Issue ya mitandao ya kijamii inataka kabisa kufanana na habari za bodaboda, Bodaboda zilipoanza kuchukua kasi kuingia Tanzania vijana wengi waliamua kuanza kuendesha hizo pikipiki bila ya hata kuwa na mafunzo ya usalama barabarani, bila ya hata leseni, yaani ilikuwa ni kama kujitoa mhanga. Nakumbuka hata shamba boy wangu alitoweka ghafla na kujongomea huko ingawa nilipokutana naye siku za mbele nilimwambia afanye mafunzo ya kuendesha pikipiki, na pia ya usalama barabarani na atafute leseni, alinisikia lakini hakutimiza ushauri wangu. Yeye kama walivyo wahanga wengine wa bodaboda alipoteza maisha badaye kwa ajali mbaya na trafiki report ilionyesha kuwa makosa yalikuwa ya bodaboda - Ilinihuzunisha sana
Sasa social media nazo kwa kiasi kikubwa zimeingiliwa na jamii ambayo haikutayarishwa na kupata maelekezo ya kufahamu kwa undani matumizi yake, umuhimu wake, taratibu na sheria za mtumiaji kama zilivyokuwa bodaboda na matokeo yake watu wengi sana wamekuwa na wanaendelea kuwa waathirika wa kisaikolojia na hata wengine wamepoteza maisha sababu ya tabia zetu za kiafrika za kugeuza lengo zuri la matumizi yake halali na kugeuza kuwa kama silaha ya kuwakosesha amani watu wengine kama vile kutukana, kueneza picha chafu, kudharau, kuchonganisha, kutoa habari za uwongo, kwa ujumla kuleta mazingira hatarishi kwa wana jamii wengine.
Mtu yeyote akiwa na simu yenye uwezo wa kuwa na facebook, whatsap, Instagram.... basi ameshajiona amehitimu anajisajili na kuanza matumizi ya hizo social media hata terms of application hazisomi, hata kama ni mgonjwa wa akili ama ana matatizo ya kisaikolojia ni kanyaga twende. Hili ni jambo la hatari sana kwa jamii ingawa wengi hawalioni
Kwa wenzetu Ulaya na America social media zinatumika kwaajili ya kuwarahisishia mawasiliano ya kukuza biashara, kama kuna janga ama hatari fulani, kielimu, kufuatilia usalama wa familia zao nk Lengo likiwa ni kumrahisishia mtu katika harakati zake za kimaisha na kumfanya awe na furaha kwa kiasi fulani maishani, kueneza upendo nk
Sasa sijui sisi waafrika tuna laana gani jamani.... Social media zimegeuzwa silaha za kuwaumiza wengine, kuwafanya wengine wasiwe na amani na maisha yao.. zimekuwa ndo dampo za mapicha machafu - Shame on us