kisokolokwinyo20
JF-Expert Member
- Apr 15, 2019
- 472
- 424
- Thread starter
- #41
Aisee hatari sana
Jamani mimi kadri siku zinavyoenda nakosa hamu kabsa na hapo kati, nakuwa sijisikii kabsa tofauti na mwanzo nilivyokuwa, nilikuwa napenda wanawake kupita kiasi lakini siku izi nakuwa kama nawaonea kinyaa fulani.
Labda tu niuseme ukweli, nilikutana na mdada fulani siku za nyuma,tulijuana kwa mda mfupi kidogo nikamuomba papuchi akatiki na tukakubaliana kupima kabla ya tendo, ila hiyo siku gambe likachukja nafasi yake na matokeo tukaenda kugegedana bila kujuana afya.
Kesho yake asubui nikajua wazi kuwa nilichokifanya kipo nje ya ibara, sasa nikamwambia tukapime japo mambo yalishatendeka, holaleee yule mdada akakutwa positive bwana, aisee nimemeza yale mavidonge sijui yanaitwa PEP yani nimeishi kwa shida sana ndani ya siku 30,
Kwa kweli kila Nikitazama mwanamke sipati hisia kabsa,tuweni makini jaman, pia nina jamaa yangu na yeye ni mtu wa totozi sana na mpiga kilaji, alinitembelea majuzi kati ila nikabaini kuwa anameza ARv ,nilishituka kidogo harafu yeye jamaa hana hata wasi wasi, unajua zile dawa mtu akizishika nakuanza kufungu utajua tu hata awe amekupa mgongo, kale kakopo kake kanasauti fulani pamoja na vidonge vyake.