Mpogoro
JF-Expert Member
- Dec 7, 2008
- 386
- 58
Ndugu zetu wabeba box wa Diaspora...please assist...haya mambo si sawa jamani!
Mabondia wapokezana kilinda ulimi
Thursday, 13 May 2010 22:04 0diggsdigg
Imani Makongoro
'UKISTAJABU ya Musa utaona ya filauni' ndio iliyokuwa kwenye kambi ya timu ya ya taifa ya ngumi za ridhaa ambako mabondia wake walilazimika kubadilisha kilinda ulimi wakati wa mazoezi ya kujiandaa na michuano ya jumuia ya Madola.
Kambi ya mabondia hao inatarajia kuanza mazoezi Jumatatu kwenye Uwanja wa Ndani wa taifa jijini Dar es Salaam, huku Shirikisho la mchezo huo nchini (BFT) ikikabiliwa na ukata.
Ukata huo ulisababisha mabondia hao kukosa vifaa muhimu vya mazoezi kama vikinga ulimi ambavyo kwa kawaida bondia uweka mdomoni kabla ya kupigana ili kumlinda na tatizo la kujing'ata ulimi alipokuwa ulingoni.
Lakini kutokana na ukata mkubwa iliyoikumba kambi hiyo mabondia watatu walilazimika kutumia kilinda ulimi kimoja kwa kupokeza kila wanaposhuka ulingoni.
Pembeni ya ulingo kuliwekwa maji kwa ajili ya kusuuzia kilinda ulimi hicho kabla ya kubadilishana mara baada ya mabondia waliokuwa ulingoni kushuka ili kuwapa nafasi wengine kupimana ubavu.
Mbali na kukosa vifaa hivyo pia dawa, maji, Vikinga vichwa na Gloves kwa mabondia hao ilikuwa ni tatizo kubwa kiasi cha kufanya mazoezi bila kuwa na vifaa hivyo.
Hivi karibuni mabondia hao walialikwa kushiriki mashindano ya kupimana ubavu kati ya wenzao wa nchini Burundi, lakini ilishindikana baada ya BFT kukosa shilingi milioni 7 kwa ajili ya kusafirisha mabondia nane na matumizi mengine nchini humo.
Katibu Mkuu wa BFT, Makore Mashaga, aliiambia Mwananchi hivi karibuni kuwa wanaendelea na mchakato wa kutafuta wadhamini ili kuweza kuisaidia timu hiyo ambayo inakabiliwa na ukata.
Alisema kuwa ili kuwa na timu imara basi jitihada zinahitajika ili kuweza kulifanikisha hilo na wanaimani wakipata mfadhili hata mmoja kikosi cha mabondia hao kitafanya maajabu kimataifa.
"Ingawa tunakabiliwa na ukata, lakini mabondia wetu hawakati tamaa kwa kweli wanajitahidi endapo tukipata mfadhili ambaye atatusaidi tunaimani tutafika mbali na tutarejesha heshima ya taifa katika mchezo huo Kimataifa" alisema Makore.
Ukata huo umesababisha mabondia hao kabla ya kupewa likizo kuweka kambi ya wazi na kushindwa kuweka kambi ya kudumu wakati wakijiandaa kushiriki katika michezo ya Jumuiya ya Madola mwezi Oktoba mjini New Dehli, India.
Mabondia wapokezana kilinda ulimi
Thursday, 13 May 2010 22:04 0diggsdigg
Imani Makongoro
'UKISTAJABU ya Musa utaona ya filauni' ndio iliyokuwa kwenye kambi ya timu ya ya taifa ya ngumi za ridhaa ambako mabondia wake walilazimika kubadilisha kilinda ulimi wakati wa mazoezi ya kujiandaa na michuano ya jumuia ya Madola.
Kambi ya mabondia hao inatarajia kuanza mazoezi Jumatatu kwenye Uwanja wa Ndani wa taifa jijini Dar es Salaam, huku Shirikisho la mchezo huo nchini (BFT) ikikabiliwa na ukata.
Ukata huo ulisababisha mabondia hao kukosa vifaa muhimu vya mazoezi kama vikinga ulimi ambavyo kwa kawaida bondia uweka mdomoni kabla ya kupigana ili kumlinda na tatizo la kujing'ata ulimi alipokuwa ulingoni.
Lakini kutokana na ukata mkubwa iliyoikumba kambi hiyo mabondia watatu walilazimika kutumia kilinda ulimi kimoja kwa kupokeza kila wanaposhuka ulingoni.
Pembeni ya ulingo kuliwekwa maji kwa ajili ya kusuuzia kilinda ulimi hicho kabla ya kubadilishana mara baada ya mabondia waliokuwa ulingoni kushuka ili kuwapa nafasi wengine kupimana ubavu.
Mbali na kukosa vifaa hivyo pia dawa, maji, Vikinga vichwa na Gloves kwa mabondia hao ilikuwa ni tatizo kubwa kiasi cha kufanya mazoezi bila kuwa na vifaa hivyo.
Hivi karibuni mabondia hao walialikwa kushiriki mashindano ya kupimana ubavu kati ya wenzao wa nchini Burundi, lakini ilishindikana baada ya BFT kukosa shilingi milioni 7 kwa ajili ya kusafirisha mabondia nane na matumizi mengine nchini humo.
Katibu Mkuu wa BFT, Makore Mashaga, aliiambia Mwananchi hivi karibuni kuwa wanaendelea na mchakato wa kutafuta wadhamini ili kuweza kuisaidia timu hiyo ambayo inakabiliwa na ukata.
Alisema kuwa ili kuwa na timu imara basi jitihada zinahitajika ili kuweza kulifanikisha hilo na wanaimani wakipata mfadhili hata mmoja kikosi cha mabondia hao kitafanya maajabu kimataifa.
"Ingawa tunakabiliwa na ukata, lakini mabondia wetu hawakati tamaa kwa kweli wanajitahidi endapo tukipata mfadhili ambaye atatusaidi tunaimani tutafika mbali na tutarejesha heshima ya taifa katika mchezo huo Kimataifa" alisema Makore.
Ukata huo umesababisha mabondia hao kabla ya kupewa likizo kuweka kambi ya wazi na kushindwa kuweka kambi ya kudumu wakati wakijiandaa kushiriki katika michezo ya Jumuiya ya Madola mwezi Oktoba mjini New Dehli, India.