Macho ya Bundi

Macho ya Bundi

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2009
Posts
43,037
Reaction score
34,741
0705211152011owlhead_72_m.jpeg


NAITWA Salome Katonaga, ni mtoto wa kwanza kuzaliwa katika familia yetu ya watoto watano. Nimeamua kuwasimulia simulizi hii ili mfahamu kwa nini wahenga walisema dunia ni tambara bovu. Nitaeleza machache lakini ya kuhuzunisha sana ambayo nilifanyiwa na watu wenye roho mbaya.

Siku moja nikiwa katika pitapita yangu nilikutana na kijana mmoja ambaye aliniuliza ilipo Hoteli ya Wapiwapi mjini Masasi.

Nilikuwa naifahamu hoteli hiyo, hivyo nilimuelekeza lakini akadai kwamba hajaelewa na kuniomba nimpeleke.
“Kaka huelewi nini, kutoka hapa stendi ya mabasi, ongoza moja kwa moja barabara ya Newala utaikuta hoteli hiyo, ipo barabarani kabisa,” nilimuambia.

“Hapana, pamoja na kunielekeza vizuri itakuwa vizuri kama utanisindikiza,” alisema kijana huyo.

Nilimuangalia na kuona kuwa alikuwa mtanashati na hakuwa mtu mbaya na kwa kuwa ilikuwa jioni ya saa kumi, sikuwa na

hofu ya kufanywa chochote na yule kijana.

Niliamua kumpeleka huku naye akiniomba nimsaidie kubeba mzigo wake wa begi dogo ambalo halikuwa zito baada ya

kumkubalia kumsaidia.

Njiani tulikuwa tukizungumza hili na lile na alitaka kujua jina langu, nikamuambia naitwa Salome.

“Jina zuri sana kwa sababu hata mama yangu anaitwa jina hilo,” alisema.
“Kwani mama yako anaishi wapi?”
“Anaishi wilaya hiihii.”
“Wilaya ni kubwa taja sehemu.”
“Kijiji cha Nanyindwa.”
“Nakifahamu sana kijiji hicho.”
“Unakifahamu?”
“Ndiyo.”
“Ulifika pale kufanya nini?”

“Nilikuwa na rafiki yangu lakini siku hizi yupo Dar es Salaam. Nilikwenda kumtembelea wakati huo kabla hajahamishia makazi yake Dar.”
“Ahaa, anaitwa nani maana pale kijijini watu wote tunajuana.”
“Huwezi kumjua, kahamia Dar miaka mingi sana.”

“Nimekuambia kijiji kile kina watu wachache sana tunajuana nitajie jina nitamjua tu.”
“Anaitwa Roja Mchopa.”

“Namjua tena sana lakini mbona siku hizi karudi kijijini anajishughulisha na kilimo na biashara ndogondogo?”
“Usiniambie! Yupo kijijini Mchopa? Nilijua yupo Dar.”
“Kwa hiyo alipokuwa Dar uliwahi kumtembelea?”

“Nilimtembelea ndiyo, alikuwa akikaa Magomeni Mikumi na aliwahi kupiga muziki.”
“Kama ni muziki bado anaendelea nao, maana ana vyombo vya disco pale kijijini.”

Mazungumzo kati yangu na kijana huyo yalikuwa marefu sana. Ni kweli alikuwa akijuana na baba huyo wa kijijini kwetu lakini kama alivyosema mwenyewe walionana muda mrefu mrefu, mwaka 1977.

“Ahhh, nilipokuwa kijijini kwenu nilikuwa mdogo, mwaka 1977 nilikuwa na miaka kumi tu.”
“ Unaitwa nani?”
“Ihopa Chinchi.”
“Ihopa Chinchi? Jina gumu, wewe mwenyeji wa wapi?”

“Kwetu ni Ndanda lakini babu zetu walihamia kutoka Msumbiji miaka mingi sana iliyopita. Kwani wewe una miaka mingapi?”
“Nina miaka 26.”

Mwendo wa kutoka stendi ya mabasi Masasi mpaka Hoteli ya Wapiwapi ulikuwa mfupi maana hatukukodi Bajaj, badala yake tuliamua kutembea kwa miguu.

