Mabosi zangu wananiandama bila sababu

Mabosi zangu wananiandama bila sababu

Moja kati ya law of power inasema "kamwe usijinyanyue ukaonekana una uwezo mkubwa na tushio kwa walio juu yako kicheo" maana hutofika mbali na utashindwa kutimiza ndoto zako, kwa maana lazima wakufanyie figisu tu....

Binadamu naturally tumeumbwa na wivu kwa maana tumeumbwa kwa mfano wake yule aliye mkuu na mwenye wivu, sasa wewe umejinyanyua na umeonekana tishio kwa walio juu yako, kwa mantiki hiyo umeshavunjwa law moja wapo ya power, hivyo lazima ukose power katika sehemu yako ya kazi....! Siku zote sehemu za kazi jitahidi usiwe na kundi wala usiwe mbinafsi kuwa mtu wa watu.....!

Act like a friend but ur a spy..! Jifanye mjinga usiejua kitu ila kumbe unakamata maboya hapo utadumu....! Usiruhusu adui yako ajue nguvu zako zilipo atakumaliza...

Then be humble man, usiwe mnoko, mjuaji, mjivuni na mbinafsi hata kama ni mchapa kazi kiasi gani utachemka tu
Ndugu yangu nazielewa sana 48 laws of power by Robert green
Sijajiinua,kamwe sina tabia hizo.
Ishu iko hivi,kuna wakati walinipa jukumu flan tena kwa maandishi wakidhan ntachemka, Mungu alivyo si athuman nikaperform kuzid hata lengo,ikawa talk of halmashauri na idara,nikapewa na zawadi kabisa ,wahusika wenyewe walishiriki kunipongeza kumbe ilikuwa roho zawauma.lol baada ya hapo nimekuwa nawindwa hadi naogopa.Na hilo jukumu walishaninyanga'nya But nashangaa bado wana mimi.
But ntaenda nao sawa la muhimu sifatilii cheo wala maslah ya mtu,zaidi Aliyenileta hapa atapigana kwa niaba yangu.
 
Thread nimeifunga rasmi.
Wacha aliyejuu ataamua hatma yetu and trust me ,hii idara haina mwaka itavunjwa yote.
 
Back
Top Bottom