Machozi ni suluhisho la matatizo ya mwanamke?

Machozi ni suluhisho la matatizo ya mwanamke?

Nikiwa na tatizo lolote huwa nalia sana hii inanifanya nipunguze mawazo na kujua suluhu ya tatizo na always nikilia huwa nasamehe na kuendelea na maisha yangu maana sipendi kukaa na dukuduku moyoni
 
Mwanamke kaumbwa na moyo wa huruma, upendo wa dhati na wenye imani. Ukiwa na sifa hizi hata mwanaume utadondosha tu machozi, embu tuangalie zile movie za wafilipino jamani siku moja moja sio mbaya akina baba, sio mpira tu unaishia kupigana timu yako ikifungwa, angalia tamthilia kama zile unamuona mwanaume anadondosha chozi kwa mpenzi wake kutokana na mapenzi ya dhati aliyoyajenga moyoni, tatizo wanaume wakibongo mapenzi kwetu ni mselebende tu, umeanzisha mahusiano leo, kesho umeomba mchezo, huh....? mapenzi sio ngono jamani ni sehemu tu ya mapenzi, ila penzi la dhati ni kujali na hubba ya kweli, halafu hata hiyo sex yenyewe hatujui, ukimchukua mdada unakimbilia kushindilia, mtoto wa watu anapiga kelele anaumia we unasema unampa raha unazidi kushindilia utafkiri kinu unatwanga buni, mapenzi ni romance, mpe mpenzi wako penzi la dhati akikukosa dakika mbili anakuwaza, ukiingia nae chumbani chukua masaa kumpeti peti, viumbe hawa hisia zao zipo mbali, lazima uzisogeze, haya ukiachwa walalamika na posti kubwa unaiandika jf eeh, embu tuwe na imani akina wakaka. Ndo maana hata wale wadini akianza kusali hata kama ni mwanaume utaona anaanza kulia maana kamkaribisha Mungu wake moyoni, sasa sio Mungu tu wajameni, hata watoto zetu tuwapende kutoka moyoni, wake zetu pia, sio mtoto anakusalimia baba shkamoo unamtolea macho makali mtoto hadi akikuona anakukwepa, kisa una stress zako za kazini. Tuwe na mapenzi ya dhati utaona kulia muhimu, chozi ni tulizo la moyo. Nawakilisha
 
ila mi nna principle moja!
silii mbele ya aliyesababisha nilie!
yani uchukue point tatu nakuona?
ni aidha 3-1
au 5-2
au 2-1
point zote tatu sikuuuuuuuuupi!
 
Kulia ni njia yangu ninayotumia kupata relief pale ninapokuwa stressed au depressed. Nitalia weeeeeee....baada ya hapo nakuwa OK na naendelea na shughuli zangu.
 
Aisee hivi hili mnafundishwa wadada au ni nini kwa mfano!!!!??????

Mbona wote vilizi.....
snowhite, Kongosho, 64Bits, miss neddy, Heaven on Earth ni juu ya nini kumwagapo michozi
hahahhahaha mi nguvu yangu ya kunyanyuka nikipigwa cha chembe ni kulia!
nisipolia ntabaki kuwa weak tu
ntado ze miserable
ntachemka mbaya!
ila uzuri ni kwamba mpk nifike point nimelia ujue wamenipa cha mbavu hasa!silii kila kitu!
 
Last edited by a moderator:
hahahhahaha mi nguvu yangu ya kunyanyuka nikipigwa cha chembe ni kulia!
nisipolia ntabaki kuwa weak tu
ntado ze miserable
ntachemka mbaya!
ila uzuri ni kwamba mpk nifike point nimelia ujue wamenipa cha mbavu hasa!silii kila kitu!


Kama na wewe umetamka haya bayana pasi na kupepesa macho basi kazi ipo!!!!
Kwa hiyo ukimkera mwanamama anayekupenda na asilie hapo kuna kitu kinafunguka taratibu au!!!!?????
 
nikiwa na hasira nakuwa na kitu kama donge limenikaba kooni, nakuwa siwezi ongea wala kufanya kitu chochote productive. ila nikilia na machozi yanavyotoka nahsi kama yanayeyusha kile kitu kilichonikaba kooni.
baada ya hapo hata sijuagi usingizi unatokaga wapi ila kinachofata ni kulala na nikiamka nakuwa fresh kabisa.