Baada ya kumfikisha katika hoteli hiyo aliulizia chumba lakini akaambiwa vyumba vilijaa. Ilibidi tugeuze na kwenda Masasi

Hoteli ambapo tulikutana na mzee David aliyekuwa akifanya kazi hotelini hapo.
“Mzee huyu unamfahamu?”

Mzee Daudi alimuangalia yule kijana akatikisa kichwa kuashiria hakumfahamu.
“Anasema amewahi kukaa Kijiji cha Nanyindwa nikadhani utakuwa unamfahamu kwa kuwa umeishi sana kule.”
“Hapana, simfahamu.”
“Anasema alifikia kwa mzee Mchopa.”

“Mzee Mchopa nilikuwa namfahamu.”
“Kwa nini unasema ulikuwa unamfahamu kwani amehama huko kijijini?” aliuliza.
“Nimesema hivyo kwa sababu ameshafariki, miaka mingi.”

“Ooh jamani, kumbe huyo mzee hayupo duniani?”
“Ndiyo hivyo, katangulia nasi tupo nyuma yake,” alisema David.

Mzee David alitufikisha katika chumba cha hoteli hiyo, ghorofa ya kwanza chumba namba saba. Tuliingia chumbani na kuweka mizigo yake. Mimi nilikuwa nimeketi kwenye kiti wakati yule mgeni anafikiri sanduku lake aliweke wapi. Baadaye akaamua kuliweka kwenye kabati.

Alisema nimsubiri kwani alikuwa anakwenda kujimwagia maji. Nilimuitikia kwa kichwa. Alichukua taulo na kuingia bafuni kwani katika chumba hicho choo na bafu vilikuwa humohumo.
Akiwa anaoga nilipenda kutafiti, nilikwenda kwenye sanduku lake nikaona kuna kifurushi kinatutumuka na kusinyaa kama vile kulikuwa na kitu ndani kinapumua.
Nilirudi haraka kwenye kiti changu huku moyo ukinidunda na kujiuliza mle ndani mlikuwa na kitu gani? Nilianza kutokwa na jasho jembamba.


Je, nini kitatokea? Mukiniwekea (Like) nitajuwa munaipenda na mimi nitaendelea na kuiweka hii hadithi

nzuri sana ya kusisimuwa musipo weka (Like) siwezi kuendelea na hadithi hii asanteni tuweni pamoja sote

kwenye hadithi hii tamu.
 
[h=1]Macho ya Bundi - 2-[/h]ILIPOISHIA
BAADA ya kuingia bafuni nilipenda kutafiti, nilikwenda kwenye sanduku lake nikaona kuna kifurushi kinatutumuka na kusinyaa kama vile kuna kitu kinapumua.
Nilirudi haraka kwenye kiti changu huku moyo ukinidunda na akili yangu ikijiuliza ni nini kile kinachopumua sandukuni? Nilianza kutokwa na jasho jembamba!
SONGA NAYO…


