wanasiasa wajue thamani ya kura zao.Ili itakapofika muda wanasiasa wanadai kupitishwa wawaulizi wamepata kuchukua hatua gani katika kutetea masilahi yao.
Ni muda mzuri kabisa kwa madaktari kugoma nawashauri sasa muda wa kukutana na Pinda umepita.Kuna taasisi tatu tu ndiyo iliyobaki kukutana navyo ilikuweza kujadiliana(Makamu wa Raisi ,Rais mwenyewe au kamati ya Bunge ya masuala ya jamii ili kikao cha Bunge kijacho PM afuliwe U-PM wake immediately at the first seating of the Parliament maana waheshimiwa Wabunge sisi walalahoi tumewapa Rungu la kuwaadabishwa Viongozi wenye Jeuri kama ya Pinda na wengineo
Cousin unajua serikali at times inapenda sana kudharau carrier za wengine wanaona kuwa kufukuza ndio suluhisho, sielewi wanaposema kuwa hawana hela miaka karibia mitano mfululizo Kikwete ametumia mamia ya hela za walipa kodi kwenda WEF (World Economic Forum) na hatujaona faida yoyote zaidi ya kufuja hela na misafara ambayo hizo hela zingefanyia mambo mengine
Jamani naomba niulize,eti ni kweli madaktari wanataka mshahara wao uwe uanaanzia mil 3.5 kwa mtu wa degree??
When the cock stands on the big rock and begins to cock then the darkness disseapears and the sun rises its tantacles to welcome the better hopes,hopes for everyone...madocs naona mko kwenye ncha ya ushindi na umoja wenu ndo ushindi wenu na jukumu lenu kwa sasa ni kupingana na aina yoyote ya lobbying till the sun brings hopes for you
This is your time,do it now!
Mkuu nisikilize vizuri, mwajiri wako anapokuita hata ukiwa kitandani unaamka na kwenda kumwona. Heshima kwanza kwa mwajiri wako hakuna habari za kufanya mgomo halafu unaweka masharti wewe kama umeichukua nchi hostage.Mkuu kama nimewaelewa vizuri hawa madaktari ni kwamba tatizo ni mtindo/efficiency ya mawasilano toka serikalini. Taarifa toka kwa Waziri mkuu zikiwataka madaktari wakutane naye (PM) Jumapili (leo) ziliwafikia jana Jumamasi saa 10 jioni! Na waliochosema viongozi ni kwamba kwa muda huo ingekuwa vigumu kuwapata madaktari hao. Pia wakasema wakati huo hata hata mkutano wa viongozi wa madaktari ulikuwa umeshaisha na watu wameshaingia uraini.
Nadhani Wizara ya Afya ndio yenye tatizo hapa. Kwanza kwa kuvurunda na kutoa kauli za kejeli, kauli ambazo ndizo ziliwapandisha maruhani hawa madaktari, na pili kutomshauri vizuri Waziri mkuu namna ya kutatua huu mtafaruku. Kama wangetumia busara kwa kuunda timu ndogo ili kuratibu mawasiliano kati ya serikali na madaktari na hakika barua ya mualiko wa kukutana na waziri mkuu ingefika kwa wakati. Hawajafanya hivyo na sasa mambo yanazidi kuharibika. Kumbuka hii sumu iko karibu nchi nzima kwa sasa. Hospitali nyingene hawasemi lakini huduma zimezorota kabisa. Nadhani wanaita mgomo baridi.
Wee unaona hizo ni Nyingi? unajua inamgarimu huyo Dr miaka mingapi kupata hiyo taaluma? Au unadhani kutibu Mtu ni sawa na kutengeneza Gari?
Mimi ,tu wa IT Navuta zaidi ya 2M na naona bado haitoshi.
Huyu PM angekuwa na busara angekubali ombi la madaktari kukutana nao kesho, uwaziri mkuu wake usingepungua na labda angejijengea heshima kwenye jamii. Kesho aibu itamshika pale madaktari watakapoendelea na mikutano yao.
Mh Pinda huwa ananifurahisha sana
Huyu Mkuu waziri anapenda sana maigizo