Uko kama mimi, nikichukia sana lazima nitalia. Iwapo kuna nafasi hata kama ni dakika 5 nisinzie huwa naamka fresh!!
 
Wakati mwingine hutokea unajikuta tu unashindwa kabisa kuyazuia machozi...kuna siku nilikuwa natembea tu njiani na mzigo mziito sana moyoni, nikajikuta wingu zito la machozi linafunika macho yangu ila chozi halishuki, mpita njia tu mmoja akaniuliza, " dada mbona unalia? " nikajikuta natabasamu kuvunga nikamwambia upepo tu unanipuliza machoni...
Machozi ni njia tu yakutua kinachonikaba kwa wakati huo, hata kama sipati suluhu ya jambo ila inapooza sana machungu
 
Ohh!! Kulia ni dawa tosha ya kupunguza hasira au maumivu.
Wanawake wanaongoza kwa kushusha machozi kwasababu ya kuumizwa/kupandwa hasira. Huwa wanaleta maafa ya mali na miili yao, kwani wakati wanalia huweza kupiga au kuharibu chochote kilichopo mbele yao..mfano, simu, vyombo, n.k.

Tuwaombee kwa Mwenyezi Mungu ili hasira zao zisiwe za kupitiliza, kwani binadamu kutendeana makosa ni jambo la kawaida.
 
Ingekuwa mtu akiomba na pesa akiambiwa hakuana analia tu halafu analala akiamka anakuwa ok ingekuwa safi sana!!!!!!
 
Ohh!! Kulia ni dawa tosha ya kupunguza hasira au maumivu.
Wanawake wanaongoza kwa kushusha machozi kwasababu ya kuumizwa/kupandwa hasira. Huwa wanaleta maafa ya mali na miili yao, kwani wakati wanalia huweza kupiga au kuharibu chochote kilichopo mbele yao..mfano, simu, vyombo, n.k.

Tuwaombee kwa Mwenyezi Mungu ili hasira zao zisiwe za kupitiliza, kwani binadamu kutendeana makosa ni jambo la kawaida.

Nawe ukichukia unalia!!!!!?????
Hata mahakamani!!!????
 
Nawe ukichukia unalia!!!!!?????
Hata mahakamani!!!????

Hapana, mimi silii ninapochukia au kupatwa na hasira, ila huwa siachi kuonyesha dalili za kuumia kwa uso kukunja na kuongea kwa ukali.

Mahakamani sio mahali pa kudondosha machozi, kwani kesi ni ya mteja (wateja) na wala sio ya wakili. Kazi ya wakili/mawakili ni kuhakikisha taratibu za kimahakama zinafuatwa na haki inatendeka katika hatua zote za kusikiliza kesi ya jinai au madai.....period.

Likely, machozi ya kuumia/hasira au furaha nitatoa kwenye matukio yafuatayo:-

1. Kufariki kwa ndugu yangu, rafiki mpendwa, jirani mpendwa, n.k

2. Ajali mbaya yenye kukatisha tamaa kwa uhai wa ndugu yangu, rafiki, jirani, n.k

3. Kupanda daraja la maisha, mfano elimu, ndoa, n.k

N.B: Machozi yakitoka ujue umeumia/kuchukizwa au kufurahia kwa kiasi kisichosemeka as it is an automatic event to happen unless uwe unavuta bangi, kubwia unga, una matatizo ya macho, n.k
 
machozi ni sehemu ya maisha yangu hunipa faraja,hunipunguzia maumivu makali ya moyoni,huelezea jinsi nilivyofurahishwa na jambo Fulani,na pi huonyesha ni jinsi gani jambo Fulani linavyonisisimua,kwa hiyo mkuu MziziMkavu dawa ya machozi wala siitaki.
 
Last edited by a moderator:
Kulia hupunguza maumivu. Mimi nikimuona mtu analia na kweli yupo kwenye tatizo namuacha alie mpaka anyamaze mwenyewe, baada ya hapo ndo naweza kuongea nae na kuangalia njia ya kutatua tatizo.

Binafsi mimi ni mwepesi wa kulia na huwa sielewi kwa nini
 
Back
Top Bottom