IHOPA Chinchi alitoka bafuni akiwa amejikausha. Alichukua suruali yake na kuingia tena bafuni ambako alivaa na kutoka akiwa nadhifu.
"Basi mimi naomba niondoke," nilimuambia.
"Ngoja basi tukapate chochote kitu hotelini."
"Hapana. Mimi nimeshiba."
"Ngoja basi nikutoe."
Bwana Chinchi alinitoa nje ya hoteni na akaniambia kuwa atanitafuta kwa simu kwa kuwa kuna jambo anataka kuniambia.
"Kwani ee…ee…" Nilisita.
Nilitamani kumuuliza kile ambacho kilikuwa kikipumua ndani ya sanduku lake lakini nilikuwa nilishindwa kwa kuwa angejua kuwa alipokuwa anaoga nilipekenyua mizigo yake.
"Inaonekana kama una jambo unataka kuniambia lakini unasita, uwe huru sema tu, usiwe na wasiwasi."
"Hapana, nitakuambia siku nyingine."
"Salome Ni nini? Mbona unanipa wasiwasi."
"Hapana nitakuambia siku nyingine," nilizidi kusisitiza.
Baadaye tuliagana name nikaenda kwetu Mtandi, nje kidogo ya mji wa Masasi.
Usiku ule sikulala kufikiria kile kilichokuwa kinapumua kwenye sanduku. Maswali yalikuwa mengi kuliko majibu. Nilijiuliza ama kuna kitoto kichanga? Lakini kama ni kitoto kichanga kwa nini muda wote huu hakikulia? Au ni kitu gani hasa?
Kwa kweli sikupata jibu sahihi na badala yake baada ya mawazo mengi nilijishitukia nikiwa nimepitiwa usingizi.
Asubuhi nilipigiwa simu na nilipoangalia kwenye skriini, sikujua ni nani aliyekuwa akipiga.
"Haloo."
"Haloo, hujambo salome Katonaga."
"Sijambo, nani mwenzangu?" nilihoji.
"Aaahh wewe Salome umenisahau? Jana hukumbuki kuwa ulinipeleka wapiwapi kisha Masasi Hoteli?"
"Nimekukumbuka." Nilitamani kuikata hiyo simu kwa kuwa sikutaka kuzungumza na yule mtu, hasa nilipokuwa nikifikiria kitu kilichokuwa kikipumua kwenye sanduku lake.
"Sasa naomba leo nikuone nikueleze kile ambacho nilitaka kukueleza jana." Akaniambia.
"Leo sina nafasi."
"Hapana, chukua Bajaj utarudi sasa hivi, nikueleze jambo halafu ukalifanyie kazi."
"Nipigie baada ya dakika ishirini au nusu saa nione kama kazi zangu zitakuwa zimeisha."
Akakata simu baada ya kunishukuru.
Nilikwenda moja kwa moja kwa rafiki yangu mpenzi Mei ili akanipe ushauri.
"Mei rafiki yangu, naomba unishauri jambo."
"Jambo gani tena?"
"Ni hadidhi ndefu kidogo, itabidi univumilie."
"Heee… makubwaa… nipe habari,"
Nilimsimulia mkasa wote wa jana kuhusu yule bwana na kisanduku chake chenye kitu kinachopumua.
"Sasa shoga itafaa nikuzindikize, maana watu wengine siyo wazuri, isije ikawa ni wachawi, wasije wakakutoa kafara bure."
"Sawa, tutaenda wote."
"Mtakuja kufa hivihivi shoga. Kwa nini ulikuwa laini na kukubali kuingia naye hadi chumbani? Kama ni hotelini si mlishafika?"
"Mtu mwenyewe nilimuamini baada ya kuniambia kuwa aliwahi kuishi kijijini kwetu na watu kadhaa anawafahamu kwa hiyo sikuwa na wasiwasi naye."
Simu inalia.
"Huyo mtu anapiga, nilimuambia apige baada ya nusu sasa,"
"Pokea muambie tunakuja."
"Haloo."
"Nimekaa zaidi ya nusu saa nimepiga sasa, utakuja?"
"Nakuja sasa hivi."
Kutoka Mtandi hadi hotelini kwake siyo mbali hasa kwa Bajaj. Nilifika nikiwa na rafiki yangu Mei.
"Karibuni." Alitukaribisha kwani tulimkuta akiwa nje ya mlango mkuu wa kuingilia hotelini.
Wakati tunaingia katika hoteli hiyo, tulikutana na mzee David, yule ambaye alitupokea jana na akatupatia chumba.
"Binti habari tangu jana."
"Nzuri sana mzee David, shikamoo."
"Marahaba, leo umekuja na kimwana, mtoto mzuri, lainiii," alisema na wote tukacheka.
"Mzee acha utani."
"Mgeni, naongopa?"
"Huongopi," alidakia Chinchi.
Tulikwenda kwenye meza moja na kukaa wote watatu. Chinchi alituambia tuagize tunachokitaka, tukafanya hivyo.
"Bwana Chinchi huyu ni rafiki yangu wa kufa na kuzikana, anaitwa Mei,"
"Mei, nafurahi kukufahamu."
"Huyu ni Bwana Chinchi, mgeni niliyekutananaye jana. Sasa mwaga habari."
"Hapana Salome. Nina jambo la siri nataka kukuambia. Tukiwa wawili tu. Jana uliniudhi sana, nisubirini napanda juu nakuja sasa hivi."
Salome alishangaa, "Au jana aligundua nimeona kitu kinachopumua sandukuni mwake?" alimuuliza mwenzake.


Je, Chinchi anakwenda kuchukua kitu gani na kwa nini wasiende wawili? Fuatilia

 
Back
Top Bottom