Madada Wenzangu wa JF Vipi?

Madada Wenzangu wa JF Vipi?

Basi tu wivu unamsumbua Kurwa. . . siunajua tena watu walivyo. Wakikosa wao basi na wewe ukose, hiyo ndio starehe yao.

Auchi Doto bana ..
Duhh tayari saa saba usiku ..
Halafu guess what tutaonana Jpili basi
Naenda kule mahali kesho
 
Unapotaka mtu abadilike unamtaka kwa vigezo vipi? Umesikia kwamba shuguli zake hazifanyiki? Au basi tu mazoea ya mtu hawezi kufanya jambo moja at once?

Japo sina haja ya kujitetea kwako naomba tu nikupe picha kidogo ya namna nnavyofanya mambo yangu kwasababu mimi ni mmoja wa watu wanaoonekana muda mwingi pale nnapoamua kufanya hivyo.

Muda wa kunywa chai asubuhi naperuzi JF, nikiwa nafanya kazi zangu shuleni nachangia mada katikati kama ambavyo naweza kujibu text, nikiwa kwenye simu mikono inatype, wakati mwingine hata nikiwa njiani/dukani nakuwa online kama ambavyo naweza kujibu text, nikiwa naandika mambo yangu naweza nikawepo JF pia, jioni nikiwa napika ule muda wa kusubiria hiki kiungue, kile kichemke naweza nikaandika kitu JF, nikiwa nimepumzika na tv naweza nikawa online kwa wakati huo huo, nikiwa nasoma/fanya kazi zangu za shule naweza nikawa active JF, nikiwa navuta usingizi naweza nikaingia JF, nikishtuka usiku naweza nikaingia JF kama ambavyo hua naishia kuangalia TV kabla ya kurudi kulala.

So far sioni uwepo wangu wa JF unanipunguzia nini, napika, nakula,naoga,naenda shule na nnafanya kazi zangu, natimiza majukumu yangu mengine ambayo ni binafsi kidogo, nafua, nafanya usafi, nalala, napumzika, naongea na ndugu/marafiki zangu/waliopo karibu naonana nao n.k

Sasa niambie UNATAKA nibadilike kwa faida ya nani?

Lakini wewe huna mume!
 
Michelle Hana mume,anaishi kwa baba yake hadi hapo atakapoondoka hapo kwenda kazini, masomoni, kwa mumewe au kaburini, Michelle anakula na kulala kwa babaye….hapendi ila sasa ndo anashughulikia aondoke kwenye hatua hiyo.


Ndo amemaliza Master's degree yake, anajipanga ajiajiri,atafute kazi au aendelee mbele kusoma PHD….!!


Michelle yuko kijijini hakuna movie za kununua au cinema ameshamaliza zote alizokuja nazo kijijini, huku aliko hakuna shopping mall, marafiki wako Dar na miji mingine, …Michelle akiamka,husali,fanya usafi wa ndani na nje,pika chai,soma e-mail,bandika chakula,then huoga na kula chakula…akimaliza,hujipumzikia kwa nusu saa, hujisomea walau kitabu chake kwenye e-books, then huanza kukaa JF hadi pale usingizi utakapompata. Michelle hushiriki kazi za kijamii pale inapombidi.


Michelle hapendi kukaa idle,kwahiyo huja JF, kujifunza,kushauri,kupeana moyo na wenzie,kushauriwa,kupata kampani na kufurahi….!


Michelle anajielewa,anajua hatua alipo kwenye maisha yake,anajua ndoto zake na mawazo yake ya mbeleni. Kwa msaada wa Mungu aliyeanza kazi njema kwenye maisha yake,na kwa mapenzi yake,kila kitu kitatimia.


Michelle ataondoka JF pale itakapobidi na si vinginevyo. Kama nakukera….Nipotezeee manziiiiiiiiii!!
 
Haya hapo chini
Wababa hao wamezamia kwenye soccer
Kuna ubaya gani kina mama wakiingia
JF ?

Hakuna ubaya. Tena wawezakuta both baba na mama wako JF kwa wakati huo mmoja.
 
Natamani nikulipe kwa topic hii,nitafute nikupunguzie kidogo dada.


cash.jpg
 
Back
Top Bottom