Madada Wenzangu wa JF Vipi?

Mamababu, wengine wako nje ya Tanzania na wakati wewe umelala wao ndio wameamka. Wengine ni watu wa usiku. Wengine kama mimi ni 24/7 highly addicted with JF.

Labda anadhani Tanzania kukiwa usiku basi dunia nzima nayo inakuwa usiku?
 
Unapotaka mtu abadilike unamtaka kwa vigezo vipi? Umesikia kwamba shuguli zake hazifanyiki? Au basi tu mazoea ya mtu hawezi kufanya jambo moja at once?

Japo sina haja ya kujitetea kwako naomba tu nikupe picha kidogo ya namna nnavyofanya mambo yangu kwasababu mimi ni mmoja wa watu wanaoonekana muda mwingi pale nnapoamua kufanya hivyo.

Muda wa kunywa chai asubuhi naperuzi JF, nikiwa nafanya kazi zangu shuleni nachangia mada katikati kama ambavyo naweza kujibu text, nikiwa kwenye simu mikono inatype, wakati mwingine hata nikiwa njiani/dukani nakuwa online kama ambavyo naweza kujibu text, nikiwa naandika mambo yangu naweza nikawepo JF pia, jioni nikiwa napika ule muda wa kusubiria hiki kiungue, kile kichemke naweza nikaandika kitu JF, nikiwa nimepumzika na tv naweza nikawa online kwa wakati huo huo, nikiwa nasoma/fanya kazi zangu za shule naweza nikawa active JF, nikiwa navuta usingizi naweza nikaingia JF, nikishtuka usiku naweza nikaingia JF kama ambavyo hua naishia kuangalia TV kabla ya kurudi kulala.

So far sioni uwepo wangu wa JF unanipunguzia nini, napika, nakula,naoga,naenda shule na nnafanya kazi zangu, natimiza majukumu yangu mengine ambayo ni binafsi kidogo, nafua, nafanya usafi, nalala, napumzika, naongea na ndugu/marafiki zangu/waliopo karibu naonana nao n.k

Sasa niambie UNATAKA nibadilike kwa faida ya nani?

Hii mbona haijajibiwa? Imemshinda?
 
Hujambo?
Nimeona niulize maana we hujaniuliza.

Mie sijambo. Ukitaka kujua afya yangu mie ni mzima hofu na mashaka ni juu yako wewe uliye mbali na upeo wa macho yangu.
 
Wanawake wengi ndoa zetu ni mateso!

Ikitokea sehemu yoyote ya kutusaulisha mateso inabidi tuwemo hivyo hivyo!

Wengine waume zetu huwa wapo nyumba ndogo mpaka saba usiku!
 
  • Thanks
Reactions: EMT
Mh, Usiku? Wa nchi gani labda ungetuhabarisha? We upo TZ au China au USA au wapi jameni maana kote kote tupo na maisha yaenda. Kwa uthiku umenithingidhia, sijawahi.
 
Mie sijambo. Ukitaka kujua afya yangu mie ni mzima hofu na mashaka ni juu yako wewe uliye mbali na upeo wa macho yangu.

Kama hofu na mashaka unayo mbona ukakawia kuuliza? Mi hali yangu sio nzuri, akili inataka JF tu.
 
Back
Top Bottom