Mtanza Mwenye Nia
Member
- Sep 10, 2013
- 76
- 21
Habari!
Natumai mu wazima! Leo nataka kutumia jukwaa hili kuwakilisha kilio cha wastaafu wa shirika la reli Tanzania (TRC) ambao kwa zaidi ya mwaka sasa wamekuwa wakifatilia mafao yao kwenye mashirika ya hifadhi za jamii bila ya mafanikio, sababu kubwa ikiwa ni kuwa shirika halikuwa likipeleka fedha walizokuwa wanawakata wafanyakazi kwenye mifuko hiyo.
Inasikitisha kwa sababu fedha hizi walikuwa wakiwakata wafanyakazii.. hili ni shirika kubwa na lenye kurudisha kiasi kikubwa hazina kila mwezi, lakini cha kushangaza hawataki kulipa stahiki za hawa wazee waliolitumikia shirika hili kwa uadilifu na uaminifu mkubwa! Hii ni dhambi!
Najua kuna uwezekano mkubwa hoja hii ikamfikia Mh. Rais kupitia hapa... Baba, Mh Magufuli, hawa wazee wamekosa namna ya kukufikishia ujumbe, naomba unisamehe labda hii sio sehemu nzuri kuitumia kufikisha ujumbe, lakini nakuomba uwasaidie wazee hawa!
Ahsante!
Natumai mu wazima! Leo nataka kutumia jukwaa hili kuwakilisha kilio cha wastaafu wa shirika la reli Tanzania (TRC) ambao kwa zaidi ya mwaka sasa wamekuwa wakifatilia mafao yao kwenye mashirika ya hifadhi za jamii bila ya mafanikio, sababu kubwa ikiwa ni kuwa shirika halikuwa likipeleka fedha walizokuwa wanawakata wafanyakazi kwenye mifuko hiyo.
Inasikitisha kwa sababu fedha hizi walikuwa wakiwakata wafanyakazii.. hili ni shirika kubwa na lenye kurudisha kiasi kikubwa hazina kila mwezi, lakini cha kushangaza hawataki kulipa stahiki za hawa wazee waliolitumikia shirika hili kwa uadilifu na uaminifu mkubwa! Hii ni dhambi!
Najua kuna uwezekano mkubwa hoja hii ikamfikia Mh. Rais kupitia hapa... Baba, Mh Magufuli, hawa wazee wamekosa namna ya kukufikishia ujumbe, naomba unisamehe labda hii sio sehemu nzuri kuitumia kufikisha ujumbe, lakini nakuomba uwasaidie wazee hawa!
Ahsante!