Mabomu yarindima Karatu kisa Rose Mhando

Mabomu yarindima Karatu kisa Rose Mhando

Tanzanite klm

JF-Expert Member
Joined
May 7, 2013
Posts
478
Reaction score
411
Hivi sasa polisi wanalipua mabomu ya machozi kutawanya raia walio kuwa kwenye uwanja wa mazingira bora karatu ambao walitoa pesa zao kumtazama Rose Muhando.

Rose amesababisha vurugu kwa sababu alikuwa aje kwenye show alafu hakuja na watu walikuwa wametoa pesa zao na uwanja ulikuwa umefurika sana watu.

Kulikuwepo na wachungaji maaskofu wa TAG na watu wengine wengi fans wa Rose Mhando,lakini mpaka saa kumi na mbili Rose alipopigiwa simu alikuwa hapokei tena.

Na wiki moja nzima mji wa Karatu ulijaa matangazo ya Rose Mhando.

Rose kama ni kweli ulishalipwa pesa za show alafu hukuja sijui damu iliyomwagika utalipaje.

Watu wanadai warudishiwe hela zao na kudai wametapeliwa na mwinjilisti.
 
Dah Rose Muhando anatakiwa ajirekebishe kazidi sna kuingia "mitini" kila akialikwa......
 
Nibebe, nibebe nibebe nibeeee, mgembeba ndo angeingia uwanjani.sasa wana- karatu mnataka age peke yake wakati ashasema anataka mmbebe
 
Inatia uchungu sana pale wachungaji,askofu na wainjilisti wanapo dhalilishwa na kutukanwa na kuzomewa na watu wengi.eti kisa tuu Rose mhando kaingia mitini,na pay slip zinaonyesha kaingiziwa milioni tatu kwenye akaunti yake tayari.
Sijui mwisho wake Rose utakuwaje,hata mimi mwenyewe nimeumia sana na kuanzia leo sitanunua wala kusikiliza kazi zake.
 
Kumbe kwenye injili kuna kula eeh,
 
Au ni dau dogo kapewa.jaman pesa isiwe mbele sana kuliko huduma.umepokea bure toa bure
 
Hawa wachungaji washakua wezi. Mwezi uliopita walitangaza kuwa Rehan Bonkeh atakuwepo Jangwani. Vyombo vyote vya habari vilitangaza ivyo, tukajaa Jagwani afu jamaa hakutokea hata nusu.
 
Back
Top Bottom