Wadau mwaka mpya umeenza nami napenda kutoa maoni machache kuhusu jukwaa hili.
Zamani jukwaa hili lilikuwa ni sehemu nzuri sana ya kupata habari kuhusu nafasi mbali mbali za kazi, ilifikia hatua huna haja ya kununua magazeti iliupate kusoma nafasi za kazi kwani wadau walizibandika fasta kila watakapo ziona.
Lakini sasa hali imekuwa tofauti kabisa hatubandiki tena nafasi isipokuwa tunaomba nafasi,
Utakuta mtu anaanzisha post inasema "Nafasi ya kazi" ukufungua ndani unakuta yeye ndio anaomba atafutiwe kazi, na hii imelifanya jukwaa kuwa la blah blah na kupoteza ile credibility yake kama source ya kupata matangazo ya kazi.
Sipingi watu kuomba wasaidiwe kazi ila wito wangu kwenu ni kuwa iwapo kila mdau ataona nafasi sehemu na kujitahidi kuibandika humu kama ilivyokuwa awali naamini wengi watafaidika kwani nafasi zitakuwa nyingi kuliko ilivyo sasa.
Ntakuwa mchoyo wa fadhila kama sita lishukuru jukwaa hili kusaidia kumpatia ajira mdogo wangu, hivyo natambua umuhimu wake.
Tubadilike
Zamani jukwaa hili lilikuwa ni sehemu nzuri sana ya kupata habari kuhusu nafasi mbali mbali za kazi, ilifikia hatua huna haja ya kununua magazeti iliupate kusoma nafasi za kazi kwani wadau walizibandika fasta kila watakapo ziona.
Lakini sasa hali imekuwa tofauti kabisa hatubandiki tena nafasi isipokuwa tunaomba nafasi,
Utakuta mtu anaanzisha post inasema "Nafasi ya kazi" ukufungua ndani unakuta yeye ndio anaomba atafutiwe kazi, na hii imelifanya jukwaa kuwa la blah blah na kupoteza ile credibility yake kama source ya kupata matangazo ya kazi.
Sipingi watu kuomba wasaidiwe kazi ila wito wangu kwenu ni kuwa iwapo kila mdau ataona nafasi sehemu na kujitahidi kuibandika humu kama ilivyokuwa awali naamini wengi watafaidika kwani nafasi zitakuwa nyingi kuliko ilivyo sasa.
Ntakuwa mchoyo wa fadhila kama sita lishukuru jukwaa hili kusaidia kumpatia ajira mdogo wangu, hivyo natambua umuhimu wake.
Tubadilike