Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 43,037
- 34,741
NAITWA Salome Katonaga, ni mtoto wa kwanza kuzaliwa katika familia yetu ya watoto watano. Nimeamua kuwasimulia simulizi hii ili mfahamu kwa nini wahenga walisema dunia ni tambara bovu. Nitaeleza machache lakini ya kuhuzunisha sana ambayo nilifanyiwa na watu wenye roho mbaya.
Siku moja nikiwa katika pitapita yangu nilikutana na kijana mmoja ambaye aliniuliza ilipo Hoteli ya Wapiwapi mjini Masasi.
Nilikuwa naifahamu hoteli hiyo, hivyo nilimuelekeza lakini akadai kwamba hajaelewa na kuniomba nimpeleke.
Kaka huelewi nini, kutoka hapa stendi ya mabasi, ongoza moja kwa moja barabara ya Newala utaikuta hoteli hiyo, ipo barabarani kabisa, nilimuambia.
Hapana, pamoja na kunielekeza vizuri itakuwa vizuri kama utanisindikiza, alisema kijana huyo.
Nilimuangalia na kuona kuwa alikuwa mtanashati na hakuwa mtu mbaya na kwa kuwa ilikuwa jioni ya saa kumi, sikuwa na
hofu ya kufanywa chochote na yule kijana.
Niliamua kumpeleka huku naye akiniomba nimsaidie kubeba mzigo wake wa begi dogo ambalo halikuwa zito baada ya
kumkubalia kumsaidia.
Njiani tulikuwa tukizungumza hili na lile na alitaka kujua jina langu, nikamuambia naitwa Salome.
Jina zuri sana kwa sababu hata mama yangu anaitwa jina hilo, alisema.
Kwani mama yako anaishi wapi?
Anaishi wilaya hiihii.
Wilaya ni kubwa taja sehemu.
Kijiji cha Nanyindwa.
Nakifahamu sana kijiji hicho.
Unakifahamu?
Ndiyo.
Ulifika pale kufanya nini?
Nilikuwa na rafiki yangu lakini siku hizi yupo Dar es Salaam. Nilikwenda kumtembelea wakati huo kabla hajahamishia makazi yake Dar.
Ahaa, anaitwa nani maana pale kijijini watu wote tunajuana.
Huwezi kumjua, kahamia Dar miaka mingi sana.
Nimekuambia kijiji kile kina watu wachache sana tunajuana nitajie jina nitamjua tu.
Anaitwa Roja Mchopa.
Namjua tena sana lakini mbona siku hizi karudi kijijini anajishughulisha na kilimo na biashara ndogondogo?
Usiniambie! Yupo kijijini Mchopa? Nilijua yupo Dar.
Kwa hiyo alipokuwa Dar uliwahi kumtembelea?
Nilimtembelea ndiyo, alikuwa akikaa Magomeni Mikumi na aliwahi kupiga muziki.
Kama ni muziki bado anaendelea nao, maana ana vyombo vya disco pale kijijini.
Mazungumzo kati yangu na kijana huyo yalikuwa marefu sana. Ni kweli alikuwa akijuana na baba huyo wa kijijini kwetu lakini kama alivyosema mwenyewe walionana muda mrefu mrefu, mwaka 1977.
Ahhh, nilipokuwa kijijini kwenu nilikuwa mdogo, mwaka 1977 nilikuwa na miaka kumi tu.
Unaitwa nani?
Ihopa Chinchi.
Ihopa Chinchi? Jina gumu, wewe mwenyeji wa wapi?
Kwetu ni Ndanda lakini babu zetu walihamia kutoka Msumbiji miaka mingi sana iliyopita. Kwani wewe una miaka mingapi?
Nina miaka 26.
Mwendo wa kutoka stendi ya mabasi Masasi mpaka Hoteli ya Wapiwapi ulikuwa mfupi maana hatukukodi Bajaj, badala yake tuliamua kutembea kwa miguu.
Baada ya kumfikisha katika hoteli hiyo aliulizia chumba lakini akaambiwa vyumba vilijaa. Ilibidi tugeuze na kwenda Masasi
Hoteli ambapo tulikutana na mzee David aliyekuwa akifanya kazi hotelini hapo.
Mzee huyu unamfahamu?
Mzee Daudi alimuangalia yule kijana akatikisa kichwa kuashiria hakumfahamu.
Anasema amewahi kukaa Kijiji cha Nanyindwa nikadhani utakuwa unamfahamu kwa kuwa umeishi sana kule.
Hapana, simfahamu.
Anasema alifikia kwa mzee Mchopa.
Mzee Mchopa nilikuwa namfahamu.
Kwa nini unasema ulikuwa unamfahamu kwani amehama huko kijijini? aliuliza.
Nimesema hivyo kwa sababu ameshafariki, miaka mingi.
Ooh jamani, kumbe huyo mzee hayupo duniani?
Ndiyo hivyo, katangulia nasi tupo nyuma yake, alisema David.
Mzee David alitufikisha katika chumba cha hoteli hiyo, ghorofa ya kwanza chumba namba saba. Tuliingia chumbani na kuweka mizigo yake. Mimi nilikuwa nimeketi kwenye kiti wakati yule mgeni anafikiri sanduku lake aliweke wapi. Baadaye akaamua kuliweka kwenye kabati.
Alisema nimsubiri kwani alikuwa anakwenda kujimwagia maji. Nilimuitikia kwa kichwa. Alichukua taulo na kuingia bafuni kwani katika chumba hicho choo na bafu vilikuwa humohumo.
Akiwa anaoga nilipenda kutafiti, nilikwenda kwenye sanduku lake nikaona kuna kifurushi kinatutumuka na kusinyaa kama vile kulikuwa na kitu ndani kinapumua.
Nilirudi haraka kwenye kiti changu huku moyo ukinidunda na kujiuliza mle ndani mlikuwa na kitu gani? Nilianza kutokwa na jasho jembamba.
Je, nini kitatokea? Mukiniwekea (Like) nitajuwa munaipenda na mimi nitaendelea na kuiweka hii hadithi
nzuri sana ya kusisimuwa musipo weka (Like) siwezi kuendelea na hadithi hii asanteni tuweni pamoja sote
kwenye hadithi hii tamu.